inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 28 Juni 2015

BIASHARA: TAMBUA UKWELI HUU MCHUNGU; KWA NINI BIDHAA ZA MAKAMPUNI YA KIMTANDAO (MULTI-LEVEL MARKETING-MLM COMPANIES) NI GHARAMA?

                Picha na shutterstock
Biashara iendeshwayo na Makampuni ya Kimtandao almaarufu kama “Multi-Level Marketing (MLM) Companies”  imeshamili na kuwa ni gumzo kwa takribani zaidi ya muongo mmoja katika nchi zinazoendelea (Afrika- Kenya, Nigeria, Ghana, Zimbabwe, Namibia, Afrika Kusini….), ingawaje tafiti zinaonyesha kuwa ilianza kwa mara ya kwanza miaka ya 1940s nchini Marekani. Hivyo basi biashara hii si mpya kama wengi wanavyofikiria na kuwaaminisha wengine.  Nchini Tanzania kampuni nyingi za MLM huingia nchini kupitia nchi ya Kenya, nisingependa kuzianisha,; unazifahamu na yawezekana nawe upo huko na umekwisha jijengea fikra ya “be your own boss” kwa kuwatoa wengine sadaka kama wasambazaji ili ufaidike kwa kupanda cheo kupitia ngazi (levels) mbali mbali kama zilizokubaliwa na kampuni unayoitumikia.
Kutokana na ukimya na sintofahamu nyingi kuhusu uwepo na gharama kubwa katika bidhaa zinazosambazwa kupitia MLM, Jielimishe Kwanza Blog tumeona ni vyema tuvunje ukimya huu kupitia kufanya utafiti wa kina kuhusu Makampuni yanayojihusisha na MLM na kukushirikisha.
Makampuni hayo yanayojihusisha na biashara ya Kimtandao  hutengeneza na kuuza bidhaa wanazoziamini sana na kuwaaminisha wengine kuwa zinatibu magonjwa sugu, kuboresha kinga ya mwili, kuthibiti uzito na mwisho wa yote ni ahadi kem kem za maisha bora yenye uhuru wa kipato na ile ya “kumiliki biashara yako mwenyewe”.
Swali la msingi ambalo kila Mtanzania anapenda kujua ni hili la kuwepo kwa gharama kubwa ya bidhaa zinazozalishwa na makampuni ya MLM. Kupitia utafiti binafsi wa Jielimishe Kwanza Blog! umebaini yafuatayo;
Tracy Coenen- mtaalamu wa masuala ya Intelijensia na upelelezi wa masuala ya biashara anasema kuwa; "The truth is that products are overpriced through multi-level marketing companies because they have to pay commissions to distributors on many levels." That’s the whole point of multi-level marketing: Many levels of distributors get a piece of the action when you buy something. Akimaanisha kuwa, gharama kubwa husababishwa na kuwalipa bakshishi/sehemu ya faida ya mauzo wasambazaji walio wanachama wa Kampuni husika.Pia huwalipa kutokana na kuwashawishi wengine kutumia na kujiunga na Kampuni husika. Bila shaka umewahi kusikia kuwepo kwa makampuni hayo hapa kwetu Tanzania yakihamasisha wengine kujiunga nao kupitia bidhaa zao, na yawezekana u mmoja wao.
Kutokana na maelezo na mafundisho yao, husingizia kuwa bidhaa zao ni bora zaidi kuliko bidhaa nyingine duniani…yaani ni kama zimeshushwa kutoka mbinguni.Tuwe na uhalisia katika hili!
Imefika wakati wa kufumbuka macho Watanzania, tusitamanishwe na mafanikio hewa kwa kutumika na wengine. Hakuna urahisi unaopatikana katika biashara hizo hasa unapoaminishwa kuwa utakuwa na uhuru wa kipato na kumiliki biashara yako mwenyewe…Biashara yako mwenyewe?...wakati unawekewa masharti na watu wengine? Mfano: hakikisha unaingiza watu 2 kwa wiki, kununua na kutumia bidhaa ndipo upate gawio la faida.Cha kusikitisha zaidi huwezi kujiunga na Makampuni hayo na kupata gawio la faida kubwa kama hujanunua bidhaa kwa gharama kubwa, kuuza bidhaa zao kwa bei waliopanga na kushirikisha wengine wajiunge kwa kuwahamasisha na kuwaaminisha kama ulivyoaminishwa kuwa zitawatoa pale walipo kimaisha. Kuhamasisha wengine wajiunge ni silaha kubwa katika kampuni hizo. Usipofanya hivyo hutaona faida ya biashara hii na mwisho wa siku itakushinda! 
Robert FitzPatrick mwandishi wa “Pyramid Scheme Alert” pia mtafiti wa masuala ya biashara za mtandao (MLM) anaweka bayana kuhusu suala zima la kuhakikisha wengine wanajiunga katika kampuni ndipo mhusika apate gawio la faida litokanalo na gharama kubwa ya kila bidhaa; “For there to be a “winner” at the top, there must be “losers” below. The ratio of losers to winners is pre-determined, usually 100 to 1.” Profit Reserved only for those at the Top. Hivyo katika wengi (watu 100) waliohamasishwa na kujiunga kama wasambazaji anayefaidika zaidi ni mtu 1 tu! Yaani, ili mtu mmoja ayaone mafanikio ya kweli ndani ya kampuni ni lazima watu 100 chini yake wapate hasara. Huu ni ukweli mchungu ambao hufichwa na washiriki wa makampuni hayo. Ndiyo maana kila kukicha wanawaza kuingiza watu wapya katika kampuni. Ki uhalisia utafanikiwa kwa kuwekeza zaidi muda wako na pesa nyingi katika kampuni hizi ili upate mafanikio si kutokana na kupendwa sana na Makampuni yao, ila ni hela na muda uliowekeza kuisaidia kampuni kutimiza malengo yake. Ndiyo maana tunapingana vikali na dhana ya kusema kuwa “be your own boss” katika biashara hii.
Siri kubwa ya makampuni hayo ni wewe kuhakikisha unahamasisha wengine wajiunge kuwa wasambazaji na watumiaji wa bidhaa zao ndipo ulipwe…hii si kazi rahisi kama wanavyoeleza na kurahisisha katika mafundisho yao. 
Nasisitiza tena, Watanzania tufumbuke macho, tusome, Tujielimishe Kwanza kabla ya kutaka kupapatikia biashara zinazoonekana kuwa na mteremko ilihali hatujui yaliyojificha; mbele kukiwa na mlima mkubwa unaolighalimu taifa katika siku za usoni.
Chaguo ni lako, kujiunga au kutokujiunga na Makampuni hayo.Ukitaka kutoka nayo kimaisha, wekeza zaidi muda na pesa yako, hamasisha wengine wakubali kujiunga.
Pia kuwa makini; kuna bidhaa kama za Makampuni ya MLM zina gharama nafuu sana na zinafanya kazi vizuri na zina ubora zaidi ya hizo za MLM. 
Usidanganyike na urembo au madoido ya vifungashio vya bidhaa hizo, zipo kama kivuli cha kuficha ujanja ujanja unaofanywa na wamiliki wa Makampuni ya MLM.
Huo ndiyo ukweli unaofichwa ili kuneemesha wengine.
Ukiwa na maoni, manung’uniko na kuhitaji ufafanuzi zaidi usisite kutuandikia.
Imetolewa na,
Jielimishe Kwanza!




