inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 3 Mei 2015

MTAZAMO: NJIA TANO (5) ZA KUWAFANYA WATU WENGINE WAKUAMINI KWA NIA NJEMA KABISA.

-->
Picha imetolewa na www.eppgroup.eu
Mafanikio yako katika kuwagusa wengine kwa mawazo yako ni ule uwezo binafsi wa kuwafanya wengine wakuamini.Pia jinsi ya kuwasiliana na kufuatilia mazungumzo na wengine hujenga uwezo na hali ya kuaminika kwa wengine.
Hata siku moja huwezi kutimiza azma yako ya kufikisha mawazo yako kwa wengine kuhusu biadhaa, huduma au suala lenye mustakabali kwa maendeleo ya jamii kama tu hawakuamini au huaminiki.
Ni sawa kabisa kuwa watu wanaweza kukusikiliza kwa makini lakini wasitendee kazi mawazo au ushauri wako; hii ndiyo hali halisi hadi watakapopiga hatua nyingine ya ujasiri kukuamini kwa kuwaaminisha kupitia vile ulivyo sanjali na unayoyasema.
Ukiwa muuzaji bidhaa, je watu watanuua bidhaa yako kama hawaiamini? La hasha! Inatakiwa uweze kuwaaminisha umuhimu na ubora wa bidhaa. Katika kuweka msisitizo wa jambo hili, Mwandishi wa kitabu “Start With Why”-Simon Sinek anasisitiza kwa kusema kuwa;  “People don't buy what you do; they buy why you do it. And what you do simply proves what you believe”. Katika tafsiri ya Kiswahili-“Watu hawanunui unachofanya, hununua kwa nini unafanya unachofanya.Unachofanya hutosha kuwaaminisha unachoamini”.
Ukiwa kama mkuu wa ofisi (Manager), unayetaka wengine wakubaliane na matakwa yako au utaratibu fulani; utaanza kujiuliza, je wananiamini? Hii ni kwasababu kama hujajenga hali ya kuaminiwa, ama kwa hakika hakuna atakayetekeleza matakwa yako.
Kwa upande mwingine kama mzazi, je watoto wako wanaamini unapowaambia, usifanye hiki mwanangu? Je, watoto wetu wanajutia unapowaeleza kuwa umewaeleza mara nyingi kuhusu kutofanya jambo fulani lakini wanakaidi?
Ijulikane kuwa, kazi ya kuwaaminisha wengine si rahisi kama huna ujuzi au mbinu stahiki.Kuwaaminisha wengine si jambo la mazoea au mzaha mzaha. Lakini kwa bahati nzuri leo napenda kutoa zawadi hii kwako msomaji kuwa kuna njia TANO (5) rahisi sana unazoweza kuzifuata kama nilivyozinukuu kutoka katika kitabu cha “Secrets of Power Persuasion” cha Roger Dawson ili kuijenga na kuinua hali yako ya kuaminika kwa wengine na kujiongezea heshima, uthamani na utendaji katika maisha yako ya kila siku. Zifuatazo ni njia TANO (5) katika dondoo, zitakusaidia sana kama utazitumia;
DONDOO 1:
“Never assume they believe you”.
USIBASHIRI KUWA UNAAMINIWA
Watu wenye nguvu ya kuwahamasisha na kuwaaminisha wengine kwa mawazo yao wana mambo matatu (3) kuhusu kutobashiri;
1)   Kutobashiri hali ya umasikini wao: kutobashiri kuwa hawawezi kulipia gharama ya bidhaa inayouzwa
2)   Kutobashiri kuwa umeeleweka
3)   Kutobashiri kuwa umeaminika. Hili jambo la mwisho ni la msingi sana. “Kutobashiri kuwa umeaminika”.
