inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 29 Juni 2013

HABARI: RAIS OBAMA AKIWA AFRIKA KUSINI...MAANDALIZI YANAENDELEA...



Mafundi wa mabango wakiwa kazini majira ya saa 9.00 mchana (Picha na Jielimishe Kwanza!)

Muonekano wa mabango yenye picha ya Rais Barack Obama katikati ya viunga vya barabara ya Ubungo-Mwenge.      (Picha na Jielimishe Kwanza!)

HABARI:UJIO WA RAIS OBAMA TANZANIA..MAANDALIZI YANAENDELEA...



Mafundi wa mabango wakiwa kazini majira ya saa 9.00 mchana (Picha na Jielimishe Kwanza!)

Muonekano wa mabango yenye picha ya Rais Barack Obama katikati ya viunga vya barabara ya Ubungo-Mwenge.      (Picha na Jielimishe Kwanza!)

Ijumaa, 28 Juni 2013

MICHEZO: NINI UTABIRI WAKO JUMAPILI HII WA FAINALI KATI YA BRAZIL NA UHISPANIA?





Vs

MICHEZO:HISPANIA YAIONDOA ITALIA KWA "MATUTA" HAPO JANA...TAZAMA MATUTA YALIVYOKUWA!



BOFYA KIUNGANISHI UONE PENATI 14  "LIVE" KUPITIA:

JAMII NA MAWASILIANO: HIVI NDIVYO SIMU ZA MIKONONI ZINAVYOTUTENGA…


Mfumuko wa Teknolojia ya mawasiliano na upatikanaji wa simu za viganjani kirahisi hasa zenye intaneti zimetufikisha hapa tulipo. Si kwa lengo baya bali jema kabisa endapo tutakuwa na mipaka ya matumizi na kuchagua vitu muhimu vya kuangalia tukizingatia kutunza wakati.
Tukiendekeza sana urafiki na simu ya mkononi kwa kuchati…tutajikuta tupo mbali na eneo halisi tulipo.Hii ni hatari, kwa sababu itamfanya mtu asijue kitu kinachoendelea jirani yake na wakati huo huo akiwa makini na mambo ya mbali.
Mfano: mtu anakata mazungumzo na mtu aliye naye jirani na kujikita na mawasiliano ya anga hivyo kushindwa kutimiza lengo la kuwa jirani.
Hivi sasa, ndani ya familia kumekuwa na migogoro mingi inayosababishwa na kuendekeza matumizi ya simu kupita kiasi.Wazazi hawaongei na watoto kuhusu malezi na kumwachia mwalimu aitwae “Teknolojia ya Habari na Mawasiliano-TEHAMA” afanye kazi yake.
Nikirejea makala yangu kuhusu umuhimu wa TEHAMA kwa wanafunzi kujifunza ya Jumatano,19 Juni 2013-http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/06/elimu_19.html.Ni vizuri kumtumia mwalimu huyu, lakini tujue fika kuwa anafundisha kila kitu; mema na mabaya kama hakuna uangalizi wa kutosha na uelimishaji sahihi wa matumizi ya teknolojia hii.

Kuthibitisha ukweli wa jambo hili, tazama video ifuatayo;
Hili ni angalizo tu, naomba nisieleweke vibaya…hii ndiyo hali halisi inayoendelea siku hadi siku.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Alhamisi, 27 Juni 2013

HABARI MUHIMU: HIVI NDIVYO OBAMA ALIVYOINGIA NCHINI SENEGALI...





Tumefika salama...Raisi Obama akiwa amemshika mkono binti yake Sasha na familia yake walipokuwa wakishuka kwenye "Air Force One" katika ardhi ya Dakar-Senegali jana jioni.(Picha na http://www.dailymail.co.uk/news/article)
Ndege waliyosafiria ijulikanayo kama “Air Force One” imegusa ardhi ya mji mkuu wa Senegali-Dakar siku ya Jumatano jioni.Raisi Obama na familia yake wanatarajia kuendelea na ziara yao nchini Afrika Kusini na Tanzania.
 Karibu Tanzania!
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Jumatano, 26 Juni 2013

MTAZAMO: JIFUNZE KUWA NA MTAZAMO CHANYA!



Picha na www.narconon.co

  Habari!

Naomba niwakaribishe tena katika ukumbi huu kuhusu “MTAZAMO”.Wiki iliyopita niliandika makala kuhusu MADHARA YA KUWA NA MTAZAMO HASI…












ISOME HAPA:  http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/06/epuka-kuwa-na-mtazamohasi-picha-na.html

Mwishoni niliahidi kukuletea mbinu za kumfanya mtu kuwa na mtazamo chanya. Karibu tena leo kuzifahamu mbinu hizo.


Awali ya yote ni vyema tukafahamu faida za kuwa na mtazamo chanya;

·   Ni njia nzuri kiafya ya kuepukana na hatari ya kupatawa na magonjwa ya moyo, pia huchochea kinga ya mwili

·      kujiongezea uwezo wa kutatua matatizo

·      ni rahisi kwa watu wenye mtazamo chanya kupambana na msongo wa mawazo

·    mtazamo chanya huvuta vitu chanya-hii ni sambamba na kufungua milango ya mafanikio katika maisha

·     Katika hali ya muonekano wa kwanza, mtazamo chanya utakufanya ukubalike na watu


Zifuatazo ni mbinu zinazoweza kumjengea mtu uwezo wa kuwa na mtazamo chanya na wenye tija;

1.TUMIA LUGHA ILIYO CHANYA- USISEME “SIWEZI KUPATA”…SEMA “NITAPATAJE?”…
Mjasiriamali maarufu na mwandishi wa vitabu aliyebobea nchini Marekani-Robert Kiyosaki anatoa mtazamo huo katika hali ya swali “NITAPATAJE?” akimaanisha kuwa swali hili litaubidisha ubongo kufikiri njia mbadala za kupata suluhisho la tatizo.
Anapingana na usemi wa kwanza ulio katika sentensi kamili “SIWEZI KUPATA” akimaanisha kuwa mtazamo huu hasi unamfanya mtu kuwa mvivu wa kufikiri.

Anasisitiza kwa kusema kujiuliza maswali ni njia moja wapo ya kuupa ubongo mazoezi na kuuongezea uwezo wa kufikiri, na mwisho wa yote ni kupata mafanikio tarajiwa.



2.EPUKA KUELEZA MALENGO YAKO KWA KILA MTU…UTAKATISHWA TAMAA!

Jifunze kuchagua mrafiki wa kuwaeleza malengo yako…kuwa makini sana! Wapo wengine kazi yao ni kukukatisha tamaa.Ukitaka kuwajua mtazamo wao, sikiliza maneno yao.
Angalizo: wapo watu watakaotaka kuboresha wazo/lengo lako kwa lugha ya kuonyesha ufanye marekebisho au maboresho, usiwabeze...chukulia hiyo kama changamoto kusonga mbele na kufanya vizuri zaidi.



 3.JIFUNZE NA UFANYIE KAZI ULIYOJIFUNZA UKIWA NA MTAZAMO CHANYA
Katika maisha ya kila siku tunajifunza kwa njia moja au nyingine…jukumu letu ni kuchagua kujifunza mema au mabaya.Nikizungumizia kuhusu kujifunza mema na yote yanayojenga ni vyema kuyafanyia kazi kwa vitendo tukitegemea majibu chanya.Kadri utavyokuwa ukipima mafanikio ya utendaji ndivyo unavyozidi kujiimarisha zaidi katika kuwa na mtazamo chanya.


4. JIWEKEE MALENGO KWA MAANDISHI

Ni kitu cha muhimu kuweka malengo-yanaweza kuwa ya muda mfupi au mrefu.Mara nyingi malengo ya muda mfupi hutupa ari ya kuyakaribia malengo ya muda mrefu, pia ni sehemu ya kutuepusha kukata tamaa tukiwa katika safari ya kuelekea kwenye malengo ya muda mrefu.Kipimo cha mafanikio ya malengo yako kitaweza kuboresha uwezo wako wa kuwa na mtazamo chanya.


5.JIHUSISHE NA WATU WENYE MATEGEMEO CHANYA

Kujihusisha na watu wenye mtazamo chanya kutakuongezea uwezo wako wa mategemeo chanya katika mambo unayofanya.Pia watakupa ari ya kusonga mbele kimawazo na kiutendaji.


6.FAHAMU FAIDA ZA KUWA NA MTAZAMO CHANYA

Ukifahamu faida za kuwa na mtazamo chanya utajibidisha kufikia lengo la kuwa na mategemeo chanya.


7.JIWEKEE MPANGO WA KUEPUKA KUWA NA MTAZAMO HASI

Panga utaratibu ulio kwa vitendo kuepukana na mtazamo hasi.Kwa kufanya hivyo, mtazamo chanya utazidi kujijenga siku hadi siku.


8.TAMBUA NA UPAMBANE NA MAWAZO HASI

Kuna msemo unasema, kulijua tatizo ni njia mojawapo ya kuoambana na tatizo au kumfahamu adui ni njia nzuri ya kuanza kupambana naye.Jaribu kujichunguza utagundua ni kwa kiasi gani au mara ngapi umekuwa na mtazamo hasi hata kwa vitu vilivyo kwenye uwezo wako?


9.JARIBU KUFANYA VITU VIPYA

Unapokuwa na uthubutu wa kutenda vitu vipya ni njia ya kujiongezea ujasiri na kuimarisha mtazamo chanya wa kufikiri.Usiogope kufanya makosa, hayo yanakuwa ni ishara ya kukuboreshea utendaji wako kwa kujifunza.


10.JISOMEE VITABU NA MAJARIDA

Kupitia vitabu na majarida utajifunza mambo mengi kuhusu kujiimarisha katika mtazamo wa kufikiri hasa ukilinganisha na wako.Ukitendea kazi mbinu mbali mbali zilizotolewa zitakuongezea uwezo wa kuwa na mtazamo chanya siku hadi siku.


11.SIKILIZA HOTUBA NA MAFUNDISHO YENYE KUIMARISHA

Kusikiza hotuba na mafundisho yenye kuimarisha ukiwa kwenye gari au nyumbani ni njia nzuri kujiongezea uwezo wa kuwa na mtazamo chanya.Kupitia hao utajifunza mbinu walizopitia kufikia malengo yao.
Tuma maoni kupitia:jielimishekwanza@gmail.com
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!






Jumanne, 25 Juni 2013

NUKUU MAARUFU YA LEO: KUONDOKANA NA UMASIKINI...


 
Nelson Mandela(Picha na www.guardian.co.uk)
"Kuondokana na umasikini si suala la kutoa msaada wa pesa,ni suala la kutenda haki.Kama ilivyo kwa utumwa na ubaguzi wa rangi,umasikini si wa asili.Unatengenezwa na mtu na unaweza kuondoshwa kupitia matendo ya wanadamu."-NELSON MANDELA.

Jumapili, 23 Juni 2013

FAMILIA: UGOMVI WA WAZAZI… WATOTO KUKOSA MUELEKEO!


Malezi bora ya watoto huchangiwa na ushirikiano wa pamoja wa baba na mama.Kisaikolojia, mtoto hujengeka na kuwa na furaha kutokana na kuwepo kwa furaha na upendo wa wazazi.


Ifahamike kuwa muunganiko wa wazazi kwa ndoa au la unaimarika zaidi kwa kuwepo na mtoto/watoto. Licha ya kuwepo na tofauti za hapa na pale ndani ya wapendanao lakini haitakiwi watoto wajue tofauti zilizopo.


Picha imetolewa:www.ehow.com
Ugomvi wa aina yoyote ile unatakiwa kupata usuluhishi wa watu wawili(baba na mama) kama walivyoanza wakiwa chumbani…watoto/mtoto hawapaswi kujua kinachoendelea isipokuwa wawaone wazazi wakipendana na kuona furaha ikitawala ndani ya familia.


Hali ikizidi kuwa mbaya, basi usuluhisi unaweza kufikishwa katika ngazi nyingine za usuluhishi kama viongozi wa dini,wazee wa familia na ngazi nyingine zinazofaa.


Katika jamii zetu tunazoishi, hasa kwa kipindi hiki kumekuwa na tabia iliyozoeleka kwa wazazi kugombana mara kwa mara na kufikia hatua ya kutengana kwa sababu wanazojijua bila ya kujali kuwa wamezaa watoto.


Madhara ayapatayo mtoto kwa wazazi kugombana na kutengana

Hapa nitatoa baadhi ya madhara yanayoonekana kirahisi ayapatayo mtoto/watoto kwa wazazi kugombana na kutengana kwa talaka au njia nyingine;

  •  Mtoto anaweza kujengeka na tabia ya ugomvi-hii ni elimu ya awali kabisa kutoka kwa wazazi wake
  • Suala la wazazi kutengana linaweza kuwafanya watoto kuwa njia panda-waende kwa mama au baba kwa sababu hawana chuki na wazazi wao(wanawapenda wote).Endapo wataenda na kukubaliana na mawazo ya mzazi mmoja, mwingine anakasirika na kusema watoto wa siku hizi wanadharau wazazi wao.

  • Mtoto anaweza kuondoka nyumbani  na kuamua kuishi maisha yake kwa sababu upendo umetoweka nyumbani.Hili humuweka mtoto kuwa huru kufanya lolote kwa sababu ushirikiano wa kumlea umevunjika.Pia ni kichocheo kikubwa cha ongezeko la watoto wa mitaani/watoto waishio kwenye mazingira magumu

  • Mtoto anaweza kupoteza muelekeo kimasomo, hii ni sambamba na kushuka kwa taaluma yake au kuacha shule kabisa

  • Mtoto anaweza kupatwa na msongo wa mawazo ulio juu ya uwezo wake, hivyo kupoteza furaha na kuwa mnyonge


Tukilitazama jambo hili kwa upande wa pili; kuna wakati kutengana kwa wazazi kunaweza kuwa na faida kwa pande zote (mzazi mmoja na watoto).


Kama alivyoainisha mtaalamu wa masuala ya talaka, divorce Judith Wallerstein  kuwa ni jambo la busara kutengana kwa talaka endapo watoto watapata mateso ya kihisia,kupigwa au kunyanyaswa kijinsia na mzazi mmoja, au mzazi mmoja anapokuwa mlevi kupindukia na kusahau majukumu ya familia.


Jamii na wanandoa kwa ujumla tujitaidi kudumisha mahusiano ili tuwalee watoto kwa pamoja hivyo kuepusha ongezeko la watoto wasiokuwa na muelekeo, pia watoto wa mitaani.

Imetolewa na

Jielimishe Kwanza!




Jumamosi, 22 Juni 2013

UBUNIFU: HUDUMA YA INTANETI BILA MALIPO NDANI YA “MATHREE” NCHINI KENYA…



 

Picha na http://www.bbc.co.uk/swahili: Daladala nchini Kenya, alimaharufu hujulikana kama "Mathree au Matatu"
Kutokana na adha ya foleni jijini Nairobi nchini Kenya, wafanyabiashara wa “Mathree” au “Matatu” wabuni njia mpya iliyo sanjari na matumizi ya intaneti ili kuwapoza abiria na kuboreka.


Abiria akiwa ndani ya “Mathree” au “Matatu” anaweza kusoma barua pepe pia kusoma habari kupitia mitandao mbalimbali.

Huduma hii imewavuta abiria wengi kukimbilia "Mathree" zenye "wiFi".

Sikiliza ushuhuda wa abiria kupitia:

Ijumaa, 21 Juni 2013

MTAZAMO: EPUKA KUWA NA MTAZAMO HASI…


Picha na hot100tips.com
Mara kwa mara watu wamekuwa na manung’uniko yaliyo sanjali na hali ngumu ya maisha.Hii imewafanya wengi kukosa muelekeo na mwishowe kukata tamaa, hasa waonapo wengine wakitesa na maisha.
Watu wamesongwa na kulaumu huku wakitumia muda mwingi kusononeka bila kuchukua hatua ya kufikiri tofauti.Ijulikane kuwa jinsi utumiavyo muda mrefu kusononeka na kunung’unika ndivyo unavyojiweka kwenye nafasi kubwa ya kupoteza fursa nyeti za kukutoa kimaisha.
Yafuatayo ni baadhi tu ya madhara ya kuwa na mtazamo hasi wa maisha;
  •       Utajiona huwezi kila kitu
  •      Utakuwa msindikizaji wa maamuzi ya watu, hutaamini maamuzi yako
  •     Utatofautiana na watu wenye mafanikio kifedha mfano; utachulia watu wote wenye fedha ni wezi ,mafisadi, na washirikina.  
Mwandishi maarufu, mfanyabiashara mkubwa nchini Marekani – Robert Kiyosaki
aliwahi kusema;  
“what you think it’s real, becomes your reality”  kwa lugha ya Kiswahili-  “unachofikiri ni halisi kinakuwa uhalisia wako”akitoa mfano kuwa mtu akisema siwezi kuwa tajiri, mtazamo huu huwa halisi kwake kwa sababu hatakuwa na juhudi zozote za kumpeleka hatua ya kuwa tajiri.
  •        Utapoteza fursa nyingi za kukutoa kimaisha
  •      Kukosa ujasiri na uthubutu wenye tija mfano mtu anaweza kusema “nikijaribu kufanya biashara hii nitapata hasara…anaweka uhakika wa kupata hasara kabla ya kuanza biashara yenyewe, hivyo kutothubutu.
Wakati mwingine nitajitahidi kukuletea mbinu za kuwa na matazamo chanya. “JIFUNZE KUWA NA MTAZAMO CHANYA.” Ukitumia mbinu hizo zitakubadilisha sana, hutakuwa kama ulivyokuwa.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!


Jumatano, 19 Juni 2013

ELIMU: MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO (TEHAMA) KUJIFUNZIA NI SULUHISHO LA ELIMU BORA TANZANIA…




Kufuatia mapinduzi makubwa ya Sayansi na Teknolojia nchini na duniani kwa ujumla mambo mengi yamerahisishwa sana.


Wakati huo huo, uzuri wa Teknolojia unaweza kuleta hasara endapo hakutakuwa na uelewa sahihi wa matumizi.Mfano halisi ni matumizi ya Intaneti kupitia simu za viganjani.Nilitegemea, hii ingekuwa ni fursa kwetu watanzania kuwasaidia watoto wetu kujifunza kwa kupata maarifa kupitia njia hiyo…kinyume chake wanajamii wanatumia intaneti “kuchat” na masuala yanayowahusu, pia kupitia mitandao ya kijamii kwa mambo yasiyojenga. 


Wakati huo huo wanasema walimu hawatoshi na hawafundishi…je umewahi kuchukua jitihada kutafuta njia mbadala? au tunasubiri majibu ya mwisho ya mtihani yatolewe ndiyo tushike vichwa na kutoa lawama kwa Serikali na walimu wake?


Hapa inatakiwa ieleweke kuwa mafanikio ya watoto wetu yanaanzia na sisi wazazi/walezi ikiwa sambamba na watoto wenyewe kujitambua na kutii.


Naomba niwathibitishie kuwa kwa hatua tuliyofikia kimawasiliano na teknolojia ya intaneti kupitia simu zetu, hakuna kitu kisichokosekana mtandaoni kuhusiana na masomo ya watoto wetu. Kuna mwalimu anaitwa Google, You tube…tuanze kuwatumia.


Cha msingi ni kumnunulia mwanafunzi muongozo wa kila somo”syllabus” na kusimamia kujifunza.Shule inakuwa ni sehemu ya kwenda kuuliza maeneo asiyoelewa na kufanya mazoezi kujifua na kile alichojifunza.


Inafika hatua nashangaa sana kuona teknolojia inabadilika kwa kasi na watu wanaipokea kwa kasi kinyume na matumizi hasa kwenye nyanja hii nyeti ya kujielimisha.


Si kitu cha ajabu kumuona kijana/mwanafunzi anatumia tabiti “tablet” kusikilizia muziki, kuchati na marafiki na kutazama sinema…ukimuuliza maswali kuhusu masomo ya shuleni anakujibu mwalimu hajafundisha bado.Hivi, tutamtegea mwalimu kwa asilimia 100% hadi lini? 

Hili linachangia  kwa asilimia nyingi idadi kubwa ya wanafunzi wa sekondari kufeli na wale walio vyuo vikuu kukosa mbinu za utendaji katika soko la ajira. Bila shaka unauona mwelekeo wa jahazi la elimu ya Tanzania…huna haja ya kuwa na Shahada ya uzamili(Masters) au ile ya uzamivu(PhD) ili kujua hatima yake.


Nikiendelea sana, watu watasema nawapangia matumizi ya simu na tabiti au komputa zao.Lakini uhalisia ndiyo huo.Tunatakiwa kubadilika ili kulikomboa jahazi la elimu ya Tanzania.


Ukiwa ni mzazi/mlezi mwenye mapenzi mema na unataka kumuandaa mwanao kusoma kuendana na teknolojia ya habari na mawasialino, pia usiyetaka mizigo isiyo ya lazima hapo baadaye, chukua hatua sasa kumsaidia mwanao kielimu na kujitambua kabla maji hayajamwagika!

Unaweza kuwasiliana  Jielimishe Kwanza! kwa ushauri zaidi.


Simu ya kiganjani: +255 754 572 143

Barua pepe: jielimishekwanza@gmail.com

Imetolewa na Jielimishe Kwanza!

Jumanne, 18 Juni 2013

UONGOZI BORA: HII NI SIRI KUBWA YA VIONGOZI WALIOFANIKIWA…

Raisi,(1994-1999), Mwanamapinduzi,Mpigania haki kuhusu ubaguzi wa rangi wa Afrika Kusini-Nelson Mandela.         (Picha na www.newstimeafrica.com). Picha hii imewekwa kwa kuthamini mchango wake, ni mfano wa kiongozi bora wa kuigwa, pia kumtakia heri.

Wataalam wa masuala ya uongozi wamekuwa wakijiuliza swali lifuatalo mara nyingi; viongozi huzaliwa au hutengenezwa? Ikimaanisha-ni mtu tu anajikuta kazaliwa ana uwezo wa kuongoza au anafundishwa kuwa kiongozi?

Mtazamo wa wengi ni kuwa viongozi wanazaliwa…ni kipaji tu cha mtu cha kuzaliwa nacho.Yaani, wakichukulia kuwa tangu kipindi cha utoto utaiona tabia ya mtoto akiwaongoza wenzake katika michezo ya kitoto.

Pia, kiasilia kunapokuwa na watu zaidi ya wawili na wanahitaji kutoa maamuzi ya pamoja utaona kuwa mmoja hujiweka kipaumbele katika kutoa maamuzi na anakubalika.

Mwandishi maarufu, Stephen R.Covey katika kitabu chake cha “The 8th Habit- From Effectiveness to Greatness” anapingana na mawazo ya wengi kwa kuweka msimamo hasi…akimaanisha kuwa viongozi hawazaliwi wala hawatengenezwi ila mazingira huwafundisha na kuwalea.

Akiunganisha na wazo la uwezo wa asili wa mwanadamu…Stephen anasema; "kikawaida mwanadamu ana nguvu ya asili ya kufanya chaguo."

Hivyo basi, akasiliba kwa kusema "viongozi hujitengeneza kwa kuchagua wenyewe", na endapo watafuata kanuni na kujiongezea nidhamu dhabiti, uhuru wao wa kuchagua huongezeka.
Akithibitisha ukweli wa wazo lake Stephen kwa kulinganisha na wazo la Dk.Noel Tichy ambaye alisema;viongozi hawazaliwi ila hufundishwa…Stephen anaunganisha mawazo kwa kusema; watu hutumia nguvu yao ya kuchagua kujifunza na kufuata mafunzo.

Tukifuatilia kwa makini orodha ya viongozi wenye mafanikio duniani ni kubwa.Nikisema nianze kumjadili mmoja hadi mwingine itachukua muda mrefu sana bila ya kumaliza.Ila viongozi wote hawa walikuwa na tabia/wana tabia za kipekee na zinazofanana ambazo ni;
1.   Kuwa na maono”vision” ya mbali yenye tija na kuyafanyia utekelezaji, ambayo wengine (wafuasi) hawayaoni. Mtaalamu wa masuala ya uongozi na mwandishi aliyebobea nchini Marekani Warren Bennin alisema, “uongozi ni kubadilisha maono kuwa uhalisia”

2.     Hutenda kwa kufuata dhamiri “conscience”…hutenda kwa kufuata sauti ya moyo ya ndani inayomfanya mtu kutofautisha jema na baya. Kama Stephen Covey anavyosema; “Sauti hii ya ndani ni tulivu na ya amani. Pia inahusisha kujitoa mzima mzima kwa jambo jema tarajiwa…Ni hii dhamiri inayotafsiri maono kuwa huruma kwa wengine.”

3.     Huwa na shauku”passion” kubwa ya kutenda.Hii hutoka moyoni. Nikimnukuu mjasiriamali mwenye mafanikio na mwandishi wa vitabu Anthony Robbins anasema; "There is no greatness without a passion to be great, whether it's the aspiration of an athlete or an artist, a scientist, a parent, or a businessperson." Akimaanisha kuwa hakuna ukuu au umaarufu unaokuja bila ya shauku ya kuwa mkuu au maarufu, si ndoto ya kuwa mwanariadha au msanii, mwanasayansi, mzazi au mfanyabiashara.Haya yote yanaanza na kuwa na shauku.

4.     Nidhamu”discipline” kwao ni silaha.Kama alivyosema raisi wa  26 wa Taifa la Marekani  Theodore Roosevelt alisema; “kila kitu kinawezekana kwa kuwa na nidhamu binafsi”

5.  Ukifuatilia mafundisho au hotuba zao, huongea na hisia za watu kwa kugusa mioyo. Hupangilia maneno yao si kwa kujifurahisha wenyewe, bali kugusa hitaji la ndani la mioyo ya wengine. Kwa mantiki hiyo, wafuasi hupenda kuwasikiliza na kutendea kazi mawazo na mafundisho yao.

Bila shaka umepata kujua kuwa kila mtu anaweza kuwa kiongozi.Pia ni suala la kuchagua kujifunza na kufuata kanuni za uongozi bora na si bora kiongozi.

Jielimishe Kwanza!
Tutumie maoni yako
Barua pepe:jielimishekwanza@gmail.com

Jumamosi, 15 Juni 2013

FAMILIA: SIKU YA BABA....




Picha na www.bagboys.net
Ni siku kuu ya kutoa heshima kwa baba na kuheshimu umuhimu wa baba katika jamii.Siku hii husheherekewa pande nyingi za dunia hasa katika  siku Jumapili ya tatu ya mwezi Juni.Mwaka huu imeangukia tarehe 16/06/2013.

Siku hii ilianzishwa nchini Marekani katika karne ya 20 ili kuendana na Siku ya mama, pia kuonyesha na kukamilisha upendo kwa wazazi-baba na mama.

Siku ya baba  ilianzia mjini Spokane,Washington katika eneo la YMCA mwaka 1910 na Sonora Smart Dodd, aliyezaliwa Arkansas.

Ni vyema tukajumuika kuienzi siku hii muhimu ili kuthamini uwepo na juhudi za baba kwenye familia na jamii kwa ujumla.

Soma zaidi: http://en.wikipedia.org/wiki/Father%27s_Day

Ijumaa, 14 Juni 2013

NUKUU MAARUFU: UNAWEZA KUJIONA WEWE UNA KIBURI NA KING'ANG'ANIZI KULIKO WENGINE...FUATILIA NUKUU MAARUFU ZA ROBERT MUGABE-RAISI WA ZIMBABWE! JILINGANISHE...

Raisi Robert Mugabe wa Zimbabwe.Picha na www.telegraph.co.uk

UNAWEZA KUJIONA WEWE UNA KIBURI NA KING'ANG'ANIZI KULIKO WENGINE...FUATILIA NUKUU MAARUFU ZA ROBERT MUGABE-RAISI WA ZIMBABWE! JILINGANISHE...

PIA KWA TAARIFA ILIYOTOLEWA JANA-13 JUNI 2013, MUGABE AMETANGAZA RASMI KUGOMBEA URAISI KWA MARA NYINGINE-YAANI IWE MARA 33 MADARAKANI...


Zifuatazo ni nukuu maarufu za Raisi Robert Mugabe kama zilivyotolewa kwa lugha ya Kiingereza na www.brainyquote.com/quotes/authors/r/robert_mugabe.html#BdG8Mvci9r0QhfKu.99


Together, After, Vote
Our votes must go together with our guns. After all, any vote we shall have, shall have been the product of the gun. The gun which produces the vote should remain its security officer - its guarantor. The people's votes and the people's guns are always inseparable twins.
Robert Mugabe

Jesus, Once, Times
I have died many times. I have actually beaten Jesus Christ because he only died once.
Robert Mugabe



Mind, Europe, Banning
We don't mind having sanctions banning us from Europe. We are not Europeans.
Robert Mugabe


Africa, White, Indigenous
The white man is not indigenous to Africa. Africa is for Africans. Zimbabwe is for Zimbabweans.
Robert Mugabe


Keep, England, Zimbabwe  
So, Blair keep your England, and let me keep my Zimbabwe.
Robert Mugabe


Fear, Heart, Enemy
Our party must continue to strike fear in the heart of the white man, our real enemy!
Robert Mugabe


Change, Themselves, Call 
Countries such as the U.S. and Britain have taken it upon themselves to decide for us in the developing world, even to interfere in our domestic affairs and to bring about what they call regime change.
Robert Mugabe


Ask, Longer, Land 
We are no longer going to ask for the land, but we are going to take it without negotiating.
Robert Mugabe


Equality, Happen, Country
 

The land is ours. It's not European and we have taken it, we have given it to the rightful people... Those of white extraction who happen to be in the country and are farming are welcome to do so, but they must do so on the basis of equality.
Robert Mugabe



Pride, Rather, Actually
 

We pride ourselves as being top, really, on the African ladder... We feel that we have actually been advancing rather than going backwards.
Robert Mugabe

Become, Lose, Choice
If the choice were made, one for us to lose our sovereignty and become a member of the Commonwealth or remain with our sovereignty and lose the membership of the Commonwealth, I would say let the Commonwealth go.
Robert Mugabe

Age, Human, Africa

We of Africa protest that, in this day and age, we should continue to be treated as lesser human beings than other races.
Robert Mugabe

May, Necessary, Methods 
It may be necessary to use methods other than constitutional ones.
Robert Mugabe

Drink, Exercise, Eat 
Don't drink at all, don't smoke, you must exercise and eat vegetables and fruit.
Robert Mugabe

Times, Started, Policy 
 In most recent times, as the West started being hostile to us, we deliberately declared a Look East policy.
Robert Mugabe

Country, Nation, Stay
 

Stay with us, please remain in this country and constitute a nation based on national unity.
Robert Mugabe

Food, Enough, Why
We are not hungry... Why foist this food upon us? We don't want to be choked. We have enough.
Robert Mugabe

History, Enough, Suffering 
Was it not enough punishment and suffering in history that we were uprooted and made helpless slaves not only in new colonial outposts but also domestically.
Robert Mugabe

Oneself 
 There are things one must do for oneself.
Robert Mugabe

Making, Means, Ways 
Some people are contriving ways and means of making us collapse.
Robert Mugabe

Done, Said, Step 
 We have said the first step was to designate the land, inform the owners. And the second would be to get the responses from the owners. And this will be openly done.
Robert Mugabe


Free, Vote, Anyone 
People are free to campaign and they will be free to vote. There won't be any soldiers, you know, at the queues. Anyone who has the right to vote is free to go and cast his vote anywhere in his own area, in his own constituency.
Robert Mugabe

I wish to assure you that there can never be any return to the state of armed conflict which existed before our commitment to peace and the democratic process of election under the Lancaster House agreement.
Robert Mugabe

Read more at http://www.brainyquote.com/quotes/authors/r/robert_mugabe.html#BdG8Mvci9r0QhfKu.99


Imetolewa na,
Jielimishe Kwanza!