inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 16 Januari 2015

MTAZAMO 2: (Cheza na Saikolojia, Usitumie nguvu) NJIA SAHIHI YA KUMWELEZA MTU MWINGINE SIRI YAKO NZITO


Kama tulivyoona wiki iliyopita kuwa kuna madhara makubwa ya kumweleza mtu mwingine SIRI yako uionayo kuwa ni nzito, kubwa zaidi likiwa ni lile la kupoteza uhuru wako.
Katika hali nyingine isiyo ya kawaida, wapo watu wengine hujisikia vizuri na huru zaidi wakielezea SIRI zao kwa wengine (wanajihisi kama wametua mzigo wa kitu fulani kutoka moyoni) lakini wakati huo huo hujitahidi kwa hali na mali kuilinda SIRI waliyoitoa isivuje.
Tuungane tena leo, ikiwa wewe huwezi kujizuia kutunza SIRI yako mwenyewe…yaani unaona kama inakuwasha na hivyo kuchukua hatua ya kumwambia mtu mwingine; fanya yafuatayo kujikinga na kupoteza uhuru wako wakati unapotaka kutoa SIRI yako kwa mtu mwingine:
1.Ifanye SIRI yako kuwa ya kawaida, ielezee kawaida na usimwonyeshe mwingine kuwa imeshikilia furaha ya maisha yako.
2.Angalia au chagua kwa uangalifu mtu wa kumwelezea SIRI yako, asiwe kama wewe uliyeshindwa kuitunza SIRI hiyo (…natania tu!)
3.Chagua wakati muafaka wa kueleza SIRI yako.Ikiwa umempata rafiki wa kumwelezea SIRI yako, jitahidi kusoma mazingira ya huyo unayetaka kumshirikisha SIRI yako.
4.Usionyeshe kutoa motisha ya aina yeyote ile kwa mtunza SIRI wako.Ikiwa mtunza SIRI wako anakutishia kuwa usipompa kitu fulani; mambo hadharani, mwonyeshe kuwa huna wasi wasi wowote.
Kuhusu SIRI, msemo huu wa Kiswahili unatawala-
“Hakuna SIRI ya watu wawili”.
Imetayarishwa na
Na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni