inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 29 Januari 2015

TANGAZO:KITABU KILICHOKUWA KINASUBILIWA KWA HAMU KIPO MADUKANI SASA!


PIA KINAPATIKANA...

DAR ES SALAAM:

1.CCBC- SURVEY, NEAR MLIMANI CITY, WAY TO UDSM
                                Mawasiliano: 0769 644 338
 

2.MLIMANI CITY-NAKUMATT WITH "MAARUFU BOOKSHOP"

MOSHI:

CHRISTIAN BOOK SHOP (Jirani na stendi kuu ya mabasi moshi)

ARUSHA:


IRINGA:
LUTENGANO INVESTMENT BOOK POINT
Mawasiliano: +255(0) 762 941 311 


 PIGA
0754 572 143

KUWA WAKALA!



Jumanne, 27 Januari 2015

MTAZAMO: ANZISHA JAMBO KWA MINAJILI YA KULIKAMILISHA, HAKIKISHA UNALIKAMILISHA!

Picha:http://crossofglorylutheran.com/run-with-perserverance-822012/
-->
Ni jambo jema kuwa na mipango au malengo yenye mikakati madhubuti ya utekelezaji na si kuwa na malengo pekee, ingawa ni bora kuwa nayo kuliko kutokuwa nayo kabisa; kwa kuwa na malengo pekee bila mkakati wa utekelezaji ni sawa na matamanio-alisema Joel Osteen katika moja ya mafundisho yake. Dhana hii imeelezwa kwa kina katika mojawapo ya makala zilizosheheni ndani ya Jielimishe Kwanza!Blog ikiwa na mtazamo chanya kabisa wa kuchochea mabadiliko yenye chachu ya utekelezaji usiyokuwa na hofu ya kukata au kukatishwa tamaa na hatimaye kuishia njiani.
Ingawaje inaonekana ni rahisi kujiwekea malengo au mipango mbali mbali ya maisha na ya Taifa kwa ujumla ila msisitizo unawekwa zaidi na unaendelea kuwekwa katika kuhakikisha kuwa kuna utekelezaji! Na ikijitokeza kuwa kuna changamoto za kukamilisha malengo yaliyo katika hali ya utekelezaji; watu au wanajamii wengi huchukua uamuzi mrahisi mno wa kuachana na mbio za kuyafikia mafanikio tarajiwa.
Leo, naomba nikutie moyo ndugu msomaji kwa kuikumbuka historia isiyoweza kufutika duniani ya mwanariadha John Steven Akwari -kijana wa kitanzania ya mwaka 1968 kule Mexico kwenye mashindano ya Olimpiki. Akwari aliushangaza ulimwengu kwa kuendelea na mbio akiwa mtu wa mwisho ili kuhakikisha anamaliza safari yake licha ya kuwa na jeraha lenye bandeji mguuni kwake. Hiyo haikutosha, alishangaza zaidi na kuwahamasisha waliokata na wanaokata tamaa kupitia changamoto zisizotarajiwa kwa kusema kirahisi “ Nchi yangu haikunituma maili 5000 kuanza mbio, bali  ilinituma maili 5000 kumaliza mbio; alitoa jibu hili kwa ujasiri  pale alipoulizwa kwanini hakuachana na mashindano mara tu alipopata jeraha.
Ama kwa hakika, tukio hilo la kihistoria na maneno ya Akwari yanahamasisha na yanachochea uwajibikaji usio dhaifu, wenye kujali uzalendo, wenye shauku ya kufikia mafanikio, pia kipimo cha utu wa mwanadamu pale kutokeapo changamoto au vipingamizi katika kufikia kiu ya mafanikio.
Hivyo basi ndugu msomaji ni vyema kuhakikisha malengo uliyojiwekea yakiwa na mpango mkakati bila ya kukata tamaa ukiwa katikati ya mbio za kuelekea mafanikio.Hakikisha unaimaliza safari yako kuelekea mafanikio licha ya kuwepo changamoto au vipingamizi vya hapa na pale.
Imetayarishwa na
Henry Kazula,
Mwandishi wa Kitabu-MTAZAMO WAKO NI UPI?
Na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Ijumaa, 16 Januari 2015

