inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 14 Aprili 2015

MTAZAMO: JIJENGEE FALSAFA BINAFSI YA MAISHA YAKO-“Building Your Philosophy of Life” .



Picha imetolewa Jukwaa huru

Neno “falsafa” kama lilivyoainishwa na tovuti ya Mwanahalisi Forum, ni imani aliyonayo mtu juu ya jambo au kitu fulani.Katika maana halisi ya neno "falsafa" kwa Kigiriki-"philosophy" lenye muunganiko wa maneno mawili; philo=love na sophia=wisdom (love of wisdom) lina mantiki kubwa katika kuhamasisha, kuchokoza fikra, hisia na ufahamu; kubwa zaidi ni kupenda kutenda mema. 
Mtandao wa Mwanahalisi Forum unafafanua zaidi kuwa; kila mwanadamu aliye timamu katika maisha anaongozwa na vitu vitatu ambavyo ni FALSAFA, MTAZAMO na MSIMAMO, vitu hivi huwa ndiyo dira ya mwanadamu katika maisha yake. Mambo hayo matatu ndiyo hufanya wakati mwingine watu kutofautiana au kuwa kitu kimoja.
Jicho letu linapenda kuangazia zaidi kuhusu kuijenga “falsafa binafsi ya maisha”-“philosophy of life” iliyo kanuni au utaratibu anaojiwekea mtu binafsi; bila kushurutishwa na mtu mwingine ikiwa ni dira ya maisha yenye kutoa maamuzi ya busara, yasiyo na kikwazo kwa maisha ya mtu au watu wengine.  
Tukiangazia fikra zetu zaidi katika falsafa ya maisha iliyo dira ya maisha ya mtu binafsi ni vyema kujua umuhimu wa kuunda falsafa binafsi ya maisha na kujua jinsi ya kuijenga falsafa hiyo ndani ya maisha yetu kwa lengo la kutawala maisha yetu.
Umuhimu Wa Kuunda Falsafa Binafsi Ya Maisha
Kama ilivyoainishwa awali, falsafa binafsi ya maisha yetu ni dira inayoongoza na kutawala upeo wa maisha yetu; hutupatia faida mbali mbali kwa kuzingatia uwezo wetu wa ndani katika kutoa maamuzi yaliyo sahihi na yasiyo kinzana na maadili ndani ya jamii husika.
Ndugu msomaji, natumaini unafuatana nami ili kuepusha mkanganyiko wa kimtazamo na kifikra…hivyo basi, nikujuze umuhimu wa kuwa au kuunda falsafa binafsi ya maisha kama hukuwa nayo, na kama ulikuwa nayo kujifunza zaidi kuiimarisha kwa mafanikio maishani.
1.FALSAFA BINAFSI HUTUEPUSHA NA HATARI MBALI MBALI KATIKA KUTOA MAAMUZI SAHIHI…
2.HUTOA MWONGOZO WA MAISHA YETU...falsafa ya maisha ni dira ya maisha yetu!
3.HUTUEPUSHA KUWA WATUMWA WA MAWAZO YA WENGINE…ikiwa tumekosa falsafa thabiti ya maisha yetu, ni rahisi kwa watu wengine kutambua mapungufu yetu hivyo kutuingia kifikra na kutawala mawazo na mtazamo wetu pasipo kujua.
4.HUTUJENGEA MSIMAMO THABITI KATIKA MAAMUZI YETU…Huepusha kuyumbishwa na msimamo wa watu wengine kuhusu sisi.Msimamo wetu ulio thabiti hudhihirisha ukweli wa vile tulivyo; hututambulisha kwa wengine vile tulivyo.
5.HUTUEPUSHA KUWA BENDERA FUATA UPEPO…hivyo kuongeza heshima na kuonyesha busara zetu kwa wengine katika kutoa maamuzi sahihi.
6.HUSABABISHA KUWEPO KWA MAHUSIANO MEMA NA WATU WENGINE…falsafa yetu iliyo na tija maishani huwavuta wengine kwetu na kujenga mahusiano mema.
Fahamu kwa undani jinsi ya kuijenga falsafa binafsi kwa kubofya HAPA
Tunakutakia kila la heri katika zoezi hili muhimu la kujijengea falsafa yako.
Imetayarishwa na,
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni