inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 13 Mei 2013

UJASIRIAMALI: NEEC NA UDEC YAANZISHA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA WAHITIMU VYUO VIKUU NCHINI.

Jumatatu, 13 Mei 2013

Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ushirikiano na Kitivo cha Ujasiriamali cha Chuo kikuu

Picha na Henry Kazula-Mshiriki wa mafunzo
cha Dar-es -salaam (UDEC) wamefanikiwa kuanzisha mafunzo kwa wahitimu na wajasiriamali wanao chipukia wa vyuo vikuu  leo katika Chuo kikuu cha Dar es salaam.

Katibu Mtendaji wa Dkt. Annacleti Kashuliza akifungua mafunzo hayo ya wiki 3 kwa Vijana 40 waliohitimu shahada mbali mbali katika vyuo vikuu tofauti nchini, ameeleza changamoto mbali mbali Taifa  ilizonazo kuhusiana na ukosefu wa ajira kwa vijana.

Aliianisha kuwa ajira ni chache, hivyo ni vyema vijana  wakawezeshwa kujiajiri, pia kuweza kuajiri vijana wengine.

Hata hivyo, Dkt. Annacleti Kashuliza alitoa sababu mbali mbali zinazopelekea vijana wengi kushindwa kujiajiri; moja ni ukosefu wa mbinu za kuendesha biashara, kukosa mitaji, kukosa taarifa sahihi kuhusu biashara na kushindwa kupata mitandao ya kusonga mbele kibiashara.

Hivyo basi, mafunzo hayo yaliyoanza leo tarehe 13 Mei 2013 hadi 31 Mei 2013 yanalenga kuwajengea vijana uwezo katika miraji waliyoianza na pia kuweza kuboresha mawazo mbali mbali ya miradi ya biashara tarajiwa.

Sambamba na mafunzo hayo vijana watapata fursa ya kuonana na kuongea na wajasiriamali vijana waliofanikiwa ili kushirikishwa uzoefu.Pia kuunganishwa na mitandao mbali mbali ya kupata mikopo.

Imeandikwa na Henry Kazula.
Jielimishe Kwanza!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni