inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 30 Julai 2013

URAFIKI: SIKU YA KIMATAIFA YA URAFIKI DUNIANI-LEO HADI TAREHE 5 AGOSTI 2013



Picha na www.vidyouth.com
International Friendship Day [1] is a day for celebrating friendship. The day has been celebrated in several southern South American countries for many years, particularly in Paraguay, where the first World Friendship Day was proposed in 1958.[2]

Official name International Friendship Day
Also called Friendship Day
Observed by Many countries
Type Historical
Date First Sunday in August (many countries), 20 July in Argentina, Brasil and Uruguay, 30 July in Paraguay
2012 date 5 August
2013 date 4 August
Related to Friendship Love

Imetolewa: http://en.wikipedia.org/wiki/International_Friendship_Day

______________________________________________________________________________________________________ 



-->
Hii ni siku kubwa duniani inayojumuisha marafiki-wanaotaka kuboresha urafiki, pia wale wanaotaka kuanzisha urafiki mpya.



Sanjali na siku hii yenye kuboresha mahusiano mema kwa jamii mbali mbali za watu duniani…amani na upendo utawale…sidhani kama utawaza kumuua au kumwibia rafiki yako  kama una urafiki ulio imara yako!



Tukiwa na malengo makubwa yenye kujenga au kuimaisha urafiki, kuna mambo 20 muhimu ya kufanya kufikia lengo(leo nitaainisha 10 tu):



1.JARIBU KUWA WEWE…USIMUIGIZE MTU

Uhalisia wa mtu ni chachu kubwa sana ya kujenga urafiki imara.Tuache kuwaiga wengine.


2. UWE RAFIKI…ONYESHA KUWA RAFIKI KWA WENGINE


3.KUWA MTOAJI…JITOE KWA AJILI YA WENGINE KWA SHIDA NA RAHA


4.UWE MTU WA KUTIA MOYO


5.KUWA MTU WA KUVUTIWA…JARIBU KUVUTIWA NA VITU TOFAUTI TOFAUTI…SOMA MAMBO TOFAUTI TOFAUITI (Pitia:http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/ifahamu-siri-iliyopo-ndani-ya-vitabu.html


6. KUWA MWAMINIFU


7.KUWA MVUMILIVU


8.THAMINI MUDA WA WENGINE


9.JITHAMINI PIA


10.KUWA MUELEWA…ANZA KWANZA KUELEWA WENGINE

10 nyingine zitatolewa hapo tarehe 5 Agosti 2013...toa maoni yako!

Pia kuisindikiza siku hii, tazama wimbo huu kutoka kwa Michael Jackson:



Video: www.youtube.com


Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Jumapili, 28 Julai 2013

FAMILIA NA MTAZAMO: NANI ANA JUKUMU LA KULIPA BILI MBALI MBALI?...TAZAMA PICHA!


Picha na
Picha:THINKSTOCK
Picha na merryfarmer.net
Picha na tvone.tv 
Ni ukweli usiojificha kuwa wanaume wamekuwa mstari wa mbele kuchukua majukumu mbali mbali ya familia yahusuyo kutoa pesa.Ingawaje katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kiuchumi na teknolojia tunaona pia wanawake wakichukua nafasi kubwa ya kubeba majumu ya familia yahusuyo kutoa pesa.

Najua kila mtu atakuwa na mtazamo tofauti kuhusiana na swali letu la leo.

Nikitumia uzoefu wangu wa kutazama kwa ukaribu masuala ya familia…chukua mfano umeenda sehemu ya starehe(hotelini), chunguza kwa makini, nani analipa bili ya mapochopocho yaliyoliwa na vinywaji? Ni mwanamke au mwanaume? Jibu unalo! 

Kautaratibu haka huendelea kujijenga kuanzia kipindi cha uchumba hadi wakati wa ndoa.

Tatizo linakuja pale wanandoa wanapokuwa wote wana kipato…utaona utata, mume huanza kumbadilisha mwanamke ghafla kwa kumwambia aanze kutoa pesa kwa matumizi mbali mbali ya nyumbani.Jibu la mke huwa ”wewe ndiyo baba na kichwa cha familia…hivyo una wajibu wa kubeba majukumu yote.” Ndiyo hivyo, hakuzoea kulipia bili tangu kipindi cha uchumba…anajua kuwa mwanaume ana jukumu la kulipia gharama zote za familia. 
Hapa ndipo ugomvi unapoanzia kuhusiana na mapato na matumizi ya pesa kwa kila mmoja.
 Utaratibu huo unaweza kubadilika, hasa ikizingatiwa kuwa mahusiano na ndoa ni makubaliano wa mwanaume na mwanamke yakilenga kusaidiana na kujenga familia iliyo imara. 






  


 

Tunaanzia wapi sasa kubadilisha mfumo? 
 1. Mwanaume una jukumu la kumzoesha mwanamke wako kuanza kulipa au kuchangia bili   au  gharama nyingine za matumizi (haijalishi kama wewe mwanume unampa pesa) …inapaswa aonekane analipa au kuchangia...

 2.  Mwanamke, huna sababu ya kukubali kulipiwa mara kwa mara…onyesha kuwa nawe
     una uwezo wa kulipa au kuchangia, hivyo huwezi kutetereshwa na hutanyanyasika wala kufanywa mtumwa wa mwanaume. 

3. Lifanye zoezi lenu kuwa endelevu na mtaona mtunda yake.Hapa ndipo lile lengo tarajiwa la kusaidiana kwenye ndoa linapojidhihirisha.Pia kuepusha ugomvi unaohusiana na matumizi ya pesa kwa kila mmoja.

Picha na myhappyfinds.com
Anzia hapo kubadilisha mtazamo ili kuepusha migogoro ndani ya familia!
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!

Jumamosi, 27 Julai 2013

MAISHA: KATIKA MAISHA KUNA KUSHINDA NA KUSHINDWA...SI KWELI WANAOSHINDWA HAWAWEZI, NI MBINU TU SIMESHINDWA, WAKIBORESHA MBINU ZAO NA MFUMO WA KUFIKIRI,WANAWEZA KUFANYA VIZURI ZAIDI YA MWANZO!

Picha na GETTY IMAGES.Ujumbe huu umetolewa kwa niaba ya Jielimishe Kwanza!

ELIMU NA MAFUNZO:KWA KUTHAMINI UWEZO NA KIPAJI CHA KILA MWANADAMU ALICHOPEWA NA MUNGU, PIA KUTAMBUA FURSA NYINGI ZILIZOPO NA ZINAZOHITAJIKA KUTATUA MATATIZO LUKUKI KATIKA JAMII YETU...



 






Jielimishe Kwanza! IKISHIRIKIANA NA KAMPUNI YA 
Science &Fine arts Resource Centre (SFRC) http://www.sfrctanzania.blogspot.com/ JIJINI DAR ES SALAAM WANAKULETEA MAFUNZO YA KIPEKEE YANAYOWAHUSISHA VIJANA-WANAFUNZI WOTE WALIOMALIZA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI NA KUTENGWA NA MFUMO WA ELIMU
(...WAMEFELI KUENDANA NA MFUMO WA ELIMU NA SI WA MAISHA).

TUNAAMINI KUWA KUSHINDWA KUENDANA NA MFUMO RASMI WA ELIMU SIYO MWISHO WA KUTIMIZA NDOTO YAKO KATIKA MAISHA, PIA SI KUSHINDWA MAISHA!

UKIWA UPO KWENYE KUNDI HILO, AU UNA MTOTO,NDUGU,RAFIKI ALIYE KATIKA KUNDI HILO NA MMEKATA TAMAA...

             KWA MAELEZO ZAIDI, TUWASILIANE KUPITIA
SIMU YA KIGANJANI: 0754 572 143         
                                          0716 075 826          
                                0785 175 157

 KUPITIA MAFUNZO YETU, KIJANA ATAELEKEZWA KUJITAMBUA KUENDANA NA KILE ANACHOKIFAHAMU NA MATAKWA YA NDOTO ZAKE!

MAFUNZO YATAANZA TAREHE 15 AGOSTI 2013 

WAHI NAFASI YAKO MAPEMA,KUNDI HILI NI KUBWA SANA KATIKA NCHI YETU

            KARIBU SANA!

Jumatano, 24 Julai 2013

VIJANA NA MAISHA: KWA HIZI SIFA 10, KIJANA MWENYE UMRI WA 18-35 UNAKARIBIA KUWA TAJIRI!

-->
Huyu ni miongoni wa vijana matajiri duniani...
______________________________________________________________________________________________________________
Mark Elliot Zuckerberg (born May 14, 1984) is an American computer programmer and internet entrepreneur. He is best known as one of five co-founders of the social networking website Facebook. As of April 2013, Zuckerberg is the chairman and chief executive of Facebook, Inc.[6][7] and in 2013 his personal wealth was estimated to be US$13.3 billion.[5]
Source: http://en.wikipedia.org/wiki/Mark_Zuckerberg
________________________________________________________________________________________________________________________________________
Mark Elliot Zuckerberg-Mwenyekiti na Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Facebook
Hizi ni baadhi ya sifa za matajiri maarufu duniani walio katika umri wa miaka 18-35.
 
SIFA 10 NI KAMA IFUATAVYO:

1.UNAFANYA MAKOSA LAKINI UNAJIFUNZA KUPITIA MAKOSA


2. UNAJIBIDISHA KWA KAZI ZENYE KIPATO HALALI…HASA KUJIAJIRI 


3. UKIPATA PESA HUTUMII YOTE, UNAHIFADHI KWA UTARATIBU MAALUM 

4.UNAJARIBU KUSIMAMA KWA MIGUU YAKO…HUTAKI KUWA TEGEMEZI!


5. UNATUMIA KILEO KIASI NA UNA NIA YA KUACHA KABISA!


6.UNAJARIBU KUTUMIA FURSA ZILIZOPO KUTENGENEZA PESA


7.HUTOI VISINGIZIO KUHUSU KUSHINDWA KUTIMIZA JAMBO…UNAVAA UHUSIKA WA MOJA KWA MOJA


8.UNATAZAMA CHANGAMOTO KAMA FURSA YA KUTOKA KIMAISHA


9.HULAUMU MAPITO YA ZAMANI…UNASONGA MBELE KUBORESHA MAISHA YAKO


10.UNAJIHUSISHA NA MARAFIKI WAPENDA MAENDELEO NA SI WADIDIMIZA MAENDELEO.

Zinaendelea kupitia http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/08/vijana-na-maishakwa-sifa-hizi-kijana.html 

Tuandikie kutoa maoni yako:barua pepe jielimishekwanza@gmail.com

Ikiwa unaona unazo sifa hizi zote kwa dhati...tuandikie kutoa maoni yako.


USIKATE TAMAA…

CHUKUA HATUA YA UJASIRI KUBADILIKA!
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!



Jumanne, 23 Julai 2013

AFYA: NI MUHIMU KUPATA KIFUNGUA KINYWA KWA AFYA YA MOYO WAKO!


Picha na www.wisegeek.org
Utafiti uliofanywa na wanasayansi wa masuala ya afya na lishe nchini Marekani umebaini kuwa “kifungua kinywa huupa moyo afya na kuuepusha na magonjwa ya mshtuko wa moyo.” 
Utafiti wao uliowahusisha wanaume 27,000 wenye umri kati ya miaka 45-82 ulionyesha kuwa wale wasiokula kiamsha kinywa wako katika hatari ya matatizo ya moyo. Wakati wa utafiti huo, zaidi ya watu 1,500 waliathirika kutokana na mshtuko wa moyo.
Utafiti huo ulithibitisha kuwa watu waliokosa kifungua kinywa wako katika hatari kubwa ya kupata matatizo ya moyo kwa asilimia 27 kuliko wale wanaokula asubuhi.
Ukizingatia utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Harvad kitivo cha afya ya jamii kilisema kuwa: “kukosa kiamsha kinywa kunasababisha mwili kutumia nguvu nyingi zaidi kuliko kawaida.” Sambamba na utafiti huo, taasisi ya matibabu ya moyo nchini Uingereza imebaini kuwa “kiamsha kinywa huwazuia watu kula vitu vyenye sukari kabla ya chakula cha mchana.”(http://www.bbc.co.uk/swahili/kwa_kina/2013/07/130723_kiamsha_kinywa.shtml).
Kupata kifungua kinywa kwa mtu wa kipato cha chini inawezekana...si lazima iwe kama picha inavyoonyesha, ni muhimu kuzingatia makundi ya vyakula unayotakiwa kula kulingana na kipato chako.Yote tisa, kifungua kinywa ni muhimu sana kwa afya yako.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!
 

ELIMU: PATA UJASIRI WA KUONGEA MBELE YA HADHIRA!

Picha na images.businessweek.co
Tunapolitazama suala zima la kujieleza mbele ya hadhira si suala rahisi kama hofu itakutawala.Itawale hofu!

Watu wengi ni waoga sana kusimama mbele ya hadhira.Mfano: utamwona mtu anatetemeka mara tu anaposimama mbele ya hadhira au kuongea maneno nusu nusu na hatimaye kushindwa kuwasilisha ujumbe uliokusudiwa kwa hadhira.Je, tatizo ni nini? Tatizo limeanzia wapi?


Awali ya yote kabla ya kueleza MBINU 5 za kukufanya ufanikiwe kujieleza mbele ya hadhira bila hofu, ni vyema tukajua chanzo cha tatizo kupitia maswali  hayo mawili yaliyotajwa.

Tatizo la kuogopa kuongea mbele za watu au hadhira linanzia tangu shuleni, pale mwanafunzi anapochekwa hasa akiwa anaongea mbele ya darasa hivyo kujikuta akikosa ujasiri wa kuendelea kuongea.Hili linawafanya wanafunzi wengine kuogopa kusimama mbele ya hadhira na mwisho hubaki kutupiana mpira wa kujieleza inapofika hatua ya majadiliano na uwasilishaji darasani.

Pia, mfumo wa elimu- mfano nchini Tanzania haujaweka msisitizo wa kutosha kwa wanafunzi kuhusiana na suala zima la kujieleza mbele ya hadhira.Wanafunzi wamekosa ujasiri wa kuelezea vitu walivyoviandika kwa ufasaha katika hali ya kawaida.Hili linatokana na kuwa na mtazamo wa moja kwa moja wa kuandika kwa lengo la kufaulu mitihani na si kuwa ujasiri wa kukielezea walichokiandika kimatendo mbele ya wengine na kupambana na changamoto za maisha ya kila siku.

Athari hii kwa mwanafunzi haishii hapo bali huathiri maisha ya ukubwani.Ndiyo maana utaona watu wengi hushindwa kujieleza kwa ufasaha kwa sababu ya hofu.
Tuje moja kwa moja kwenye MBINU 5 za kuwa na ujasiri wa kuongea mbele ya hadhira:
1. JIANDAE VYA KUTOSHA! FANYA ZOEZI UKIWA MWENYEWE...
Ni vyema kujiandaa kuhusiana na kile unachataiwa kukieleza mbele ya hadhira.Ifahamu hadhira utakayokwenda kuielezea jambo fulani. Usiende kuongea mbele ya hadhira ukifikiria kuwa maneno yatapatikana ukiwa mbele yao.
Unashauriwa kufanya zoezi la kujieleza ukibashiri kama unaongea na hadhira.Kipekee zaidi ukimtazama mtu mmoja akiwakilisha hadhira yote.Hili ni la muhimu sana katika maandalizi, unapaswa kujua kuwa huwezi kukidhi matakwa ya kila mtu.
Inashauriwa uongee ukiwa unajitazama kwenye kioo au ukamwomba rafiki yako akurekodi.Hii itakusaidia kuondoa mapungufu uliyonayo na itakujengea ujasiri zaidi hata utakapokuwa ukiongea na hadhira halisia. 
MUHIMU: Hakikisha unaifahamu hadhira utakayokwenda kuongea nayo, itakusaidia kupanga mbinu za kuwasilisha hoja zako.

2. EPUKA KUKARIRI HOTUBA YAKO KWA KILA NENO…ELEWA!
Si jambo baya kuandika hotuba yako kwenye karatasi au kijitabu, lakini kuwa makini sana wakati wa kutumia ukiwa mbele ya hadhira. Ni vyema kuelewa kile unachotaka kukiwasilisha mbele ya hadhira.
3. EPUKA KUSOMA HOTUBA YAKO NENO KWA NENO
Ukizingatia mbinu namba 2, itumie hotuba yako uliyoandika kwa kujikumbusha sehemu zenye utata.Usiisome hotuba yako…utawachosha wasikilizaji watasema; “ ni vyema angetupatia hotuba yake tukajisomee nyumbani…”
4.  USIOGOPE KUHUSU WOGA WAKO
Itambulike kuwa kila binadamu ana chembe ya woga. Ni vyema kuitambua hofu yako na kujaribu kupambana nayo bila kujulikana na hadhira pia bila kuharibu uwasilishaji wako.
5. USIJIWEKE KUWA MKAMILIFU WAKATI WOTE
Unapaswa kujua kuwa hata waongeaji maarufu wa hadhara hufanya makosa.Hivyo usifikiri kuwa hutakuwa na makosa katika uwasilishaji wako.Ni vizuri ukuamua kurekodiwa kwenye video ili ujitazame baada ya hotuba yako.Itakusaidia kujua makosa uliyoyafanya wakati wa uwasilishaji hivyo kuboresha utendaji wako siku hadi siku.
Sambamba na mbinu hizi, ni vyema pia kuboresha muonekano wako-mfano mavazi nadhifu, uongeaji wako na uhusiano mzuri na hadhira (kuwatazama moja kwa moja).Pia matendo yako yaendane na kile unachotaka watu waelewe.

Nakutakia kila la heri katika kutumia mbinu hizi na kuboresha ujasiri wako wa kuongea mbele ya hadhira. Ukifanikiwa, ni sehemu mojawapo ya kupata ajira na kuwa mahiri katika fani yako...Itambulike kuwa suala la kuongea mbele ya hadhira HUWEZI KULIKWEPA, ipo siku tu utatakiwa kusimama mbele ya hadhira na kutoa neno.

BOFYA HAPA KUTAZAMA VIDEO UONE JINSI UNAVYOTAKIWA KUONGEA MBELE YA HADHIRA...

Ijumaa, 19 Julai 2013

ELIMU NA MALEZI: MJENGEE MTOTO WAKO TABIA YA KUSOMA VITABU...

-->
Picha na www.pbs.org
Mzazi/Mlezi unaonekana kama kioo kwa mtoto.Mtoto anajifunza mengi kupitia wewe, pia anaamini mafundisho yako. 
Tukizungumzia utamaduni wa kusoma vitabu vyenye tija ya kuelimisha, ni muhimu sana kumjenga mtoto wako akiwa katika umri unaoendana na hatua ya kutaka kujua mambo mengi- hasa kwa kukuuliza maswali mbali mbalimbali.Toa majibu mazuri kwa mtoto ukiambatanisha na maarifa kutoka kwenye vitabu.

Kwa sasa najua sio tatizo tena kwa mzazi kusoma kitabu chenye tija ya maendeleo, hasa ukizingatia somo lilitolewa kupia makala ihusuyo mbinu 10 za kuanza kusoma kitabu chenye tija ya maendeleo kupitia http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/elimu-na-mtazamo-mbinu-10-za-kuanza.html?utm_source=BP_recent
Leo naomba ufuate nami katika hatua nyingine ya ujasiri na yenye mafanikio katika kumjengea mtoto wako uwezo na shauku ya kuwa msomaji wa vitabu.

1.     Kuwa mfano wa kuigwa katika kusoma kitabu…weka utaratibu unaoleweka na kufuatwa na familia kuhusu usomaji (najua hili sio tatizo tena kwa kuwa umesoma na kuzifanyia kazi mbinu 10 kupitia http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/elimu-na-mtazamo-mbinu-10-za-kuanza.html?utm_source=BP_recent
2.     Msomee mtoto wako kitabu na kumsaidia sehemu zenye utata (Zingatia umri na uelewa wa mtoto)

Picha na home-startwigtownshire.co.uk

3.     Mwekee mtoto utaratibu wa kusoma kitabu na kuwasilisha taarifa fupi mara amalizapo sehemu ya kitabu au kitabu chote…soma zaidi http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/malezi-na-elimu-ukitaka-mtoto-wako.html (Zingatia umri na uelewa wa mtoto)
4.     Jenga utamaduni wa kununua vitabu mbali mbali vyenye kuchochea maarifa kwako na kwa mtoto( unaweza kuweka utaratibu wa kununua vitabu 3-5 kwa mwezi)

5.     Mpongeze mtoto anapoonyesha juhudi ya kusoma kitabu-chagua zawadi zinazochochea usomaji zaidi mfano kumpeleka sehemu tulivu ya kuvutia ili kujisomea na kuburudika.(Zingatia hali ya kipato chako-huna sababu ya kujitetea, zipo sehemu nzuri za mapumziko zisizohitaji hata pesa)

Hongera sana kwa kutimiza zoezi hili!

Maarifa mengi sana yamefichwa kwenye vitabu…
Yapekue! Yasome!Yaelewe!Yafanyie kazi kwa dhati hasa yale yanayofaa kwa wakati husika.

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!
Ikiwa una maoni au una hitaji ushauri kuhusu usomaji wa vitabu ulio na manufaa,usisite kuwasiliana nasi. Hakuna gharama ya huduma hii!
0785 175 157                             Barua pepe:jielimishekwanza@gmail.com

Jumanne, 16 Julai 2013

ELIMU NA MTAZAMO: MBINU 10 ZA KUANZA KUSOMA KITABU CHENYE TIJA YA MAENDELEO


Nikizingatia makala iliyoandikwa kuhusu kuijua siri iliyopo ndani ya vitabu http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/ifahamu-siri-iliyopo-ndani-ya-vitabu.html unaweza kujua umuhimu au faida mbali mbali unazoweza kupata.
Imekuwa ni utamaduni wa Watanzania wengi na Waafrika wengi kupuuzia suala la usomaji vitabu hasa vyenye kujenga,kuongeza uwezo wa utendaji,kuamsha hisia za utendaji, na vingine vyenye maudhui chanya.
Kupitia makala tajwa nilieleza faida mbali mbali tunazoweza kuzipata moja kwa moja kwa kusoma vitabu.Tuondoe visingizio mbali mbali kuhusu suala zima la usomaji wa vitabu mfano suala la uvivu.
Picha na www.praesa.org.za
Napenda nikupe mbinu na hatua za kufuata ukitaka kusoma kitabu ukipendacho kuhusu maendeleo, ni vyema ukaanza kuzifanyia kazi hatua kwa hatua kama mtoto mdogo anavyojifunza (kama ilijulikanavyo na wasomi wengi kuwa ukitaka kujifunza vizuri ni vyema kujiweka kwenye nafasi ya mtoto):
1.Anza kusoma kitabu chenye kurasa chache
2.Chagua kitabu kinachoeleza wazo moja kwa kurasa moja au mbili
3.Una uhuru kuanza kusoma wazo lolote unalolipenda…si lazima uanze mwanzo wa kitabu
4.Jiwekee malengo ya kusoma kurasa moja au mbili kwa siku…unaweza kuongeza kutegemeana na uhitaji na shauku ya kusoma zaidi
5.Tumia kalamu ya kuweka kivuli kwa sehemu muhimu sana-zitakusaidia baadaye kuweka utekelezaji
6.Mara zote usiache kutembea na kitabu ukipendacho…unaweza kusoma muda wowote ukihitaji kusoma
7.Ukifanikiwa kutimiza mbinu 1,2,3,4,5,na kumaliza kusoma kitabu ulichokichagua, vuka hatua nyingine kubwa kuanza kusoma kitabu kingine ukiongeza idadi ya kurasa-hasa kile kinachotoa maelezo marefu kuhusu wazo moja kwa kurasa zaidi ya kumi.
8.Jichunguze uwezo na mapungufu yako kulingana na ujuzi uliopata kupitia kitabu ulichosoma.Chunguza fursa zilizopo katika nchi yako ukilinganisha na ujuzi ulioupata kwa kusoma kitabu.
9.Jipongeze unapomaliza kusoma kitabu kimoja na kujifunza mbinu mpya ya kuboresha maisha yako na ya wengine.
10.Chagua wazo moja au ujuzi uliopata kwa majaribio katika maisha halisi(weka katika utendaji).
Pia unaweza kutumia ipad yako kusoma kitabu ukitakacho.

Picha na app-of-ipad.blogspot.com
Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi  zifanyie kazi hizo mbinu 10,  pia tuungane wakati mwingine na makala “Mjengee mtoto wako tabia ya kusoma vitabu”.Makala  ijayo itakuwa ya msaada mkubwa endapo utakuwa kioo kwa mtoto kwa kutimiza hizo mbinu 10 kwa ukamilifu.
Usiposoma kitabu chochote, utapitwa na maarifa, utakosa fursa mbali mbali pia utaamini sana ufahamu wako(si kweli kuwa unafahamu vitu vyote zaidi ya wengine)...