inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 5 Julai 2013

MTAZAMO: JIFUNZE KUWEKA MALENGO YENYE MAFANIKIO!



Picha na blog.readytomanage.com
Maisha yenye mafanikio ni yale yanayotawaliwa na malengo halisia yanayoambatana na utekelezaji katika wakati husika.
Nikimnukuu mwandishi wa vitabu maarufu Norman Vincent Peale anasema;

A goal is a dream with a deadline” kwa lugha ya Kiswahili “lengo ni ndoto yenye kikomo cha wakati.”

Kwa mtazamo mwingine mwandishi na msemaji wa hadhara maarufu nchini Marekani Joel Osteen anasisitiza kuwa ndoto ni lazima iwe na mpango mkakati; “ A dream without a plan ends up as a wish”- “Ndoto bila utendaji unaofuata mpango mkakati ni sawa na matamanio tu.”

Ikiwa una malengo pekee bila mpango mkakati haisaidii, cha msingi ni kuwa na malengo yaliyo kimaandishi na mpango mkakati kuyafikia malengo yako.

Watu wengi huwa na ndoto nzuri zilizo katika hali ya shauku na matamanio pekee.Hii ni kwa sababu hawana/wamekosa mpango mkakati wa kufanikisha ndoto zao.
Hili ni tatizo kubwa linalowafanya watu kuwa katika hali ile ile ya maisha kwa miaka mingi.
Jielimishe Kwanza! imewahi kuwauliza watu wa makundi tofauti kama wana malengo...iligundulika kuwa watu wengi hushindwa kuyapangilia malengo yao kwa kuzingatia kiwango cha muda wa utekelezaji.
Mfano, mtu mmoja alisema anataka kumiliki chuo binafsi...alipoulizwa amechukua hatua zipi kuanza kutekeleza lengo lake...alishindwa kueleza. 


AINA ZA MALENGO

Mwandishi na mhubiri maarufu nchini Marekani Joel Osteen ameainisha aina mbili za malengo; 1) Malengo ya muda mrefu 2) Malengo ya muda mfupi

1)Malengo ya muda mrefu

Malengo haya huchukua miaka 10-20 kukamilika.Kama nilivyosema awali ni vyema kuandika malengo yako na kujiwekea mpango mkakati.

2)Malengo ya muda mfupi

Malengo haya ni yale unayoyafanyia kazi kwa sasa.Faida ya malengo haya ni kukufanya usheherekee ukiwa kwenye safari ya kuyafikia malengo makubwa/ya muda mrefu.Pia hukupatia ari ya kusonga mbele kuyafikia malengo ya muda mrefu.


Kiundani tuangalie mbinu 10 zinazoweza kukuondoa hapo ulipo ili ndoto zako zilizo katika malengo zitimie na kuzaa matunda.

1.ANDIKA MALENGO YAKO KWENYE KITABU MAALUMU

Usipuuze hata kidogo kuandika malengo yako na kuwa na mpango mkakati wa kuyafikia.

2.USIWEKE MALENGO MAKUBWA YASIYO HALISI

Jitahidi kuweka malengo yaliyo kwenye uwezo wako.Unaweza ukawa na picha kubwa ya maono lakini unaweza kuanza kidogo kidogo.Mfano mtu hawezi kusema ana lengo la kumiliki gari la kifahari wakati hata kula yenyewe ni ya shida.

3.HUSISHA MALENGO MAPYA NA ULIYONAYO KWA SASA
Kuna faida kubwa ya kuhusisha malengo ya sasa na yajayo, hapa unaweza kujipima uwezo wako kiutendaji katika kuyafikia malengo mapya.

4.JIKITE KWENYE MALENGO YENYE FAIDA ZA HARAKA

Ni vizuri kujiwekea vipaumbele katika malengo unayojiwekea ukizingatia faida za haraka ili upate ari ya kuyafikia malengo makubwa.Jiulize: Malengo ninayojiwekea yana faida za haraka kwa sasa?

5.ONGELEA MALENGO YAKO KATIKA HALI CHANYA

Hii itakupa ari ya kuyafanyia kazi malengo yako.Utajiona ni mtu wa kufanikiwa kila siku katika malengo yako (ya muda mfupi hata yale ya muda mrefu).

6.JIWEKEE MPANGO MKAKATI KUFANIKISHA MALENGO

Jiulize:Je ninazo taarifa? Nahitaji taarifa zipi? Je kuna mbinu na ujuzi ninaotakiwa kujifunza?

7.YAGAWE MALENGO YAKO KATIKA HALI YA UTEKELEZAJI

Inafika wakati mtu anakuwa na malengo makubwa kupita uwezo wake wa kutekeleza.Ni vyema kabisa kuyagawa katika hatua ndogo ndogo ili mwisho wa siku ulifikie lengo kubwa ulilojiwekea.

8.TAMBUA KUWA KUYAFIKIA MALENGO YAKO SI LAZIMA UPITIE SHIDA NA KUJITOA MHANGA

Kuna kasumba iliyozoeleka kwa watu wengi eti ili uyafikie malengo ni lazima upate shida sana.Hii si kweli, bali watu hupenda kuongelea vitu kwa ujumla sana wakati kuna malengo yanaweza kutimia kwa kujipanga vizuri na kujikita kikamilifu.  
Ndugu msomaji, ukifikiri kwa mtazamo kama ilivyo kasumba ya watu wengi utakata tamaa na hutajiwekea malengo hivyo kuishi maisha ya "...bora kumekucha..." "...ya leo ni afadhali ya jana..." 
9.EPUKA KUWAAMBIA WATU WENYE MTAZAMO HASI MALENGO YAKO

Watu wanaokuzunguka ni wengi, na kila mmoja ana mtazamo wake.Utaniuliza, nitawajuaje? Kuna msemaji wa hadhara na mhubiri na mwandishi wa vitabu Joyce Meyer aliwahi kusema; ukitaka kujua mtazamo wa mtu msikilize maneno yake…Hivyo basi ni vyema kuwa muangalifu wakati wa kuchagua aina ya marafiki unaweza kuwashirikisha malengo yako.

10.USIKUBALI KUYUMBISHWA NA MTU, NG'ANG'ANIA MALENGO YAKO
Mafanikio ya malengo yako yanaanzia na wewe kifikra, kimtazamo na kiutendaji.Ukifanya kosa la kumwachia mtu mwingine asimamie na kukuendeshea malengo yako hutapiga hatua stahiki. Itambulike kuwa, si watu wote wana nia njema na malengo yako.Wapo wengine wanaotaka usiyafikie malengo uliyowaambia.
Jifunze kutokana na makosa.Tumia makosa yaliyofanyika awali kuwa changamoto na ujifunze kufanya vizuri ili utimize malengo yako kwa mafanikio makubwa.
 

Je, una malengo yasiyo na ufumbuzi au huna malengo yoyote? Tumia mbinu tajwa katika makala hii kubadilika na kuwa mtu mwenye malengo yenye tija.



Imetolewa na

Jielimishe Kwanza!