inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 21 Machi 2015

MTAZAMO: WENGINE HUFANYA HIVI ILI UWATEGEMEE…

--> 
Picha na seriouslymen.com
Ifahamike kuwa binadamu haishi kama kisiwa; anaishi kwa kutegemea, kutegemewa pia kwa kutegemeana na wengine, pia viumbe hai na visivyo hai.Kusema hivi nakumbuka mwaka 2005-2009 nilipokuwa nikifundisha somo la “Elimu ya Viumbe-Baiolojia” katika mada ya Ikolojia ngazi ya shule za sekondari kuwa; viumbe hai (mimea na wanyama) hutegemeana pia hutegemea viumbe visivyo hai kama hewa, maji, ardhi n.k.Hii hupelekea kuwepo kwa mlishano wenye kutegemeana ili kuishi na kuendeleza kizazi.Napenda kukumbushia tu kuhusu kutegemeana!
Sihitaji kuingia ndani zaidi ya hapo, sipendi kuigeuza safu hii darasa la Baiolojia. Moja kwa moja nianze na safu hii kwa kumlenga binadamu nikidhamilia kurusha mkuki kwa watu wanaopenda wengine wawategemee kupita kiasi ili wawafanye watumwa/mateka wa fikra na hatimaye kupora uhuru wao.


Ndugu msomaji, ikiwa unahusika au huusiki kwa kuwafanya wengine wakutegemee kupita kiasi napenda nikujuze SIRI 10 zilizojificha na zinayoonekana kuwa hali ya kawaida katika maisha ya kila siku. Watu hao wanaoonekana au kujiona wajanja huwafanyia watu wengine yafuatayo kwa kujua au kutokujua ili kuwaweka kwenye mtego wa kuwa watumwa wao kifikra, kimtazamo, kiutendaji na waendelee kuwa tegemezi;

1.               HUWAPATIA WENGINE “Samaki Na Si Nyavu...”
Katika lugha rahisi ni kuwa hawakupatii ujuzi au mbinu au msaada ujikomboe mwenyewe na shida ulizonazo.Hutumia kanuni iliyoainishwa na mwandishi wa 48-Laws of Power akisema;  Never teach them enough so that they can do without you”. Katika tafsiri ya Kiswahili isiyo rasmi-Usiwafundishe vya kutosha ili washindwe kufanya lolote bila ya wewe”
2.           HUTOA MSAADA WA FEDHA KWA DHAMANA YA KITU KINGINE CHA THAMANI WANACHOONA WENGINE (WATUMWA WAO) WANACHO

Ikiwa unapokea msaada wa fedha kutoka kwa mtu wako wa karibu na kuwekewa sharti-nitakupatia fedha unazohitaji ukinipatia…...au “nakupatia hizi hela ila itabidi unipe……” ujue unakaribia kuingia kwenye mdomo wa simba.
3.               HAWAELEZI SIRI YA KUFANIKIWA KWAO
Watu au makundi ya watu wanaopenda uwategemee, hata siku moja hawatoi siri ya kufanikiwa kwao…wataeleza mafanikio yao juu juu tu katika lugha tamu iliyozoeleka na wengi kama kujituma na juhudi binafsi-hivyo watakuambia fanya kazi kwa bidii! Ni vigumu kwao kutoa ile silaha ya kufanikiwa kwao kwa watu wanaowachukulia kuwa watumwa au wategemezi wao.
4.       WANAKUCHAGULIA MARAFIKI
Ikiwa wamekuweka mikononi mwao; yaani unawategemea katika msaada, wataanza kukuchagulia marafiki wa kuambatana nao walio marafiki kwao na kutaka ujitenge na maadui wao au waliowazidi mbinu za kiuchumi.Haijalishi kama una urafiki wa karibu na hao maadui zao, itakulazimu tu ujitenge nao ili uendelee kupata msaada-ama sivyo msaada hakuna tena! Kufanya hivyo wanataka usizinduliwe kutoka usingizini na hao maadui zao.
5.       WATADHARAU/KUBEZA/KUYASHUSHA MAAMUZI/MAWAZO YAKO, Haijalishi Kama Yana Maslahi Kwako Katika Kukukomboa Na Utegemezi
Kama umezoea kwenda kuomba ushauri kwa mtu unayemtegemea sana akupe msaada, watu wenye kupenda uendeele kuwa mteja wa maamuzi yako watafanya kila hila kuhakikisha maamuzi au mikakati ya kuelekea kujinasua na utumwa/utegemezi inagonga mwamba. Watadharau na kukuona kuwa una mawazo mgando.
-->
Kufahamu jinsi ya kujikomboa na hali hii au utegemezi unaopelekea utumwa wa fikra na mtazamo: Tafuta na usome Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi? cha Mwandishi makini Henry Kazula.

Ikiwa unahitaji kujua zaidi SIRI 5 zilizobaki, tuma anwani ya barua pepe ukionyesha kuguswa na makala zetu kupitia jielimishekwanza@gmail.com, au tuma SMS yenye anwani yako kupitia 0754 572 143.Nasi bila hiyana tutakutumia makala hii yote, pia utakuwa wa kwanza kupata kila makala mpya kutoka Jielimishe Kwanza! Blog.

Jumamosi, 14 Machi 2015

MTAZAMO: KABLA HUJAHUKUMU WENGINE JITATHIMINI KWANZA!

-->
Maisha yetu ya kila siku tunakumbana na maswahibu mbali mbali yanayopelekea fikra na utashi wetu kuchukua maamuzi rahisi na wakati mwingine maamuzi magumu sambamba na kutoa hukumu kwa yatokanayo.
Ukweli mchungu na usio na kificho ni kuwa, kila siku katika hali yetu ya kibinadamu tunakalia kiti cha heshima cha uhakimu na kutoa hukumu kuwahukumu wengine isivyo haki na kweli  kutokana na makosa yatokanayo na maamuzi yao; maamuzi rahisi au magumu.
Kuna jambo la msingi la kuzingatia kwanza ikiwa tupo kwenye kiti cha kutoa hukumu; ni la kiimani, Sawa! (kama inayovyoaminiwa na baadhi ya dini) kuwa usihukumu wengine kabla hujahukumiwa-Mungu pekee ndiye wa kuhukumu kwa haki pia kabla ya kuwahukumu wengine tujichunguze/tujitathmini wenyewe kwanza; je tu wasafi?, je tupo katika upande wa kutenda haki au upande wa kupenda kutendewa haki?

Pia, tunapoonyeshea wengine kidole kwa kuhukumu, itambulike kuwa kuna vidole vitatu vinatonyeshea sisi; hii ina maana kubwa sana katika uumbaji wa Mungu-tujitathmini sisi kwa kina kwanza kabla ya kutoa hukumu kwa wengine.
Sehemu hii imekuwa ya msingi sana ili tuweze kutoa hukumu za kibinadamu zilizo za haki na zisizo na mawaa, ilhali Mungu pekee ndiye anayehukumu kwa Haki na Kweli!
Binadamu kwa asili, tunahukumu masuala mbali mbali ili kukosoa na kujiridhisha nafsi zetu.Hukumu zetu huambatana na mtazamo hasi kuhusu wengine, mfano: naweza kuona ndugu au rafiki yangu amekata mawasiliano na mimi kwa muda mrefu, hii inasumbua akili yangu na mwisho nashindwa kuchelea kutoa hukumu kwa maneno hasi (bila kujitathmini mimi kwanza kama sijamkwaza)- kuwa ndugu/rafiki yangu ameanza dharau siku hizi, anajisikia sana, ananionea wivu ameona nimemzidi kimaisha, yeye ameona kuwa mimi sifai na si wa hadhi yake, ameona atuendani kiuchumi na mengine mengi; haya ni baadhi tu ya majibu rahisi ya kupoza hisia ingawaje sijui kama natoa hukumu ya haki na kweli juu yake. Je,  ni kweli ipo hivyo? Vipi kama ana matatizo? Mara ngapi nimefuatilia kujua kuhusu ndugu/rafiki yangu? Ni mfano tu ndugu hakimu mwenzangu ambao umewahi kunitokea…nimejifunza na ninaendelea kubadilika kwa hili.Natumaini nawe utafanya juhudi kwa hili.
Sawa, tunaweza kuona ni jambo jema kwa kufurahisha nafsi zetu na kuwakosoa wengine kwa mapungufu yao lakini jambo la kuzingatia na la msingi, narudia tena kwa msisitizo; tujitathmini wenyewe kwanza ili hukumu zetu ziendane na matakwa ya Yule aliye Hakimu wa Kweli na Haki.
 “Kumpatia mtu silaha asiyohitaji na asiyoweza kuitumia ni sawa na kutompa kabisa, pia ni hatari; inaweza kumdhuru” –HenryKazula.
Maarifa kwa wanaohitaji maarifa, pia walioonyesha nia ya kuhitaji maarifa.Onyesha uhitaji wa maarifa,tutakuelimisha kutumia vizuri maarifa uliyopewa.
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.



Jumatatu, 9 Machi 2015

MTAZAMO: CHUNGUZA CHANZO CHA MATATIZO!


Picha na lauraecpaul.wordpress.com

Tunaishi katika dunia iliyozungukwa na matatizo kadha wa kadha yaliyo ya asili na mengine ni chanzo cha mwanadamu mwenyewe kwa kudharau mambo yanayoonekana kuwa ni madogo.
Matatizo yaliyopo huchochea fikra za mwanadamu katika kuelekea kutoa suluhisho au kutatua matatizo; mwisho wa siku imekuwa ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku kupambana na kukuna vichwa kutatua matatizo.
Mtazamo tofauti umejengeka na kuzoeleka kwa wanajamii katika kuelewa na kutatua matatizo, wengi hutizama matatizo pekee na kukurupuka kutoa majibu rahisi ya matatizo kwa hisia bila kuyafahamu matatizo yenyewe kwa kina na kujali chanzo cha matatizo hayo kwa kufanya uchunguzi au utafiti wa kina.Hii ni sahihi kurejea msemo huu wa Kiswahili-“usiangalie umeangukia wapi,angalia ulipojikwaa”.
Katika ulimwengu huu tunaoishi kuna matatizo kama nilivyosema awali; matatizo yana chanzo chake kama ilivyobainishwa na msemo wa kisayansi katika sheria ya mwanafalsafa Socratic- na sheria yake ya “law of causality”“The Law of Cause & Effect states that absolutely everything happens for a reason.” sheria hii ikiainisha wazi kuwa kila jambo hutokea kwa sababu maalum.
Tukitupia jicho upande mwingine wa kutoa au kutafuta suluhisho la matatizo duniani, mwana fisikia maarufu duniani- Albert Einstein  anatukumbusha kuwa; “We cannot solve our problems with the same thinking we used when we created them.” Akimaanisha kuwa matatizo hayapatiwi suluhisho kwa uelewa wetu ule ule uliotumika kuyatengeneza-hivyo tunahitaji kufikiri tofauti.
Einstein anasisitiza tena kwa kujiweka mwenyewe katika kuchunguza na kuelewa matatizo kuwa-“If I had an hour to solve a problem I'd spend 55 minutes thinking about the problem and 5 minutes thinking about solutions.”-Akimaanisha kuwa ni vizuri kutumia au kujipatia muda wa kutosha (wa dakika 55) kufikiri na kuelewa tatizo na hatimaye kutumia muda mchache (wa dakika 5) kutoa suluhisho ikiwa angepata saa moja kutatua tatizo fulani.
Nikutie ujasiri ndugu msomaji, hatupaswi kuwa watu wa kulalamika au kukata tamaa kutokana na matatizo yaliyopo na yanayoendelea kuwepo.Tunapaswa kutumia utashi au akili binafsi tuliyopewa na Muumba wetu kufikiri na kuyaelewa matatizo kwa kina-hasa chanzo chake kupitia tafiti na njia mbali mbali zilizotumika na wengine kwa kujielimisha kwanza hatimaye kupata suluhisho sahihi la matatizo yetu.
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.