inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 18 Aprili 2015

AJIRA:KUACHISHA KAZI: AINA NA TARATIBU ZAKE ZA KISHERIA.

--> 
Na Emmanuel C. Zongwe

Mtaalamu wa Masuala ya Mahusiano Mahali pa Kazi.
 ____________________________________________



Picha na www.gradientpixels.ca
 
UTANGULIZI
Kuachisha kazi kwa ujumla maana yake ni kumalizika/kuvunjika kwa mkataba wa ajira kati ya muajiri na muajiriwa. Kwa maneno mengine, ni kumalizika kwa mahusiano ya kiajira kati ya muajiri na muajiriwa. Kusitishwa kwa mahusiano hayo kunaweza kuanzishwa na upande wowote wa mkataba huo (muajiri au muajiriwa).
Katika Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini (Kanuni za Utendaji Bora) za mwaka 2007, imeelezwa kuwa kuachishwa kazi kazi itakuwa ni apamoja na:-
a)   Kuachisha kazi chini ya Sheria ya Kimila ya Uingereza (Common Law).
b)   Muajiri kusababisha ugumu kwa muajiriwa kuendelea na ajira.
c)   Kushindwa kuongeza mkataba wa muda maalum kwa masharti yaleyale au yanayofanana kama kulikuwa na matumaini ya kuongeza mkataba.
d)  Kushindwa kumruhusu mfanyakazi kurejea kazini baada ya likizo ya uzazi au ulezi.
e)   Kushindwa kumuajiri tena mfanyakazi pale ambapo muajiri amewaachisha kazi wafanyakazi kadhaa kwa sababu kama hiyo au zinazofanana na ametoa nafasi z ajira kwa baadhi ya wafanyakazi walioachishwa kazi tu.
KUACHISHA KAZI KIHALALI
Katika Sheria ya Kimila ya Uingereza (Common Law), kuachisha kazi kihalali kumeelezwa kuwa ni pamoja na :-
     i.         Kuachisha kazi kwa makubaliano – hapa ni pale ambapo muajiri na muajiriwa wanakuwa wamekubaliana kusitisha mahusiano yao ya kiajira. Kwa mfano; kama mkataba wa ajira ni wa mwaka mmoja na muda huo umekwisha, hapo mkataba huo utakuwa umefikia ukomo.
   ii.         Ajira kukoma yenyewe – hapa ni pale ambapo mkataba wa ajira unakuwa umesitishwa katika mazingira kama kifo au kumalizika kwa shughuli ya muajiri.
 iii.         Kuachishwa kazi kunakofanywa na muajiri – muajiri pia anaweza kusitisha mkataba wa ajira lakini itampasa kwanza kuzingatia na kufuata taratibu za kisheria.
Ø Katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini na. 6 ya mwaka 2004 kumetajwa vigezo vine ambavyo vinahalalisha uachishaji kazi unaofanywa na muajiri. Vigezo hivyo ni pamoja na:-
a)   Mwenendo mbaya (misconduct)
b)   Kutokuwa na uwezo (incapacity)
c)   Kutohitajika (incompatibility)
d)  Mahitaji ya kiuendeshaji (operational requirement)