Hakikisha unagusia masuala yote ya msingi kwa kuzingatia kuwa watu unaotaka wakuamini nao wanakusikiliza kwa makini na kutafakari kwa kina kuhusu unayowaeleza na kukuamini.Tumia kila mbinu kuhakikisha unaeleweka ili wengine wakuamini. Ni lazima uonyeshe uwezo wa kutekeleza kile unachotaka wengine waamini na kutekeleza.
Dondoo hii inasisitiza; narudia tena na tena-Usibashiri kuwa umeeleweka au kuaminiwa na wengine.
DONDOO 2:
“Only tell them as much as they’ll believe”.
WAELEZE KADIRI UWEZAVYO HADI WAKUAMINI
Dondoo hii inamaanisha kuwa usiwaeleze watu zaidi ya vile unavyofikiri ili wakuamini.Kiuhalisia kabisa unaweza kuwa na bidhaa au huduma inayozidi mategemeo au matarajio ya wateja, lakini kama utashindwa kuwafanya wakuamini, hutakuwa na wakumlaumu.
DONDOO 3:
“Tell the truth, even if it hurts”.
WAELEZE UKWELI MTUPU HATA KAMA UNAUMA
Ni kweli kabisa kueleza au kuelezwa ukweli inauma.Kama ulikuwa hufahamu maana halisi ya kueleza ukweli ni vyema ukaanza sasa utawafanya wengi wakuamini.Haijalishi ni ukweli mchungu kiasi gani, usisite! eleza kila kitu wazi wazi.Hakika narudia tena, utaaminiwa kibiashara, kiutendaji na kimaisha kwa ujumla.
DONDOO 4:
 “Point out the disadvantages”
ONYESHA MAPUNGUFU YA WENGINE KIUTENDAJI
Ukiwa ni mtu wa kutoa au kuonyesha mapungufu ya bidhaa au huduma za wengine au utendaji wa mtu fulani ni dhahiri kuwa lolote utakalosema baada ya hapo litaaminika au kuaminiwa na wengine.Tafiti zimeonyesha kuwa kuna faida NNE (4) nzito kwa kukosoa au kutoa mapungufu ya upande mwingine kimtazamo;
1)                  Huufanya upande unaokosolewa kuamini kuwa huna unafiki,ubaguzi wala upendeleo.Pia ni mtu wa haki uliye na upeo mpana katika kushauri wengine kutenda na kuenenda katika unyoofu.
2)                  Humfanya msikilizaji ajione kuwa unamthamini na kuamini uwezo wake kiakili hivyo kuweza kuyaona mapungufu yake na pia kujiona ni mkosaji kupitia ukosoaji wako.
3)                  Hukuhamasisha na kukulazimisha kutarajia mambo halisi yasiyo na mapungufu hivyo kujitahidi kufanya mahojiano yenye kujenga
4)                 Inakuongezea sifa ya kukubalika na kuaminika katika kila utalosema.
DONDOO 5:
“Use Precise Numbers”
ONGEA UKITUMIA TAKWIMU KWA NAMBA HALISI
Watu huamini zaidi  takwimu kwa namba halisi na si makisio au makadirio kwa namba.Takwimu unazotoa kwa namba halisi zitakuongezea hali ya kuaminika zaidi kwa wale wanaokusikiliza.Hii huonyesha ni jinsi gani unavyoeleza mambo kwa uhakika na ufasaha. Hivyo basi, ukitaka kujijengea hali ya kuaminika, tumia namba halisi.Mfano, unaweza kusema kuwa kampuni yako inaweza kuongeza mapato yake kwa asilimia 75 kuliko kusema kampuni inatarajia kuongeza mapato yake  kwa takribani mara mbili ya yale ya mwaka jana.
Nakutakia utekelezaji mwema katika kujijengea uwezo wa kuaminika na kila mtu.
Makala hii imeandaliwa kwa kutumia ubunifu na uelewa binafsi wa kisaikolojia wa mwandishi Henry Kazula kwa kushirikiana na uzoefu kutoka katika kitabu cha “Secrets of Power Persuasion” cha Roger Dawson.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.









Hakuna maoni:

Chapisha Maoni