Jumamosi, 20 Juni 2015

MTAZAMO: TAMBUA UWEZO WAKO KIUTENDAJI, USISUBIRI KUAMBIWA!

Picha na www.trinityp3.com
-->
Wengi hujiuliza, mimi nikiwa mmoja wao; hivi utendaji kazi wangu unaendana na matakwa ya mwajiri au malengo ya kazi niliyojiwekea? Wengi wao hushindwa kupata majibu sahihi kupitia uhakiki au tathmini binafsi “self- assessment” kutokana na kukosekana kwa mbinu stahiki. Hii imepelekea wengi kuwa tegemezi kwa kupata tathmini zisizokidhi kiu zao kutoka kwa wengine kuhusu utendaji kazi wao; ingawaje ni jambo jema pia kupata tathmini ya wengine kukuhusu na kuhusu utendaji kazi wako.
Kutegemea tathmini ya wengine pekee kuhusu utendaji kazi wetu inaweza isiwe njia sahihi zaidi kuliko ile binafsi-“self assessment” kutokana na kuwepo kwa ubinafsi/ unafsi na roho za korosho au roho za kwanini yeye? baina ya mfanyakazi mmoja na mwingine, kadhalika kati ya mfanyabiashara mmoja na mwingine.Hakuna anayependa mafanikio ya mwingine katika utendaji kazi na biashara.
Katika karne hii ya utandawazi iliyo na mabadiliko kila kukicha, bila kusahau ubunifu wenye ushindani mkubwa -ujulikanao kama "creative destruction" kama alivyowahi kuainisha Joseph Schumpeter (1883–1950), ni muhimu kutambua kuwa upo umuhimu mkubwa wa kujitathmini mwenyewe kiutendaji ili kuboresha mapungufu uliyo nayo kwa haraka zaidi ukiendana na uhitaji wa soko la ajira au biashara.Ubunifu wenye tija unahitajika sana katika wakati huu tulio nao.
Kwa bahati nzuri sana; kumekuwepo na tafiti mbali mbali zinazohamasisha kujifanyia tathmini binafsi ya kiutendaji kabla ya kuomba ridhaa ya wengine kututathimini. Michelle Roccia, mtendaji msaidizi wa kitengo cha “Employee Engagement” katika kampuni ya WinterWyman anasema; “The self-assessment is an essential part of performance evaluation because it's an opportunity for you to assess your own achievements. You own the performance appraisal. You should look across the past year and tell your manager what you've done and areas you'd like to focus on," Anasisitiza kuwa tathmini binafsi ya kiutendaji ni fursa kwako kujua maendeleo na mafanikio katika utendaji kazi wako.Pia ni kipimo cha utendaji wa kazi au biashara yako.Kwa kuzingatia mwaka uliopita unaweza kujionea ni maeneo yapi unayopaswa kuweka maboresho na msisitizo zaidi ili kuongeza uzalishaji.
Ford Myers, mwandishi wa kitabu "Get The Job You Want, Even When No One's Hiring anaongezea tena kwa kukazia fikra kuhusu “self-assessment” akisema kuwa; "It's an opportunity for you to reflect on how you're doing in your career, not just your job".Use it to think about where you are going long-term and where you are in your career. Akimaanisha kuwa; tathmini binafsi ni fursa kwako kuvuta taswira ya jinsi unavyofanya katika ujuzi na utendaji wako na si kazi pekee. Itumike kutafakari kwa kina kuhusu mwenendo wako kiutendaji na wapi ulipo kiutendaji.
Pia tathmini binafsi hupelekea kujiongezea sifa katika soko la ajira-bringing value to the market place; kama alivyosema Jim Rohn. Mtu binafsi kwa kufanya tathmini binafsi anaweza kujifunza mbinu mbali mbali za kujiongezea utendaji kazi zinazohitajika katika soko la biashara au ajira kutokana na mapungufu au uhitaji alio nao.
Ukizingatia faida tajwa za kujifanyia tathmini binafsi ya kiutendaji, ni vyema kuanza sasa kuangalia wapi ulipo katika utendaji kazi wako; ikiwa unafanya kazi bora upate ujira pekee au unafanya kazi ili kujiongezea fursa za kupata pesa zaidi; utaamua wewe.
 Nimeandika makala hii kwa makusudi kabisa ikiwa ni sawa na “kurusha jiwe kwenye giza nene”; yeyote atakayepiga kelele huko, limempata kwa nafasi yake kiutendaji.Utaangalia ni eneo gani upo katika utendaji kazi, hivyo anza sasa kujitathmini mwenyewe, usisubiri kuambiwa na wengine kwa kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. Najua kuna swali mahsusi unataka kuuliza tena; nawezaje kujitathmini mwenyewe?  How can I make self -assessment?
Ungana nami wakati mwingine kama huu utajibiwa bila hiyana ikiwa tu utaniandikia kuhusu kuguswa na makala hii.
 Whatsapp +255(0) 754 572 143
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-“Mtazamo Wako Ni Upi?”
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!