inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 21 Oktoba 2013

AJIRA NA KAZI: JIEPUSHE! ZUIA! UTUMWA WA KISASA…

Kabla ya kukoma kwa biashara ya utumwa mnamo karne ya 18, binadamu alikuwa akiuzwa kutoka nchi moja hadi nyingine(mfano Afrika kwenda Ulaya na Uarabuni) kwa lengo la kuwatumikia wengine kwa ujira mdogo sana au bila ujira kabisa.
Mara tu baada ya kukoma kwa biashara hiyo ya watumwa, wafanyabiashara na watu wa kada nyingine za ajira walikaa chini na kutafakari…mwisho wakaweka kitu kinachoitwa ujira/mshahara kulingana na utendaji au ubora auletao mwajiriwa katika eneo la kazi.Hapa kukatokea ngazi/madaraja mbali mbali ya mishahara!  

Nikimnukuu Jim Rohn aliyekuwa mwandishi maarufu na msemaji wa hadhara nchini Marekani- anasema; “People get paid by bringing value to the market place”.(Watu hulipwa kutokana na ubora wanaouweka katika soko)-Alizungumzia soko kama watu au eneo la kazi kwa kuwatumikia watu.

Kama ulikuwa hujui hilo, funguka macho ndugu msomaji.Hiyo ndiyo hali halisi.Hivyo basi ukiona unalipwa kidogo ujue una mchango mdogo sana kwenye soko.Hili limepelekea watu wengi sasa kuishi katika utumwa ulioboreshwa/Utumwa wa kisasa au kwa lugha ya Kiingereza “Modern-day Slavery”.
Picha na www.cvent.com
______________________________________________________________________________________________________________

Utumwa huu wa kisasa unahusisha; usafirishwaji wa binadamu ndani au nje ya nchi (aina hii ni kama inaturudisha tulikotoka-Kihistoria),watumishi wa ndani, kuzidiwa na madeni,kulazimishwa kuomba omba, kushurutishwa kimapenzi, kulazimishwa kuolewa katika umri mdogo, kunyanyaswa kijinsia na manyanyaso katika sehemu za kazi(kufanyishwa kazi ngumu kwa ujira mdogo au bila ujira kabisa).
______________________________________________________________________________________________________________

Nimeamua kukujuza hili kwa kulinganisha na taarifa ya gazeti la “The Citizen” –Jumamosi, 19 Octoba 2013 la nchini Tanzania kuripoti kuwa zaidi ya watu 300,000 nchini Tanzania ni watumwa katika mfumo huo wa utumwa wa kisasa!Tanzania ikiwa inaongoza kuwa na idadi kubwa ya watu walio katika utumwa wa kisasa katika nchi za Afrika Mashariki.

Kulingana na takwimu za mwaka 2013 za “Global Slavery Index” zinaeleza kuwa kati ya watu 310,000 hadi 350,000 wanaishi kama watumwa.Namba kubwa ya watu ikiwa mjini.Tanzania ikiwa ya 29 katika nchi 162 zilizofanyiwa utafiti huo duniani. Gazeti la “The Citizen” limeripoti.  Soma hii                                                        


Utumwa huu wa kisasa una viashiria vingi ambavyo nitavieleza siku nyingine.Pia tutafahamishana mbinu za kuepukana na utumwa huu wa kisasa hasa katika maeneo ya rasmi ya kazi.

Hivyo endelea kuifuatilia blog yako Jielimishe Kwanza! Ujielimishe! zaidi kwa Kuhamasika! Pia Kuhamasisha! wengine kubadili mtazamo ili kuepuka manung’uniko na kuwa na mtazamo chanya.
Soma na hii kujua zaidi kuhusu utumwa wa kisasa http://www.antislavery.org/english/slavery_today/what_is_modern_slavery.aspx

Imetayarishwa na kutolewa na,

Jielimishe Kwanza!








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni