inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 12 Septemba 2015

MTAZAMO: KILIMO CHA KIJASIRIAMALI; ANZIA ULIPO...



“ …Kufanya biashara yenye mafanikio si kutegemea kuona mafuriko ya pesa kwa mkupuo; ila ni kukusanya faida/pesa kidogo kidogo kutoka vyanzo vidogo vidogo vya mapato” 
-Bw.Baraka Mponda-
______________________
Tunapozungumzia kilimo cha kijasiriamali ni kilimo kinachofanyika na kufanikiwa katika mazingira yenye changamoto ambazo hubadilishwa kuwa fursa. Mkulima mvumilivu na makini huona na kuitumia fursa ambayo wengine hawajaiona au wameiona na kupuuzia.
Jicho la blog hii kimtazamo liliweza kumuona mkulima  makini na mjasiriamali mwenye mafanikio Bw. Baraka Mponda (44) wa kitongoji cha Patandi, Tengeru-Mita chache kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Nelson Mandela -Arusha anayejihusisha na kilimo cha kijasiriamali cha mboga mboga na viungo. Alianza  kujihusisha na kilimo mnamo mwaka 1992 katika eneo la nyumba yake ambalo tumemkuta.
Bw. Baraka Mponda (44) akielezea jambo kwa mwandishi-Henry Kazula kushoto kwake.                      



































____________                                                                                                                        _________
Yafuatayo ni mahojiano yetu na Bwana Mponda ikiwa ni hamasa kwa vijana na wakulima wengine wenye kianzio lakini wanashindwa kuchukua hatua nyingine ya kiujasiri kuondoa changamoto na kuzibadilisha kuwa fursa.
Mahojiano yalianza hivi:
·        Je, ni shughuli hii hii ya kilimo cha kijasiriamali cha mboga mboga na viungo, ufugaji wa ng’ombe, mbuzi na kuku wa kienyeji imekufikisha katika mafanikio tunayoyaona leo? Ukizingatia kuwa unauza mboga kwa shilingi 100 kwa fungu moja!
“ …Kufanya biashara yenye mafanikio si kutegemea kuona mafuriko ya pesa kwa mkupuo; ila ni kukusanya faida/pesa kidogo kidogo kutoka vyanzo vidogo vidogo vya mapato” 
alisema Bw.Baraka Mponda kwa kujiamini.
Bw. Baraka Mponda (44) akionyesha kiwango cha fungu la viuongo-mboga kwa sh.100(TZS).
·        Ni lini umeanza kujishughulisha na kilimo cha kijasiriamali na kiutaalamu kwa mfumo wa umwagiliaji matone-“drip irrigation” kupitia njia ya “pump” na kisima ulichochimba.Vipi ulitumia gharama kiasi gani kwa huu mfumo wa “drip irrigation”?
…Mfumo huu wa kilimo cha kijasiriamali cha-“Drip irrigation” nimeanza mwanzoni mwa mwaka 2015 kwa gharama ya shilingi milioni 5, ingawaje nilianza kujishughulisha na kilimo cha mboga mboga na viungo mnamo mwaka 1992. Mipira ya kutandaza kwenye matuta iliyounganishwa katika mfumo wa maji ya kisima cha kuchimba mwenyewe na “pump” nimenunua kutoka kampuni ya “Bulton Tanzania Limited” kwa teknolojia kutoka Israel...Alisema Bw.Mponda.
Mfumo wa umwagiliaji katika shamba la Bw. Baraka Mponda (44) nyumbani kwake.
·        Unaweza kuelezea jinsi ulivyoweza kuchimba na kuhifadhi maji kwenye "reservoir"; umetumia gharama kiasi gani?
…Chanzo cha maji kwa matumizi ya nyumbani na kilimo ni kupitia kisima cha kuchimba na kuhifadhi maji kutumia “pump” katika “tank” na “reservoir” yenye ujazo wa 36,000ml. Zoezi zima la kupata maji limenigharimu shilingi milioni 7…alisema kwa ujasiri Bw.Mponda.
Hapa ndipo chanzo cha maji (kisima) kwa matumizi ya nyumbani na kilimo.Maji hupandishwa kwa "pump" ya umeme kwenye "tank"na "reservoir" iliyojengwa katika mwinuko mita chache kutoka nyumbani kwake kama inavyoonekana katika picha hapa chini.
Nyumba ya Bw. Baraka Mponda (44) inavyoonekana katika mwinuko ilipo "reservoir" kwa ajili ya kilimo.
·        Nini mafanikio yako tangu uanze kujihusisha na kilimo cha kitaalam na kijasiriamali?
…Mimi ni baba wa watoto 3, nina uwezo wa kuwahudumia watoto wangu kwa kila kitu ikiwa pamoja na kielimu hadi ngazi ya chuo kikuu. Mtoto wangu wa kwanza anaenda chuo kikuu mwaka huu, wa pili yupo shule ya sekondari nzuri na inafanya vizuri kitaaluma. Nina nyumba yangu  na Magari mawili; moja la kutembelea mke wangu na lingine la shughuli za shamba.Pia nimeajiri vijana 3 wanaonisaidia shughuli za shamba na ufugaji…alijibu kwa tabasamu Bw.Mponda.
Bw. Baraka Mponda (44) na mke wake(katikati), nyuma ni magari wanayomiliki.Wengine ni mwandishi Henry Kazula(kushoto) na John Karugah (kulia); wote ni wanafunzi shahada ya uzamili- Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia-Nelson Mandela.

·      Je unajishughulisha na nini kingine zaidi ya kilimo?
Mimi ni msambazaji wa mboga mboga kwa “tender” katika mahoteli jijini Arusha  (shughuli hii inayohitaji kuwa na mtaji wa shilingi milioni 10).
·    Nini malengo yako ya siku za usoni?
…Malengo yangu ya baadaye ni kulima kisasa zaidi kwa kutumia “greenhouse” hasa kwa zao la Hoho nyekundu na Njano…Alisema Bw.Mponda.
·    Kipato chako cha mwezi ni wastani wa sh.ngapi?
…haina shida! Kipato changu kwa mwezi hakipungui milioni 2 ikiwa nilianza na mtaji wa shilingi 10,000 kununua mbegu.
·      Umepitia changamoto zipi hadi leo tunaona mafanikio yako?Ulifanyaje kupambana nazo?
…Bila kuficha, hakuna kazi isiyo na changamoto; Kutokuwezeshwa kimtaji; mafanikio niliyonayo yangeweza kuwa makubwa zaidi na kutoa fursa ya ajira kwa wengine.Kutokata tamaa/uvumilivu na kuthamini kidogo unachopata ni msingi mkubwa katika kukua kibiashara.Maisha ni kupambana hata katika mazingira magumu.
·   Tumalizie kwa kutoa ushauri  wako kwa vijana na wakulima wengine:
…Nawashauri vijana na wakulima wenzangu kuwa na Uvumilivu na kupambana…alijibu kwa kifupi.
·    Nini rai yako kwa wadau wa kilimo na serikali?
…Nasisitiza utolewaji wa semina na warsha kwa vijana zenye kuwawezesha na kutoa fursa za kujiajiri katika kilimo. Pia, Serikali inatakiwa iwafungulie vijana milango ya kujiajiri kwa kumaanisha na isiwe kuongea tu bila utekelezaji…alimalizia Bw.Mponda.
Picha zote na Paul Lucas- mwanafuzi shahada ya uzamili, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia-Nelson Mandela.
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-“Mtazamo Wako Ni Upi?”
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!