inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 22 Februari 2014

MTAZAMO: HOJA HUPINGWA KWA HOJA...


MwanaTYVA na
Mwanafunzi wa Azania Sekondari.

W
akati pakiwa na taarifa zinazosambaa kwa kasi kuhusu wajumbe wa Bunge maalum la Katiba kudai kuwa fedha wanayolipwa kwa siku ya kiasi cha shillingi laki tatu (300,000=/) haitoshi hivyo waongezewe posho.

Nilipata muda na kurejea kusoma kijitabu kidogo cha TUJISAHIHISHE kilichoandikwa na Raisi wa TANU Julius K.Nyerere ili nirejee makosa yaliyofanyika kipindi cha TANU hadi akaamua kuandika kitabu hicho.Ulikuwa ni wakati mzuri wa kugundua kuwa makosa mengi hayajasahihishwa na yanaendelea, na yametufikisha hapa tulipo.Soma hii pia ili kujisahihisha makosa yetu.
J.K.Nyerere anaandika anasema "Ukiondoa matatizo yanayowapata binadamu kwa sababu ya mambo kama mafuriko,nzige,kiangazi na kadhalika MATATIZO YAO MENGI HUTOKANA NA UNAFSI" jambo linalowafanya kuuliza hali yao ya baadae itakuwaje na hufanya hivyo si kwa maslahi ya jamii ya watu,bali kwa maslahi yao binafsi.
Hayo yameanza kujitokaza ikiwa ni siku chache tu tangu wajumbe wa bunge maalum la Katiba kuwasili huko bungeni kutimiza yale jamii iliyowateuwa na  kuwaamini kuwa wanaweza fanya kazi waliyotumwa na wananchi.
Hayati J.K.Nyerere hakuishia upande mmoja tu,bali aliangalia upande wa pili wa shillingi na kuandika akisema "Kosa jingine linalotokana na unafsi tunalifanya wakati wa kuchagua viongozi,mahala pengine viongozi ( na hata wawakilishi) wetu hawana budi watokane na WATU bila hila au ujanja wa aina yoyote".Nimenukuu kifungu hiki nikihusisha na uhalisia kuwa tayari kuna taarifa za ndani toka bunge hilo maalum la Katiba na pengine katika vyombo mbalimbali ya habari kuwa kuna wawakilishi hawajaenda kuiwakilisha jamii yao,bali ni kwa manufaa yao binafsi.
J.K. Nyerere anaendelea na kusema "lakini mara nyingi wawakilishwaji huchagua wawakilishi bila kufikiri kwa makini kuwa viongozi hao wanaweza, au hawawezi kazi wanayochaguliwa kufanya.Wawakilishwaji watafanya makosa makubwa saana kama watachagua viongozi wao ovyo tu. Kimsingi yote ni makosa na kosa la kwanza ni tofauti na kosa la pili japo yote hutokana na Unafsi.”Swali la kujiuliza ni kwamba"
Wakati pakiwa na muendelezo wa matukio kadhaa kama haya, tunajifunza nini? na twapaswa kujisahihisha wapi? Kama Mtanzania mwenye kulichukulia kwa uzito wa hali ya juu Bunge maalum la Katiba nikijua fika ndipo mahali pekee patakapojenga hatma ya Tanzania njema,bora na yenye matumaini kwa Watanzania wote leo kesho,kesho kutwa au hata baada ya miaka hamsini ijayo tena,Wawakilishi wangeweka tofauti zao za kimaslahi pembeni kwanza na kutafakari kukubaliana kutimiza kwa moyo wa dhati majukumu watakayofanya wakiwa Bungeni-Dodoma kwa hizo siku na pengine zaidi kadri ya ufanishikishaji wa Katiba hiyo mpya, tarajiwa ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
Hata hivyo napenda kumalizia kwa kusema kadhaliwa matakwa na mapendekezo ya wachache pia hujulikana katika mijadala,majadiliano na mazungumzo.Bila wachache kusema waziwazi matakwa yao,mijadala na majadiliano hayana maana.Kwa kadri ya mapendekezo na matakwa yao hao wachache waje na hoja na kupewa nafasi ya kusikilizwa kisha wenye kupinga nao wapinge kwa hoja.
Hivyo ni matumaini yangu kuwa wachache waliokuja na hoja ya kutokutosha kwa posho wanayolipwa, hivyo kutaka kuongezewa… watakuwa na hoja kwanini waona hivyo? na wachache wanaosema inatosha na kwa maana hiyo hapana uhitaji wa kuongeza posho hizo watakuwa na hoja kwanini wao wanaona hivyo.Hoja hujibiwa kwa hoja.
Mungu ibariki Tanzania. 
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!


Alhamisi, 20 Februari 2014

BIASHARA: NJIA PEKEE ZA KUPAMBANA NA KUMSHINDA MSHINDANI WAKO KATIKA BIASHARA…


Ikiwa unafanya biashara tambua kuwa huwezi kukosa mshindani.Mshindani wako ni yule anayetoa huduma au bidhaa kama yako kwa wateja uliowalenga.Anaweza kuwa na mbinu mbali mbali zinazomfanya aweze kukaa kwenye soko.Hivyo unapaswa kumfahamu na kumchunguza.
Picha imetolewa blog.bounzd.com 
Ndugu msomaji na mfanyabiashara unayependa kujielimisha kujiimarisha, naomba itambulike kuwa katika eneo hili sijabagua aina ya biashara, ila nazungumzia biashara halali zenye kipato halali…ikiwa sasa kuna njia nyingi tu za kufanya biashara halali, mfano kupitia teknolojia ya habari na mawasiliano-mitandao ya jamii n.k. unaweza kuamua mwenyewe njia mahsusi itakayo kupatia mafanikio kwa urasahisi.

Katika  mtazamo wa biashara, inapaswa ujue kuwa, njia hizo zote huwezi kukosa mshindani.

Unajisikiaje au unajipangaje unapoona mfanyabiashara mwenzio anatoa huduma au kuuza bidhaa ile ile kwa mafanikio kiasi kwamba anakaribia kukushinda? Hili ni swali gumu kwa mfanyabiashara yeyote anayefanya biashara halali isiyo na mawaa.

Nikushirikishe mbinu (5) pekee za kibiashara zinazotumiwa na wafanyabiashara wakubwa ambazo hata wewe kama ni mfanyabiashara mdogo au mkubwa unaweza kuzitumia ikiwa tu umewahi kusoma alama za nyakati.
Kabla ya kuanza kutafuta na kutumia mbinu hizi, unapaswa kumjua mpinzani wako.Je wajua jinsi ya kumjua mpinzani wako? Soma hii.
Mbinu hizo ni; (leo nitaainisha 2)


1.Inunue kampuni inayoelekea kukutisha ili ubaki kileleni.
Hapa unaweza kuniuliza; inawezekanaje hapa ndugu mwandishi?  Inawezekana kabisa.Naomba nikupe mifano halisi: Mwaka 2012 Facebook iliweza kuinunua Instagram (ikiwa ni kampuni changa iliyotishia uwepo wa Facebook) kwa dola bilioni 1($1 bilioni) kama ilivyoripotiwa na   @CNNMoneyTech February 19, 2014: 6:54 PM ET.
Mwaka 2014, Facebook tena, imetangaza kuinunua kampuni pinzani-WhatsApp kwa dola bilioni 19. Hiyo ndiyo biashara kubwa zaidi ya ununuzi kuwahi kutekelezwa na Facebook hadi kufikia sasa. Najua umejionea mwenyewe jinsi WhatsApp inavyokuja kwa kasi ikiwa na watumiaji zaidi ya mil.450, na inajiongezea watumiaji wapya milioni 1 kila siku. 
 Pia, kwa kufanikisha hilo mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amesema kuwa mtandao huo upo njiani kuwaunganisha watu bilioni moja jambo litafanya Facebook kuwa na thamani kubwa, BBC Swahili imeripoti leo, 20 Februari, 2014 - Saa 04:27 GMT.

2.Ingia Ubia Na Mpinzani Wako
Hapo zamani nchini Tanzania, tukiwa na teknolojia hafifu tulitegemea sana kuhifadhi  na kutoa fedha zetu benki. Mapinduzi makubwa yametokea katika eneo hili la biashara mara tu matumizi ya simu za mkononi ikiwa sanjari na teknolojia ya kutuma na kupokea pesa pale ulipo…ikimaanisha si lazima uende benki kupanga foleni.
Mfano halisi wa jambo hili ni pale baadhi ya benki nchini Tanzania(sitaki kuzitaja, unazijua) zimepata mtikisiko mkubwa kutoka kwa mpinzani mpya aitwae teknolojia ya kutuma na kupokea fedha kupitia simu za viganjani. Huduma hii mpya imewavuta wateja wengi kiasi cha kutishia maisha ya Mkongwe wa biashara.
Nikuulize ndugu msomaji, benki wanaishije na mpinzani katika mazingira ya biashara? Bila shaka…utakuwa umejionea mwenyewe jinsi Makampuni yanavyojenga ubia na mfumo mpya wa kutuma, kuweka na kupokea fedha.
…Itaendelea.
Imetayarishwa na kutolewa na
Jielimishe Kwanza! Social Interprises.