inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 28 Julai 2013

FAMILIA NA MTAZAMO: NANI ANA JUKUMU LA KULIPA BILI MBALI MBALI?...TAZAMA PICHA!


Picha na
Picha:THINKSTOCK
Picha na merryfarmer.net
Picha na tvone.tv 
Ni ukweli usiojificha kuwa wanaume wamekuwa mstari wa mbele kuchukua majukumu mbali mbali ya familia yahusuyo kutoa pesa.Ingawaje katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kiuchumi na teknolojia tunaona pia wanawake wakichukua nafasi kubwa ya kubeba majumu ya familia yahusuyo kutoa pesa.

Najua kila mtu atakuwa na mtazamo tofauti kuhusiana na swali letu la leo.

Nikitumia uzoefu wangu wa kutazama kwa ukaribu masuala ya familia…chukua mfano umeenda sehemu ya starehe(hotelini), chunguza kwa makini, nani analipa bili ya mapochopocho yaliyoliwa na vinywaji? Ni mwanamke au mwanaume? Jibu unalo! 

Kautaratibu haka huendelea kujijenga kuanzia kipindi cha uchumba hadi wakati wa ndoa.

Tatizo linakuja pale wanandoa wanapokuwa wote wana kipato…utaona utata, mume huanza kumbadilisha mwanamke ghafla kwa kumwambia aanze kutoa pesa kwa matumizi mbali mbali ya nyumbani.Jibu la mke huwa ”wewe ndiyo baba na kichwa cha familia…hivyo una wajibu wa kubeba majukumu yote.” Ndiyo hivyo, hakuzoea kulipia bili tangu kipindi cha uchumba…anajua kuwa mwanaume ana jukumu la kulipia gharama zote za familia. 
Hapa ndipo ugomvi unapoanzia kuhusiana na mapato na matumizi ya pesa kwa kila mmoja.
 Utaratibu huo unaweza kubadilika, hasa ikizingatiwa kuwa mahusiano na ndoa ni makubaliano wa mwanaume na mwanamke yakilenga kusaidiana na kujenga familia iliyo imara. 






  


 

Tunaanzia wapi sasa kubadilisha mfumo? 
 1. Mwanaume una jukumu la kumzoesha mwanamke wako kuanza kulipa au kuchangia bili   au  gharama nyingine za matumizi (haijalishi kama wewe mwanume unampa pesa) …inapaswa aonekane analipa au kuchangia...

 2.  Mwanamke, huna sababu ya kukubali kulipiwa mara kwa mara…onyesha kuwa nawe
     una uwezo wa kulipa au kuchangia, hivyo huwezi kutetereshwa na hutanyanyasika wala kufanywa mtumwa wa mwanaume. 

3. Lifanye zoezi lenu kuwa endelevu na mtaona mtunda yake.Hapa ndipo lile lengo tarajiwa la kusaidiana kwenye ndoa linapojidhihirisha.Pia kuepusha ugomvi unaohusiana na matumizi ya pesa kwa kila mmoja.

Picha na myhappyfinds.com
Anzia hapo kubadilisha mtazamo ili kuepusha migogoro ndani ya familia!
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!