inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 27 Januari 2015

MTAZAMO: ANZISHA JAMBO KWA MINAJILI YA KULIKAMILISHA, HAKIKISHA UNALIKAMILISHA!

Picha:http://crossofglorylutheran.com/run-with-perserverance-822012/
-->
Ni jambo jema kuwa na mipango au malengo yenye mikakati madhubuti ya utekelezaji na si kuwa na malengo pekee, ingawa ni bora kuwa nayo kuliko kutokuwa nayo kabisa; kwa kuwa na malengo pekee bila mkakati wa utekelezaji ni sawa na matamanio-alisema Joel Osteen katika moja ya mafundisho yake. Dhana hii imeelezwa kwa kina katika mojawapo ya makala zilizosheheni ndani ya Jielimishe Kwanza!Blog ikiwa na mtazamo chanya kabisa wa kuchochea mabadiliko yenye chachu ya utekelezaji usiyokuwa na hofu ya kukata au kukatishwa tamaa na hatimaye kuishia njiani.
Ingawaje inaonekana ni rahisi kujiwekea malengo au mipango mbali mbali ya maisha na ya Taifa kwa ujumla ila msisitizo unawekwa zaidi na unaendelea kuwekwa katika kuhakikisha kuwa kuna utekelezaji! Na ikijitokeza kuwa kuna changamoto za kukamilisha malengo yaliyo katika hali ya utekelezaji; watu au wanajamii wengi huchukua uamuzi mrahisi mno wa kuachana na mbio za kuyafikia mafanikio tarajiwa.
Leo, naomba nikutie moyo ndugu msomaji kwa kuikumbuka historia isiyoweza kufutika duniani ya mwanariadha John Steven Akwari -kijana wa kitanzania ya mwaka 1968 kule Mexico kwenye mashindano ya Olimpiki. Akwari aliushangaza ulimwengu kwa kuendelea na mbio akiwa mtu wa mwisho ili kuhakikisha anamaliza safari yake licha ya kuwa na jeraha lenye bandeji mguuni kwake. Hiyo haikutosha, alishangaza zaidi na kuwahamasisha waliokata na wanaokata tamaa kupitia changamoto zisizotarajiwa kwa kusema kirahisi “ Nchi yangu haikunituma maili 5000 kuanza mbio, bali  ilinituma maili 5000 kumaliza mbio; alitoa jibu hili kwa ujasiri  pale alipoulizwa kwanini hakuachana na mashindano mara tu alipopata jeraha.
Ama kwa hakika, tukio hilo la kihistoria na maneno ya Akwari yanahamasisha na yanachochea uwajibikaji usio dhaifu, wenye kujali uzalendo, wenye shauku ya kufikia mafanikio, pia kipimo cha utu wa mwanadamu pale kutokeapo changamoto au vipingamizi katika kufikia kiu ya mafanikio.
Hivyo basi ndugu msomaji ni vyema kuhakikisha malengo uliyojiwekea yakiwa na mpango mkakati bila ya kukata tamaa ukiwa katikati ya mbio za kuelekea mafanikio.Hakikisha unaimaliza safari yako kuelekea mafanikio licha ya kuwepo changamoto au vipingamizi vya hapa na pale.
Imetayarishwa na
Henry Kazula,
Mwandishi wa Kitabu-MTAZAMO WAKO NI UPI?
Na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni