inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 12 Mei 2013

ELIMU YA JINSIA: TATIZO LA MHEMKO:Zifahamu mbinu za kupambana na mihemko hasa katika umri wa shule...


Picha na batonrougecounseling.net
-->

-->
Wanafunzi wengi kuanzia darasa la tano hadi kuelekea sekondari huwa katika umri wa kubarehe (wavulana) na kuvunja ungo (wasichana) ambao huwa na changamoto nyingi zinazoweza kupelekea kushuka kwa taaluma zao kama hawatajitambua.

Hii ni hatua kubwa katika makuzi na maendeleo ya kijana inaanzia umri wa miaka 12-18.Mwanasaikolojia Erick Erickson aliainisha bayana kuwa katika kila hatua ya makuzi na maendeleo ya mwanadamu kuna changamoto, na kila changamoto inapaswa kupitiwa na kushinda. Hivyo katika makuzi na maendeleo ya mwanadamu hupambana na vikwazo hivi ili kufanikiwa kuendelea hatua nyingine kwa mafanikio. 
Kama nilivyosema awali, wanafunzi wengi huwa katika  umri wenye mabadiliko makubwa ya ujinsia ambayo huendana sana na kutamani kujihusisha na tendo la ndoa.
Ni katika hatua hii wanafunzi na vijana wa umri huu hujiamini na kuona wanaweza kufanya lolote hapa duniani.Tukumbuke kuwa huu ni wakati wao muhimu kujifunza na kuandaa maisha yao wenyewe, ila wanakuwa wanapambana na hali ya matamanio ya mwili.
Ili kufanikiwa katika masomo ni vyema waweze kushindana na kupambana na hali hii ya matamanio ambayo kama mwanafunzi au kijana hatakuwa makini basi huweza kuharibikiwa kiafya na kiakili.Hatari kubwa kuliko ni kuweza kupata magonjwa ya zinaa na UKIMWI, na ujauzito katika umri mdogo bila kutarajia, pia kupoteza uelekeo wa maisha.
Vijana wanapaswa kujitambua kuwa hiki ni kipindi cha mpito, hivyo ni vizuri kuwa makini ili waweze kutimiza malengo yao katika maisha.
 ____________________
Mwanafunzi au kijana aweza kukishinda kipindi hiki cha makuzi kwa kuzingatia yafuatayo:  
1. SHIRIKI KATIKA IBADA MARA KWA MARA
Kumjua Muumba wako hasa kwa kupitia neno lake utajifunza njia nzuri ya kuishi na jamii, pia kujitambua. Utajifunza kufuata sheria zilizopo kwenye maandiko zikiwa kama mwongozo wa maisha na malengo yako.
2.EPUKA KUANGALIA PICHA ZINAZOCHOCHEA NGONO  
Katika mabadiliko makubwa ya sayansi na teknolojia, mambo mengi yamerahisishwa kwa faida na hasara.Picha zinazochochea ngono zipo nje nje kupitia sinema, mikanda ya video na intaneti.
 Ningependa kukushauri mwanafunzi na kijana, tumia teknolojia kwa faida ikiwa ni kutafuta masuala yanayoendana na masomo na kutafuta pesa kwa njia halali. 
3.JIWEKE MBALI NA MAKUNDI YENYE TABIA MBAYA
Kipindi cha shule ni kipindi chenye marafiki wengi; wazuri na wabaya.Epuka sana marafiki wanaoweza kukupeleka katika njia zisizofaa kama ulevi,uvutaji sigara na bangi.Matumizi ya vilevi huchochea ngono hata kufikia hatua ya ubakaji. 
4.SHIRIKI KWENYE MICHEZO
Kama inavyoshauriwa na wataalamu wa sayansi ya afya kuwa michezo huboresha afya ya mwili na akili.Kuna faida lukuki za kujihusisha na michezo, moja ni kukuondolea mawazo ya kujihusisha na ngono hii ni kwa sababu unakuwa umechoka hivyo utahitaji kupumzika. 
5.JIEPUSHE NA UPWEKE
Hakuna kitu kibaya kama upweke.Hali hii hukupelekea kuwa na mawazo mbali mbali hasa yakilenga kupambana na hali hiyo.
Mama Teresa aliwahi kusema umasikini mkubwa kuliko wote ni upweke, na kujifikiria hupendwi" kwa lugha ya kiingereza inasomeka “The most terrible poverty is loneliness, and the feeling of being unloved.” Mother Teresa.
Bila kujijua, upweke unaweza kukufanya  ushawishike kujiingiza kwenye mahusiano ukidhani upweke utaisha.Kupambana na tatizo la upweke fuata mbinu namba 3,5 na 6.  
6.JIBIDISHE NA MASOMO, SOMA VITABU
Ukijibidisha na masomo utajikuta tu upo "busy" na hivyo kuweza kutimiza majukumu ulipewa shuleni hivyo kuongeza ufaulu wako.
Pia, ukisoma vitabu vya lugha na maarifa vitakujenga kiakili na maarifa, hivyo kujiongezea upeo wako wa kufiriki.Hivyo basi unaweza kugundua wito wako na kipaji chako na mwishowe utajitambua.
7.JIPANGIE RATIBA UTAKAYOIFUATA WIKI NZIMA
Wataalamu wa masuala ya kutunza muda wamethibitisha kuwa mtu asiyejua mpangilio wa mambo yake kwa siku nzima ni sawa sawa na mfu au bendera inayofuata upepo. Hivyo, weka utaratibu wa siku kwa wiki nzima kimaandishi utakaouheshimu na kuufuata.  
8.USIOGOPE KUOMBA USHAURI
Watumie wazazi, walimu na ndugu waliokuzidi umri ili wakushauri pale unapoona mambo hayaendi sawa.
Najua katika umri wenu kiasilia huchukulia kuwa wakubwa hawakuwahi kupitia hatua kama hiyo ya makuzi.
Naomba nikuhakikishie kuwa watumie hao wakubwa wakupe ushauri, wanayajua hayo mapitio.
9.SHIRIKI KWENYE MIDAHALO YA VIJANA
Ushiriki wako katika midahalo yenye kuelimisha vijana kuhusu mwenendo wa maisha ni muhimu sana.Kupitia mafunzo hayo utajitambua na kuishi kwa malengo, wakati huo huo ukipata fursa ya kujieleza na kuboresha uwezo wako wa kuwasiliana na kujiamini mbele ya kadamnasi.

Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.



Maoni 1 :