  iv.         Ukatishwaji wa ajira unaofanywa na muajiriwa – hapa ni pale ambapo mfanyakazi analazimika kuacha kazi baada ya muajiri kuvunja mkataba wa ajira baina yake na muajiriwa.
Ø Katika Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini (Kanuni za Utendaji Bora) za mwaka 2007, Kanuni ya 7 (1) inasema kuwa, “… pale ambapo muajiri anafanya ajira kushindwa kuvumilika, ambapo inaweza kusababisha muajiriwa ajiuzulu, kujiuzulu huko kutakuwa sawa na kuacha kazi kwa kulazimika.”
Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini na Kanuni zake, pia imeeleza kuwa ili kuachisha kazi kuwe ni halali basi ni lazima kuwe na sababu halali na ya haki (valid and fair reason) na utaratibu wa haki (fair procedure) uwe umefuatwa. Muajiri anapaswa kuwa na sababu halali na awe amefuata utaratibu wa haki katika kumuachisha kazi muajiriwa.
Taratibu za kuachisha kazi zinatofautiana kulingana na sababu inayopelekea kuachisha kazi, lakini taratibu zote hizo ni lazima zimpe muajiriwa nafasi ya kusikilizwa kabla ya uamuzi wa kumuachisha kazi. Bila kujali uzito wa kosa lililofanywa na muajiriwa, bila kujali kuwa muajiri wake ana ushahidi wa kutosha, ni lazima kisheria kufuata taratibu za kumuachisha kazi kama zilivyoelezwa katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini na. 6 ya mwaka 2004 na Kanuni zake za mwaka 2007.
Kushindwa kufuata taratibu hizo kutamaanisha muajiriwa ameachishwa kazi bila kupewa nafasi ya kujitetea (summary dismissal). Kutokumpa muajiriwa nafasi ya kujitetea au kujieleza ni kumnyima haki yake ya kisheria. Kwa mujibu wa Sheria za kazi, kuachisha kazi kwa namna hii ni sawa na kuachisha kazi kusivyo halali (unfair termination).
Endapo itathibitika kuwa kuachisha kazi kulikofanywa na muajiri si halali inaweza kuamuriwa kuwa muajiri atekeleze moja ya mambo yafuatayo kwa mfanyakazi/muajiriwa husika.
1.   Kumrudisha muajiriwa kazini (reinstatement) – hapa muajiriwa atarudishwa kazini na itahesabika alikuwepo kazini kutokea siku alipoachishwa kazi na atastahili kulipwa stahiki zake alizostahili kulipwa kwa kipindi chote tangu kuachishwa kwake. Pale ambapo amri ya kumrudisha muajiriwa kazini imetolewa na muajiri ameshindwa kutekeleza amri hiyo, atapaswa kumlipa mfanyakazi huyo fidia ya mishahara ya miezi isiyopungua kumi na mbili (12) na stahiki nyingine alizostahili kulipwa tangu kuachishwa kwake.

2.   Kumuajiri upya mfanyakazi kwa masharti mapya yatakayoamuliwa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi au Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi (Labour Court). Endapo muajiri atashindwa kutekeleza amri hii, atalazimika kulipa fidia ya mishahara ya miezi isiyopungua kumi na mbili pamoja na stahiki nyingine ambazo muajiriwa alistahili kulipwa tangu siku aliyoachishwa kazi isivyo halali.

3.   Kumlipa mfanyakazi fidia ya mshahara wa miezi isiyopungua kumi na mbili. Pamoja na fidia hiyo, pia atalazimika kumlipa stahiki zake nyingine anazostahili kulipwa kwa mujibu wa Sheria yoyote ile au makubaliano yoyote yaliyokuwepo kati ya muajiri na muajiriwa.
Imetolewa na
 Jielimishe Kwanza





Jumanne, 14 Aprili 2015

MTAZAMO: JIJENGEE FALSAFA BINAFSI YA MAISHA YAKO-“Building Your Philosophy of Life” .



Picha imetolewa Jukwaa huru

Neno “falsafa” kama lilivyoainishwa na tovuti ya Mwanahalisi Forum, ni imani aliyonayo mtu juu ya jambo au kitu fulani.Katika maana halisi ya neno "falsafa" kwa Kigiriki-"philosophy" lenye muunganiko wa maneno mawili; philo=love na sophia=wisdom (love of wisdom) lina mantiki kubwa katika kuhamasisha, kuchokoza fikra, hisia na ufahamu; kubwa zaidi ni kupenda kutenda mema. 
Mtandao wa Mwanahalisi Forum unafafanua zaidi kuwa; kila mwanadamu aliye timamu katika maisha anaongozwa na vitu vitatu ambavyo ni FALSAFA, MTAZAMO na MSIMAMO, vitu hivi huwa ndiyo dira ya mwanadamu katika maisha yake. Mambo hayo matatu ndiyo hufanya wakati mwingine watu kutofautiana au kuwa kitu kimoja.
Jicho letu linapenda kuangazia zaidi kuhusu kuijenga “falsafa binafsi ya maisha”-“philosophy of life” iliyo kanuni au utaratibu anaojiwekea mtu binafsi; bila kushurutishwa na mtu mwingine ikiwa ni dira ya maisha yenye kutoa maamuzi ya busara, yasiyo na kikwazo kwa maisha ya mtu au watu wengine.  
Tukiangazia fikra zetu zaidi katika falsafa ya maisha iliyo dira ya maisha ya mtu binafsi ni vyema kujua umuhimu wa kuunda falsafa binafsi ya maisha na kujua jinsi ya kuijenga falsafa hiyo ndani ya maisha yetu kwa lengo la kutawala maisha yetu.
Umuhimu Wa Kuunda Falsafa Binafsi Ya Maisha
Kama ilivyoainishwa awali, falsafa binafsi ya maisha yetu ni dira inayoongoza na kutawala upeo wa maisha yetu; hutupatia faida mbali mbali kwa kuzingatia uwezo wetu wa ndani katika kutoa maamuzi yaliyo sahihi na yasiyo kinzana na maadili ndani ya jamii husika.
Ndugu msomaji, natumaini unafuatana nami ili kuepusha mkanganyiko wa kimtazamo na kifikra…hivyo basi, nikujuze umuhimu wa kuwa au kuunda falsafa binafsi ya maisha kama hukuwa nayo, na kama ulikuwa nayo kujifunza zaidi kuiimarisha kwa mafanikio maishani.
1.FALSAFA BINAFSI HUTUEPUSHA NA HATARI MBALI MBALI KATIKA KUTOA MAAMUZI SAHIHI…
2.HUTOA MWONGOZO WA MAISHA YETU...falsafa ya maisha ni dira ya maisha yetu!
3.HUTUEPUSHA KUWA WATUMWA WA MAWAZO YA WENGINE…ikiwa tumekosa falsafa thabiti ya maisha yetu, ni rahisi kwa watu wengine kutambua mapungufu yetu hivyo kutuingia kifikra na kutawala mawazo na mtazamo wetu pasipo kujua.
4.HUTUJENGEA MSIMAMO THABITI KATIKA MAAMUZI YETU…Huepusha kuyumbishwa na msimamo wa watu wengine kuhusu sisi.Msimamo wetu ulio thabiti hudhihirisha ukweli wa vile tulivyo; hututambulisha kwa wengine vile tulivyo.
5.HUTUEPUSHA KUWA BENDERA FUATA UPEPO…hivyo kuongeza heshima na kuonyesha busara zetu kwa wengine katika kutoa maamuzi sahihi.
6.HUSABABISHA KUWEPO KWA MAHUSIANO MEMA NA WATU WENGINE…falsafa yetu iliyo na tija maishani huwavuta wengine kwetu na kujenga mahusiano mema.
Fahamu kwa undani jinsi ya kuijenga falsafa binafsi kwa kubofya HAPA
Tunakutakia kila la heri katika zoezi hili muhimu la kujijengea falsafa yako.
Imetayarishwa na,
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!


Alhamisi, 9 Aprili 2015

AJIRA: USITISHWAJI WA AJIRA KWA SABABU YA UTOVU WA NIDHAMU MAHALA PA KAZI

-->
Picha na dailyjobads.com
Usitishaji wa ajira ni kukoma  kwa ajira (mkataba wa ajira) kunakosababishwa na mambo mbalimbali kama; mfanyakazi kujiuzulu (kuacha kazi kwa hiari), muajiri kusababisha mazingira magumu kwa muajiriwa kuendelea na kazi, muajiri kushindwa kumruhusu muajiriwa kurudi kazini baada ya likizo (ya uzazi au ya mwaka) na mfanyakazi kuachishwa kazi kwa utovu wa nidhamu.
Utovu wa nidhamu ni sababu kubwa inayoweza kupelekea kusitisha ajira. Hata hivyo muajiri hapaswi kuchukua hatua zozote za kinidhamu dhidi ya muajiriwa mpaka pale atakapokutana naye kwanza na kujadili suala hilo. Pia katika Kanuni za Utendaji Bora Mahala pa Kazi za mwaka 2007 imeelezwa wazi kuwa muajiri anapaswa kuweka kanuni za kusimamia nidhamu zinazoeleza namna mfanyakazi anavyopaswa kuzingatia nidhamu mahali pa kazi. Muajiri anapaswa kuwafahamisha wafanyakazi kanuni hizo wakati wa kuajiri.
Kama hiyo haitoshi, Kanuni hizo pia zimetoa muongozo/utaratibu wa kusitisha ajira kwa sababu ya utovu wa nidhamu. Kabla ya kumuachisha kazi mfanyakazi, muajiri anatakiwa kufikiria kwa umakini na kuzingatia mambo yafuatayo:-
    i.         Je, mfanyakazi amekiuka kanuni za nidhamu za kampuni/ taasisi?
  ii.         Je, kanuni iliyokiukwa ni ya msingi na haki?
iii.      Je, kanuni iliyokiukwa inaeleweka kwa mfanyakazi na haina utata? Na
iv.         Je, kanuni iliyokiukwa imekuwa ikitumika na muajiri kwa usawa?
Katika Kanuni za Utendaji Bora Mahala pa Kazi za mwaka 2007, Kanuni ya 12 (2) imeelezwa kuwa kosa la kwanza la mfanyakazi halihalalishi adhabu ya kuachisha kazi isipokuwa pale itakapothibitika kuwa kosa ni kubwa kiasi cha kuharibu uhusiano wa kiajira kiasi cha kutovumilika. Pia katika Kanuni ya 12 (3) yametajwa makosa makubwa yanayoweza kuhalalisha mfanyakazi kuachishwa kazi kwa kosa la kwanza. Makosa hayo yametajwa kuwa ni pamoja na:-
a)   Kukosa uaminifu kulikokithiri
b)  Kuharibu mali kwa makusudi
c)   Uzembe uliokithiri
d)  Kuhatarisha usalama wa watu wengine kwa kukusudia
e)   Kushambulia wafanyakazi wengine, wateja au mtu mwingine yeyote mwenye kuhusiana na muajiri
f)    Ukaidi uliokithiri.
Pamoja na muajiri kuweza kumuachisha kazi mfanyakazi mara moja kutokana na makosa yaliyoainishwa hapo juu, Kanuni zimeweka utaratibu wa haki ambao muajiri anapaswa kuufuata kabla ya kuchukua hatua za kinidhamu juu ya mfanyakazi anayetuhumiwa kwa  kosa la kinidhamu.
Kabla ya kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya mfanyakazi mtuhumiwa, muajiri anatakiwa kufanya uchunguzi ili kubaini iwapo kuna haja ya kuitisha kikao cha nidhamu. Muajiri atakapobaini kuwa ipo haja ya kuitisha kikao cha nidhamu atapaswa kufanya mambo yafuatayo:-
    i.         Kutoa kwa mfanyakazi taarifa ya tuhuma kwa namna ambayo mfanyakazi ataelewa tuhuma hizo.
  ii.         Kumpa mfanyakazi muda usiopungua saa 48 ili aweze kuandaa utetezi wake.
iii.         Kumueleza mfanyakazi haki yake ya kuwasilishwa na mfanyakazi mwenzake au kiongozi wa chama katika kikao cha nidhamu.
iv.         Kuteua mwenyekiti wa kikao hicho ambaye hajahusika na tatizo lililopelekea kuitishwa kwa kikao cha nidhamu.
   v.         Kumpa mfanyakazi nafasi ya kuwahoji mashahidi wa muajiri na ikibidi kuleta mashahidi wake.
vi.         Kikao kitakapothibitisha tuhuma dhidi ya mfanyakazi mtuhumiwa, muajiri atoe nafasi kwa mfanyakazi kueleza hoja ya kupunguziwa adhabu.
vii.         Kutoa nafasi kwa mtendaji wa chama kuwakilisha katika kikao hicho endapo mfanyakazi mtuhumiwa ni kiongozi au muwakilishi wa chama mahali pa kazi.
viii.         Endapo adhabu inayokusudiwa ni kuachisha kazi, muajiri ni lazima aeleze sababu na pia aeleze haki ya mfanyakazi kukata rufaa.
ix.         Kumpa mfanyakazi nakala ya fomu ya kusikilizia shauri la kinidhamu baada ya kikao.
Pamoja na uwepo wa taratibu hizi, mara kwa mara waajiri wamejikuta wakiingia kwenye migogoro ya kiajira dhidi ya wafanyakazi kwa kuzikiuka.
Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini na. 6 ya mwaka 2004 na Kanuni zake za mwaka 2007 imeweka utaratibu huu ili kupunguza au kumaliza kabisa tatizo la waajiri kusitisha ajira au kuachisha kazi wafanyakazi kwa makosa ya kubambikiwa, lakini pia kumfanya mfanyakazi azingatie suala la nidhamu mahali pa kazi.
Imeandaliwa na Emmanuel C. Zongwe kwa msaada wa vitabu vya sheria na machapisho mbalimbali.
Emmanuel C. Zongwe ni msomi na mtaalamu wa masuala ya Ajira na Mahusiano Mahali pa Kazi. Pia ni Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Mashambani na Kilimo (TPAWU), Wilaya ya Mufindi, Iringa.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.

Jumapili, 5 Aprili 2015

MTAZAMO: IMARISHA MTAZAMO WAKO KWA MAFANIKIO MAISHANI…


Katika kitabu chetu kinachofanya vizuri sokoni cha-Mtazamo Wako Ni Upi? Mtazamo Wako, Maisha Yako Na Mwandishi makini Henry Kazula ananukuliwa akisema; “Mtazamo ulio nao kukuhusu ukilinganisha na ule wa wengine unakuwa uhalisia wako kama utaamini” una mantiki kubwa hasa katika kuamini kuwa mtazamo tulionao unakuwa halisi katika maisha yetu kama tutajilinganisha na wengine. Mfano: ikiwa kimtazamo tutaamini kuwa wote waliofanikiwa wamepitia “njia za panya”; ndivyo itakavyokuwa! Hivyo utajijengea mtazamo hasi kuwa watu wote waliofanikiwa wana mafanikio yasiyo halali, ilhali kuna njia kem kem za halali kufikia mafanikio maishani.Mtazamo huo hutufanya watumwa wa mtazamo wa wengine bila kujijua, yaani kupitia mtazamo huo unaamua hatma ya mtazamo wetu tusipochukua hatua za makusudi kujifunza kwa makini kupitia hao waliotuzidi.
Hatupaswi kuwa watumwa wa mtazamo kupitia mtazamo wa wengine tunaowaona wametuzidi kimaisha. Zaidi ya yote, hatupaswi kuruhusu mtazamo wa wengine uamue hatma ya mtazamo wa maisha yetu.
Tunapaswa kujijengea mtazamo wetu ulio thabiti kupitia kujifunza kutoka mtazamo wa wengine kutuhusu kwa kuzingatia kuundwa kwa falsafa binafsi ya maisha yetu. Hii inamaanisha kuwa; mtazamo wetu ulio “jicho la rohoni” kama ilivyo kwa dhamiri –“sauti ya ndani” huunda falsafa binafsi ya maisha yetu.
Jim Rohn-mmoja wa waandishi na msemaji mashuhuri wa hadhara duniani anaainisha ukweli na umuhimu wa kuwa na falsafa binafsi ya maisha kwa kusema; Jijengee falsafa ya maisha yako-“philosopy of lifeikiwa ni dira inayosimamia, kutawala na kuongoza maisha yako.Pia hutuepusha  na hatari mbali mbali ikiwa sambamba na kuingia kwenye mkenge wa kutawaliwa na wengine kifikra na kimtazamo.
Swali la msingi kujiuliza ndugu msomaji; je, tunaimarishaje mtazamo wetu ili kujijengea falsafa binafsi yenye mafanikio maishani? Ikiwa unahitaji kutoka hatua moja hadi nyingine ya kimtazamo kuwa chanya kwa kuzingatia uundwaji wa falsafa binafsi hauna budi kuzingatia  yafuatayo;
 1.KUSOMA VITABU
Ni ukweli usiopingika kuwa kusoma vitabu mbali mbali ili kujitambua kunachangia kujenga mtazamo thabiti unaopelekea kujijengea falsafa binafsi ya maisha.Hii ni njia nzuri kuweza kujua mtazamo wa wengine kukuhusu wewe na kujitathimini kujenga na kuimarisha mtazamo wako.Soma hii kufahamu SIRI iliyopo ndani ya vitabu.
2.NI VYEMA KUHOJI KWANINI
Soma hii kujifunza kuhoji kwanini….
3.JIFUNZE KWA UZOEFU BINAFSI
Jifunze kupitia makosa.Soma hii
4.JIFUNZE KWA KUTAZAMA WENGINE
Njia mojawapo ya kujifunza ni kuwa mtazamaji mzuri wa yale yanayotokea kwa wengine.Utagundua makosa yao na mbinu walizotumia kuondoa makosa.Kupitia njia hii utajifunza mbinu mbali mbali kutoka kwa watu tofauti kuimarisha mtazamo wako. 
5.CHUKUA HATUA YA UJASIRI KUTUMIA MBINU ULIZOJIFUNZA KWA VITENDO
Kujifunza bila vitendo ni sawa na kutojifunza kabisa.Soma hii kujua zaidi.
____________________________________________________
Wakati mwingine nitajikita kwa undani kuelezea kuhusu “Kujijengea Mtazamo na falsafa binafsi ya maisha yako-“philosopy of life”.
Imetayarishwa na,
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!