inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 15 Januari 2015

MTAZAMO: SEHEMU 2-RUDISHA FURAHA ILIYOPOTEA KWA KUFANYA YAFUATAYO...

Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Ushauri zaidi: +255 754 572 143
________________________________________
 Soma SEHEMU YA 1 HAPA


Picha:http://www.hischerishedones.org
6.EPUKA KUKAA MAZINGIRA YA UPWEKE…
Upweke hupelekea huzuni na kupunguza furaha tuliyo nayo.Mazingira ya kujitenga na kuwa wewe ndiyo wewe kwa kukumbatia mawazo yaliyo hasi na masononeko huikimbiza furaha na kujiona kuwa ni mkosaji usiyestahili kuwepo duniani.
7.TAMBUA KUWA PESA PEKEE HAIWEZI KUKUPA FURAHA MAISHANI
Natumaini unakubaliana na mimi kuwa si kila mwenye pesa ana furaha wakati wote.Sawa! pesa ni sabuni ya roho kama walivyosema wahenga, lakini si kiashiria cha kumuweka mtu katika nafasi ya kuwa na furaha.Mtu aweza kuwa na pesa nyingi lakini akapungukiwa furaha. Hii ina maanisha kuwa pesa ni kitu kinachofuata baadaye baada ya kitu kisichohitaji pesa kukupa furaha.Bila shaka umeshuhudia jamii za watu waishio maisha yenye kipato cha chini lakini wana furaha iliyo kifani! Jifunze kutoka kwao upekee wa maisha walio nao na kuikubali hali halisi ya maisha na kuongeza juhudi kusonga mbele.
8.JIANGALIE ULIVYO, WEWE NI WA THAMANI SANA! HAKUNA MWINGINE KAMA WEWE (tumia hali uliyonayo kwa manufaa na kujiongezea furaha)…
Kama ilivyoelezwa awali kuwa binadamu tumeumbwa kwa upekee sana na kila mmoja ana uwezo, akili na kipaji kutofautiana na mwingine ili tufaidiane.Ikiwa mtu hajajitambua uwezo wake kwa jinsi alivyo, ni vyema kuchukua hatua madhubuti ya kujikubali kwanza na kujitathimini.Vile tulivyo yatosha kujitumia kujiongezea furaha na uthamani wetu.Ijulikane kuwa, hakuna mtu mwingine kama wewe.Jitambue, tumia uwezo ulio nao kuanza pale ulipo kwa kupenda unachofanya na kujiongezea furaha.
9.REKEBISHA TABIA YAKO INAYOWAKWAZA WENGINE…
Kuwa na mahusiano mema na jamii ya watu waliokuzunguka ni jambo zuri linalochangia furaha yako.Jitahidi kuondoa tofauti ulizo nazo na marafiki au watu wengine ili kuishi kwa amani, hii itakuweka huru na kukuongezea furaha yako.Hivyo basi, chukua hatua ya kujichunguza na kujirekebisha tabia yako iliyo kinyume na utaratibu wa maisha ya kawaida.
10. TAMBUA KUWA SI WOTE WENYE KUONYESHA MENO NJE (KUKENUA) WANA FURAHA MAISHANI.
Msemo huu wa Kiswahili-"Moyo unaweza kufurahi lakini macho yanalia" ni sawa kabisa na kinyume chake-"Macho yanacheka (kuonyesha furaha ya uso) lakini moyo unalia".Inamaanisha kuwa mtu aweza kuonyesha furaha ya uso kumbe moyoni ana chuki na majonzi au hasira.Hivyo, usiigize furaha kwa kuonyesha meno pekee ukajiita una furaha ya kweli, jitathimini na utafute au kufanya mambo yatakayokupa furaha ya kweli-furaha ya uso na ile ya moyoni.
Nakutakia kila la heri kurudisha furaha iliyopotea au inayoelekea kupotea kwa kufuata mambo 10 niliyoainisha kwa kina.
Imetolewa na,
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni