inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 10 Mei 2015

MTAZAMO: HIVI NDIVYO WANAVYOFANYA WENGINE KUKUAMINISHA WANACHOAMINI KWA MASLAHI ZAO BINAFSI…Kuwa Makini Kutambua Viashiria Vifuatavyo.

Makala inayofanana: NJIA TANO (5) ZA KUWAFANYA WATU WENGINE WAKUAMINI  KWA NIA NJEMA KABISA.


Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa Jielimishe Kwanza Blog, unapaswa kujua kuwa kuna watu au makundi ya watu hapa duniani hutumia njia za ujanja ujanja na pia kuchanganya na saikolojia ya maisha ya binadamu ili kujinufaisha.Hutumia ujanja huo kuwaaminisha wengine wanachoamini na mwisho wa siku hutumia migongo na ufikiri hafifu wa wengine kujineemesha.
Bila kificho nakuletea viashiria VITANO (5) ili kukuweka wazi ndugu msomaji na ujue kuwa katika viashiria hivyo vinavyoainishwa unataka kutumika au unatumika kwa maslahi ya wengine.

1.SIKU ZOTE HUONYESHA KUWA NA MAMLAKA
Katika kila mahojiano na majadiliano yenu huonyesha kuwa ni wenyewe pekee wanaoweza kutatua tatizo husika kwa wakati husika. Hivyo kukufanya uwe mtu wa kusindikiza mawazo na matakwa yao.
2.WANAAMINI SANA MAWAZO YAO NA KUBEZA YA WENGINE…
Kiashiria hiki hakina tofauti sana na namba 1, tofauti ni kuwa wao hupenda kupuuza na kubeza mawazo ya wengine wazi wazi kwa makusudi na baadaye huyatumia yale ya msingi kwao kwa manufaa binafsi.
Ni watu walio mafundi wa kukatisha tamaa kwa kutumia maneno yenye uzito katika hali iliyo halisi.Hutumia takwimu kwa namba halisi na nukuu mbali mbali kubeza mawazo ya wengine.
3.WANAJIAMINI SANA KWA YALE WANAYOYASEMA BILA KUBADILIKA BADILIKA
Kujiamini ni silaha yao kubwa.Wanaelewa maana halisi ya kujiamini kwa kile wanachoeleza na ni rahisi kwao kukuaminisha wanachoamini kwa matakwa binafsi.
4.HUJENGA HOJA NZITO KUPITIA HOJA YAKO
Huunganisha kiashiria hiki na kiashiria namba 2; kubeza mawazo yako lakini kwa upande mwingine hutumia hoja yako kutoa hoja nzito iliyo na maslahi kwao.
5.HUONYESHA MAPUNGUFU YA KATIKA HOJA ZAKO
Ni mahili sana wa kuchunguza na kuelezea mapungufu ya wengine katika lugha ambayo utaridhika.Mwisho wa siku hutumia mapungufu yako na kuyaboresha kwa manufaa yao binafsi bila hata kukushirikisha.
_________
Ndugu msomaji wa makala hii usifikiri watu hao ni “magenius” au wana uwezo wa kipekee kwa kupendelewa na Mungu; La hasha! Ni wepesi tu wa kujifunza, kujielimisha kwanza na kusoma vitabu mbali mbali vilivyosheheni maafunzo na uzoefu wa maisha ya watu waliofanikiwa kwa kupitia saikolojia ya maisha ya binadamu.
Kazi kwako, je unataka kuendelea kutumika na hao wajanja kwa maslahi zao binafsi au unachukua hatua ya ujasiri kubadilika na kuhama hapo ulipo kifikra na kimtazamo? Jibu unalo!
Makala hii imeandaliwa kwa kutumia ubunifu na uelewa binafsi wa kisaikolojia wa mwandishi Henry Kazula  kwa kushirikiana na vitabu mbali mbali vya kisaikolojia.

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza

Maoni 2 :

  1. Ni kweli Henry!

    JibuFuta
  2. Hapo naona umehamasisha kusoma vitabu na kujifunza

    JibuFuta