MTAZAMO 2: (Cheza na Saikolojia, Usitumie nguvu) NJIA SAHIHI YA KUMWELEZA MTU MWINGINE SIRI YAKO NZITO


Kama tulivyoona wiki iliyopita kuwa kuna madhara makubwa ya kumweleza mtu mwingine SIRI yako uionayo kuwa ni nzito, kubwa zaidi likiwa ni lile la kupoteza uhuru wako.
Katika hali nyingine isiyo ya kawaida, wapo watu wengine hujisikia vizuri na huru zaidi wakielezea SIRI zao kwa wengine (wanajihisi kama wametua mzigo wa kitu fulani kutoka moyoni) lakini wakati huo huo hujitahidi kwa hali na mali kuilinda SIRI waliyoitoa isivuje.
Tuungane tena leo, ikiwa wewe huwezi kujizuia kutunza SIRI yako mwenyewe…yaani unaona kama inakuwasha na hivyo kuchukua hatua ya kumwambia mtu mwingine; fanya yafuatayo kujikinga na kupoteza uhuru wako wakati unapotaka kutoa SIRI yako kwa mtu mwingine:
1.Ifanye SIRI yako kuwa ya kawaida, ielezee kawaida na usimwonyeshe mwingine kuwa imeshikilia furaha ya maisha yako.
2.Angalia au chagua kwa uangalifu mtu wa kumwelezea SIRI yako, asiwe kama wewe uliyeshindwa kuitunza SIRI hiyo (…natania tu!)
3.Chagua wakati muafaka wa kueleza SIRI yako.Ikiwa umempata rafiki wa kumwelezea SIRI yako, jitahidi kusoma mazingira ya huyo unayetaka kumshirikisha SIRI yako.
4.Usionyeshe kutoa motisha ya aina yeyote ile kwa mtunza SIRI wako.Ikiwa mtunza SIRI wako anakutishia kuwa usipompa kitu fulani; mambo hadharani, mwonyeshe kuwa huna wasi wasi wowote.
Kuhusu SIRI, msemo huu wa Kiswahili unatawala-
“Hakuna SIRI ya watu wawili”.
Imetayarishwa na
Na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Alhamisi, 15 Januari 2015

MTAZAMO: SEHEMU 2-RUDISHA FURAHA ILIYOPOTEA KWA KUFANYA YAFUATAYO...

Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Ushauri zaidi: +255 754 572 143
________________________________________
 Soma SEHEMU YA 1 HAPA


Picha:http://www.hischerishedones.org
6.EPUKA KUKAA MAZINGIRA YA UPWEKE…
Upweke hupelekea huzuni na kupunguza furaha tuliyo nayo.Mazingira ya kujitenga na kuwa wewe ndiyo wewe kwa kukumbatia mawazo yaliyo hasi na masononeko huikimbiza furaha na kujiona kuwa ni mkosaji usiyestahili kuwepo duniani.
7.TAMBUA KUWA PESA PEKEE HAIWEZI KUKUPA FURAHA MAISHANI
Natumaini unakubaliana na mimi kuwa si kila mwenye pesa ana furaha wakati wote.Sawa! pesa ni sabuni ya roho kama walivyosema wahenga, lakini si kiashiria cha kumuweka mtu katika nafasi ya kuwa na furaha.Mtu aweza kuwa na pesa nyingi lakini akapungukiwa furaha. Hii ina maanisha kuwa pesa ni kitu kinachofuata baadaye baada ya kitu kisichohitaji pesa kukupa furaha.Bila shaka umeshuhudia jamii za watu waishio maisha yenye kipato cha chini lakini wana furaha iliyo kifani! Jifunze kutoka kwao upekee wa maisha walio nao na kuikubali hali halisi ya maisha na kuongeza juhudi kusonga mbele.
8.JIANGALIE ULIVYO, WEWE NI WA THAMANI SANA! HAKUNA MWINGINE KAMA WEWE (tumia hali uliyonayo kwa manufaa na kujiongezea furaha)…
Kama ilivyoelezwa awali kuwa binadamu tumeumbwa kwa upekee sana na kila mmoja ana uwezo, akili na kipaji kutofautiana na mwingine ili tufaidiane.Ikiwa mtu hajajitambua uwezo wake kwa jinsi alivyo, ni vyema kuchukua hatua madhubuti ya kujikubali kwanza na kujitathimini.Vile tulivyo yatosha kujitumia kujiongezea furaha na uthamani wetu.Ijulikane kuwa, hakuna mtu mwingine kama wewe.Jitambue, tumia uwezo ulio nao kuanza pale ulipo kwa kupenda unachofanya na kujiongezea furaha.
9.REKEBISHA TABIA YAKO INAYOWAKWAZA WENGINE…
Kuwa na mahusiano mema na jamii ya watu waliokuzunguka ni jambo zuri linalochangia furaha yako.Jitahidi kuondoa tofauti ulizo nazo na marafiki au watu wengine ili kuishi kwa amani, hii itakuweka huru na kukuongezea furaha yako.Hivyo basi, chukua hatua ya kujichunguza na kujirekebisha tabia yako iliyo kinyume na utaratibu wa maisha ya kawaida.
10. TAMBUA KUWA SI WOTE WENYE KUONYESHA MENO NJE (KUKENUA) WANA FURAHA MAISHANI.
Msemo huu wa Kiswahili-"Moyo unaweza kufurahi lakini macho yanalia" ni sawa kabisa na kinyume chake-"Macho yanacheka (kuonyesha furaha ya uso) lakini moyo unalia".Inamaanisha kuwa mtu aweza kuonyesha furaha ya uso kumbe moyoni ana chuki na majonzi au hasira.Hivyo, usiigize furaha kwa kuonyesha meno pekee ukajiita una furaha ya kweli, jitathimini na utafute au kufanya mambo yatakayokupa furaha ya kweli-furaha ya uso na ile ya moyoni.
Nakutakia kila la heri kurudisha furaha iliyopotea au inayoelekea kupotea kwa kufuata mambo 10 niliyoainisha kwa kina.
Imetolewa na,
Jielimishe Kwanza!

Jumatatu, 12 Januari 2015

MTAZAMO: KUWA MAKINI! KUMKABIDHI MTU MWINGINE SIRI YAKO NZITO UNAWEZA KUPOTEZA UHURU WAKO KAMA IFUATAVYO:

1.Utakuwa tayari kupokea kila sharti utakalopewa na huyo mlinzi wa SIRI yako.
2. Wakati wote utaishi kwa mashaka mashaka.Utahisi: labda SIRI ataivujisha nini? Vipi SIRI ikivuja itakuwaje? Nitaweka wapi uso wangu?
3.Hofu itatawala, kila umuonapo mlinzi wa SIRI yako.Utahisi: labda anataka kusema kitu fulani kuhusiana na SIRI yangu nini?
4.Utajikuta ukitumia pesa kinyume na utaratibu ili kuilinda SIRI isivuje.Mlinzi wa SIRI yako asikohoe kidogo tu kuhusu shida ya pesa, utampatia!…utahisi kuwa usipompatia atavujisha SIRI.
5.Utakuwa mtumwa tu! hasa ukimwona mlinzi wa SIRI yako akiwa na rafiki zako wa karibu wakijadili jambo na kucheka  ukitazama. (Ilihali wana mambo yao mengine tu) Utahisi: Ameshawaambia SIRI yangu…
Kuhusu SIRI, msemo huu wa Kiswahili unatawala-
“Hakuna SIRI ya watu wawili”.
Pia hatupaswi kutawaliwa na hisia kupita kiasi!
Kwa wale wasioweza kukaa na SIRI zao-wanaona zinawawasha, tuungane siku kama ya leo ili nikujuze njia sahihi ya kumweleza mtu mwingine SIRI yako na usipatwe na hayo 5 niliyoyaainisha.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Jumapili, 11 Januari 2015

UTAMADUNI:JE, WEWE NI MSWAHILI WA KWELI? SIKILIZA HII...

Msikilize mkuu wa mkoa wa Dodoma, Dr.Rehema Nchimbi akiongea na wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).Najua hii itakuhusu tu! Msikilize kwa makini akianisha sifa za Mswahili wa kweli. Je, wewe ni Mswahili wa kweli? Imetolewa kupitia redio-TBC FM katika kipindi cha "Kumepambazuka Kiswahili".

...

Imekujia kwa udhamini wa Jielimishe Kwanza!

Jumatano, 7 Januari 2015

MTAZAMO: RUDISHA FURAHA ILIYOPOTEA KWA KUFANYA YAFUATAYO…



________________________________________ 

Picha:http://www.hischerishedones.org
Furaha ni hali ya kibinadamu inayotawaliwa na hisia au akili, hujitokeza kiasilia kwa kuchangiwa na mazingira mazuri yanayomzunguka mtu katika shughuli zake za kila siku.Humfanya mtu kujisikia vizuri, kujihisi kutosheka. Pia, ni kichocheo cha kusonga mbele kiutendaji na kuboresha maisha.

Kila mtu anapenda au anahitaji kuwa na furaha wakati wote.Swali la msingi la kujiuliza; Je, inawezekana kuwa na furaha wakati wote? Kiuhalisia, mwanadamu ameumbwa kukutana na changamoto mbali mbali zichocheazo utashi wake au hisia zake.Uwezo wa asili na akili ya binadamu kupambana na kushinda changamoto hizo huongeza furaha.Lakini, si kila changamoto iliyopo na inayojitokeza hupelekea furaha…kuna wakati hali huwa kinyume na matarajio kiasi cha kupoteza furaha. 
Shughuli za binadamu na mwenendo wa maisha yetu huchangia kwa kiasi kikubwa katika kuikaribisha au kuikimbiza furaha iliyo asili ya mwanadamu, ondolea mbali mambo tusioweza kuyazuia kama kifo, magonjwa, dhoruba mbali mbali n.k. Hivyo basi, si jambo rahisi kuwa na furaha wakati wote! Hii ni sawa sawa na kusema hatuwezi kuipata furaha ya milele tungali tunaishi katika dunia hii yenye kila aina ya udhalimu na maovu.
Ingawaje hatuwezi kuwa na furaha wakati wote, tumaini lipo na tunaweza kuirejesha furaha iliyopotea kutokana na mambo yaliyo katika uwezo wa kibinadamu hasa kutokana na maisha ya kila siku na shughuli mbali mbali za kila siku.
Je, umepoteza furaha kwa kufeli mtihani?, kukosa ajira?, kukimbiwa na marafiki?, kutengwa na ndugu?, kuachwa/kukimbiwa na akupendaye(mke/mume au mchumba?), kuchekwa na watu kwa jinsi ulivyo? na hali nyingine zinazofanana na hizo? Usikate tamaa wala kurudi nyuma.Chukua hatua hizi 10 za ujasiri au ushujaa kufanya yafuatayo; (leo zitaainishwa 5):


1.ACHA KUNUNG’UNIKA, CHUKUA HATUA YA KUANZA UPYA!
Jinsi unavyoendelea kunung’unika ni dhahili kuwa hali itaendelea kuwa jinsi ilivyo na ndivyo fursa nyingi zitakapokupita.Manung’uniko huchochea hasira na chuki hivyo kuzidi kuipoza furaha yako. Hivyo, ni vyema kuacha kunung’unika na kuchukua hatua ya ujasiri kuanza upya, anzia ulipo ukiboresha mapungufu yaliyopo.
2.USIGEUKE NYUMA/USIKUMBUKE YALIYOPITA, SONGA MBELE!
Hakuna kitu kibaya kama kuendelea kukumbuka maumivu au matukio mabaya yaliyopita! Shukrani kwa Mungu hata kutuumbia hali ya kusahau…katika hali hii, kusahau mabaya hutupatia mtazamo chanya wa kuyaona maisha katika sura iliyo rafiki na kutujengea furaha nyingine.Songa mbele, jiwekee mkakati wa kutokumbuka yaliyopita.Najua kuwa kuna matukio mengine ni vigumu kuyasahau-lakini jitahidi kujibidisha, kuna wakati utafika na kuiona furaha yako ikirejea.
3.TAMBUA KUWA, ULIVYOVIPOTEZA HUKUZALIWA NAVYO…
Ni jambo la kipekee sana kumshukuru Mungu kwa kuwa tunaishi! Vile tulivyo ni upekee tuliopewa.Tumezaliwa na kuvikuta vitu na watu mbali mbali.Pia tunategemeana katika masula mbali mbali katika kuendesha gurudumu la maisha.Ni ukweli usiopingika kuwa hakuna kitu tumezaliwa nacho…vingi tumevikuta na tunavitafuta kila kukicha.Pia, vingine ni vigumu kuvirudisha katika hali ya mwanzo.Hivyo,tunavyovipoteza visitukatishe tamaa na kupoteza furaha zetu.Tunapaswa kuanza upya kuanzia pale tulipo kama ilivyoelezwa katika hatua mbili zilizopita.
4.USIJIONE KUWA NI WEWE PEKEE MWENYE SHIDA IPELEKEAYO KUKOSA FURAHA…
Hatua hii inanifanya nikukumbushe moja ya makala zetu yenye kichwa Tambua kuwa wengine pia wana shida zao”kwa mantiki kuwa hakuna mtu asiye na shida; tunatofautiana jinsi ya kuziona shida na kupambana nazo.Ikiwa umepatwa na maswahibu yapelekeayo kupoteza furaha yako, ni vyema kutafakari kuwa hauko peke yako…yawezekana wewe una unafuu mkubwa kuliko wengine wenye shida.
5.JIJENGEE MTAZAMO MPYA WA MAISHA ULIO CHANYA…
Katika kitabu “MTAZAMO WAKO NI UPI? Mtazamo Wako, MaishaYako” kinaeleza na kuhamasisha mtazamo ulio chanya kwa kuwa maisha yetu hutawaliwa kwa kiasi kikubwa na mtazamo tulio nao na tunaotaka kuwa nao.Jitahidi kujiepusha na hali au mazingira yenye kukatisha tamaa, hali ya majonzi na kusononeka nafsi (mtazamo hasi) ili kuijenga na kuiimarisha furaha iliyo asili yetu. 
Tukutane tena siku nyingine kama hii tumalizie hatua 5 zilizobaki.
Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Ushauri zaidi +255 (0) 754 572 143
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.

Ijumaa, 2 Januari 2015

WATU MASHUHURI HUTUMIA SIRI HII KUWATEKA WAFUASI WAO…


…ifahamu siri hiyo ili kujizolea mashabiki na kusikilizwa!
Picha na albertaventure.com
Kwa kipindi kirefu Jielimishe Kwanza! Blog imekuwa ikifuatilia kwa ukaribu sana tabia au hulka za watu mbali mbali walio mashuhuli. Mwishowe kubaini kuwa watu hao wana hulka zinazofanana kupelekea mafanikio yao.
Utafiti huu unanikumbusha mshangao wa Profesa mmoja katika chuo kikuu cha “Nelson Mandela African Institution of Science and Technology” cha Arusha-Tanzania ambaye alipigwa na butwaa kuona /kusikia wanamuziki wa kizazi kipya almaarufu kama “Bongo Flavor” nchini Tanzania wanavyokuwa maarufu kuwapita Maprofesa wote wa vyuo vikuu. Hakupata jibu la swali lake na kuishia kupigwa na butwaa.
Naomba nimsaidie Profesa huyo na watu wengine wanaoendelea kujiuliza swali kama lake kwa kuwafunulia siri ya mafanikio ya vijana hao na watu wengine mashuhuri.
Kama nilivyoeleza awali, watu hawa mashuhuri wana hulka au tabia zinazofanana kupelekea siri ya mafanikio yao. 
JIPATIE KITABU " MTAZAMO WAKO NI UPI? Mtazamo Wako, Maisha Yako" kuifahamu SIRI hiyo iliyoainishwa katika moja ya SURA zilizosheheni ndani ya kitabu hiki, uweze kuitumia ili kufanikiwa. PIGA +255 754 572 143
https://www.facebook.com/pages/Mtazamo-Wako-Ni-Upi/1527825034153354

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza! Social Enterprise.