inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 24 Desemba 2014

TAMBUA KUWA WENGINE PIA WANA SHIDA ZAO…


Naandika makala hii nikiburudika na muziki pia maneno ya msingi kutoka moja ya mstari wa wimbo-“Sugua gaga” wa mwanamuziki maarufu wa “bongo flava” nchini Tanzania- Sara Kaisi almaarufu “Shaa”. Katika mstari huo anasema; “…kama una shida unamwambia nani? hata mimi za kwangu nimeacha nyumbani” akimaanisha kila mtu ana shida zake.Ama kwa hakika wasanii wa nchini Tanzania wanajitahidi kwa ubunifu katika kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa jamii kupitia muziki, huyu ni miongoni mwa wasanii walionukuliwa katika KITABU chetu kitakachotoka mapema mwaka 2015.Wasanii wengine utakuwa umeona tulivyowanukuu na kuendelea kuwanukuu katika makala zetu kutokana na sehemu za mashairi yao yenye kukonga nyoyo na kufikisha ujumbe mahsusi kwa jamii.
Sasa turudi kwenye mada iliyopo mezani, wengine wana shida zao. Katika maisha ya kila siku iendayo kwa Mungu, kila mtu hupatwa na maswahibu au shida mbali mbali. Watu hutofautiana sana katika ujasiri na uvumilivu wa shida mbali mbali. 
Watu wengine ni wavumilivu sana kukumbatia shida zao na kupambana kwa njia moja au nyingine kupata suluhisho. Wapo makini sana kutoa shida zao kwa wengine. Huamini kuwa unapotoa shida yako kwa kila mtu ni kujidhalilisha na kujishusha thamani, hivyo basi huamua “kufa na tai shingoni” kuhusiana na shida zao.
Pia wapo wengine walio waoga sana kwa shida-wakiamini kuwa ni wao pekee duniani wenye shida. Kundi hili halitulii kukaa na shida, hivyo humweleza kila mtu wanayemfahamu shida zao. Bila kuchagua aina ya watu wa kuwaeleza shida zao; imewapelekea kukosa msaada na mwisho wa siku kuishia kutangazwa na kukimbiwa mara wawapo na shida. Hii imetokana na wao kuwa wavivu wa kuwajibika katika kutatua shida zao na kuwa tegemezi kwa wengine kupita kiasi.
Ndugu msomaji, nimeamua kuainisha makundi hayo mawili kwa kuzingatia uwezo wa kila kundi kuhimili na kustahimili shida ili iwe rahisi kwako kujichagulia kundi ulipendalo au kujiimarisha katika kundi husika kwa manufaa ya maisha yako. Suala la msingi la kuzingatia ni kuhakikisha kuwa shida uliyonayo haiwasumbui wengine. Pia kujitafutia watu au mtu sahihi ambaye mtakuwa mkisaidiana.
Sitarajii kueleweka vibaya kuwa nahamasisha watu wasisaidie wenye shida, hapana! Nafanya hivyo kwa mapenzi mema ili kuhamasisha uwajibikaji wa kila mwanajamii katika kujiinua kimaisha na si kuwa tegemezi kupita kiasi. Fuatilia zaidi KITABU chetu kitakachohamasisha badiliko la kimtazamo na uwajibikaji ulio na uhusiano wa machaguo mbali mbali ya maisha bila kuwakwaza au kuwatwisha wengine majukumu.
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni