inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 1 Novemba 2013

ELIMU NA SAIKOLOJIA: MBADALA WA ADHABU YA VIBOKO KWA WANAFUNZI


M
akala hii  ni muendelezo wa makala ya Jumapili, 27 Octoba 2013 katika eneo la elimu kuhusu mtazamo wa Kisaikolojia kuhusu adhabu ya viboko mashuleni:


Picha www.brisbanetimes.com.au
Zifuatazo ni mbinu mbadala wa adhabu ya viboko zinazofuata taratibu za Wanasaikolojia, zinazoweza kutumiwa na mwalimu au mzazi bila kuleta madhara kwa mwanafunzi/mtoto wakati huo huo zikichochea tabia njema na ufaulu;


1.CHUNGUZA CHANZO CHA TABIA MBAYA YA MTOTO
Hupaswi kumwadhibu mtoto/mwanafunzi kwa viboko au adhabu nyingine ya kuutesa mwili wake kama amekiuka kanuni, au kuonyesha tabia mbaya.
Fuatilia kwa makini ukitafuta chanzo cha mabadiliko ya tabia yake,mpatie ushauri nasaha ukimfanya ajichunguze tabia yake, wakati huo huo ukimuelekeza madhara ya tabia yake mbaya.
Kubaliana naye kubadilika kwa kupanga naye mikakati iliyo na faida kwa mtoto/mwanafunzi(mfano-mkakati utakao chochea kujisomea na kuepuka tabia mbaya.

2. KEMEA TABIA MBAYA
Onyo litolewalo kwa mdomo ni adhabu yenye kugusa hisia ya ndani kwa mtoto/mwanafunzi kuliko adhabu ya viboko.Kemea kuonyesha kutoridhishwa na tabia mbaya au ufunjivu wa kanuni na maadili.
Zingatia: Mbinu hii ni nzuri na ina matokeo mazuri kama tu haitatumika mara kwa mara.Mtoto/mwanafunzi huweza kuchukulia kama mazoea na kutoa tafsiri kuwa mwalimu/mzazi ana hasira/mkali wakati wote ikitumika mara kwa mara.

3. TAFAKARI KWA PAMOJA NA MTOTO/MWANAFUNZI KUHUSU TABIA MBAYA
Tenga muda wa kukaa na mtoto/mwanafunzi kujadili madhara ya tabia mbaya au kukiuka kanuni mlizokubaliana.

4. TUMIA ZAWADI KUCHOCHEA TABIA NJEMA
Pongezi kwa mtoto/mwanafunzi huchochea kuendelea kwa tabia njema.Inaweza kuwa ya kitu cha kushikika au maneno ya pongezi.
Pia, mpongeze mtoto/mwanafunzi anapoonyesha kuwa na tabia njema.
 
Angalizo:Unapaswa kuwa makini sana katika kutoa zawadi kwa mtoto/mwanafunzi.Anaweza kuigiza tabia njema ili akufurahishe ilihali amaanishi kutoka moyoni. Ni vizuri kutompa mtoto/mwanafunzi zawadi mara kwa mara kila anapokufurahisha/anapoonyesha tabia njema.Kufanya hivyo hupoteza maana halisi ya zawadi, mwisho mtoto/mwanafunzi huchukulia zawadi kama mazoea au kitu cha lazima akiwa ameonyesha tabia njema.
 Imetayarishwa na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni