inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 26 Juni 2013

MTAZAMO: JIFUNZE KUWA NA MTAZAMO CHANYA!



Picha na www.narconon.co

  Habari!

Naomba niwakaribishe tena katika ukumbi huu kuhusu “MTAZAMO”.Wiki iliyopita niliandika makala kuhusu MADHARA YA KUWA NA MTAZAMO HASI…












ISOME HAPA:  http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/06/epuka-kuwa-na-mtazamohasi-picha-na.html

Mwishoni niliahidi kukuletea mbinu za kumfanya mtu kuwa na mtazamo chanya. Karibu tena leo kuzifahamu mbinu hizo.


Awali ya yote ni vyema tukafahamu faida za kuwa na mtazamo chanya;

·   Ni njia nzuri kiafya ya kuepukana na hatari ya kupatawa na magonjwa ya moyo, pia huchochea kinga ya mwili

·      kujiongezea uwezo wa kutatua matatizo

·      ni rahisi kwa watu wenye mtazamo chanya kupambana na msongo wa mawazo

·    mtazamo chanya huvuta vitu chanya-hii ni sambamba na kufungua milango ya mafanikio katika maisha

·     Katika hali ya muonekano wa kwanza, mtazamo chanya utakufanya ukubalike na watu


Zifuatazo ni mbinu zinazoweza kumjengea mtu uwezo wa kuwa na mtazamo chanya na wenye tija;

1.TUMIA LUGHA ILIYO CHANYA- USISEME “SIWEZI KUPATA”…SEMA “NITAPATAJE?”…
Mjasiriamali maarufu na mwandishi wa vitabu aliyebobea nchini Marekani-Robert Kiyosaki anatoa mtazamo huo katika hali ya swali “NITAPATAJE?” akimaanisha kuwa swali hili litaubidisha ubongo kufikiri njia mbadala za kupata suluhisho la tatizo.
Anapingana na usemi wa kwanza ulio katika sentensi kamili “SIWEZI KUPATA” akimaanisha kuwa mtazamo huu hasi unamfanya mtu kuwa mvivu wa kufikiri.

Anasisitiza kwa kusema kujiuliza maswali ni njia moja wapo ya kuupa ubongo mazoezi na kuuongezea uwezo wa kufikiri, na mwisho wa yote ni kupata mafanikio tarajiwa.



2.EPUKA KUELEZA MALENGO YAKO KWA KILA MTU…UTAKATISHWA TAMAA!

Jifunze kuchagua mrafiki wa kuwaeleza malengo yako…kuwa makini sana! Wapo wengine kazi yao ni kukukatisha tamaa.Ukitaka kuwajua mtazamo wao, sikiliza maneno yao.
Angalizo: wapo watu watakaotaka kuboresha wazo/lengo lako kwa lugha ya kuonyesha ufanye marekebisho au maboresho, usiwabeze...chukulia hiyo kama changamoto kusonga mbele na kufanya vizuri zaidi.



 3.JIFUNZE NA UFANYIE KAZI ULIYOJIFUNZA UKIWA NA MTAZAMO CHANYA
Katika maisha ya kila siku tunajifunza kwa njia moja au nyingine…jukumu letu ni kuchagua kujifunza mema au mabaya.Nikizungumizia kuhusu kujifunza mema na yote yanayojenga ni vyema kuyafanyia kazi kwa vitendo tukitegemea majibu chanya.Kadri utavyokuwa ukipima mafanikio ya utendaji ndivyo unavyozidi kujiimarisha zaidi katika kuwa na mtazamo chanya.


4. JIWEKEE MALENGO KWA MAANDISHI

Ni kitu cha muhimu kuweka malengo-yanaweza kuwa ya muda mfupi au mrefu.Mara nyingi malengo ya muda mfupi hutupa ari ya kuyakaribia malengo ya muda mrefu, pia ni sehemu ya kutuepusha kukata tamaa tukiwa katika safari ya kuelekea kwenye malengo ya muda mrefu.Kipimo cha mafanikio ya malengo yako kitaweza kuboresha uwezo wako wa kuwa na mtazamo chanya.


5.JIHUSISHE NA WATU WENYE MATEGEMEO CHANYA

Kujihusisha na watu wenye mtazamo chanya kutakuongezea uwezo wako wa mategemeo chanya katika mambo unayofanya.Pia watakupa ari ya kusonga mbele kimawazo na kiutendaji.


6.FAHAMU FAIDA ZA KUWA NA MTAZAMO CHANYA

Ukifahamu faida za kuwa na mtazamo chanya utajibidisha kufikia lengo la kuwa na mategemeo chanya.


7.JIWEKEE MPANGO WA KUEPUKA KUWA NA MTAZAMO HASI

Panga utaratibu ulio kwa vitendo kuepukana na mtazamo hasi.Kwa kufanya hivyo, mtazamo chanya utazidi kujijenga siku hadi siku.


8.TAMBUA NA UPAMBANE NA MAWAZO HASI

Kuna msemo unasema, kulijua tatizo ni njia mojawapo ya kuoambana na tatizo au kumfahamu adui ni njia nzuri ya kuanza kupambana naye.Jaribu kujichunguza utagundua ni kwa kiasi gani au mara ngapi umekuwa na mtazamo hasi hata kwa vitu vilivyo kwenye uwezo wako?


9.JARIBU KUFANYA VITU VIPYA

Unapokuwa na uthubutu wa kutenda vitu vipya ni njia ya kujiongezea ujasiri na kuimarisha mtazamo chanya wa kufikiri.Usiogope kufanya makosa, hayo yanakuwa ni ishara ya kukuboreshea utendaji wako kwa kujifunza.


10.JISOMEE VITABU NA MAJARIDA

Kupitia vitabu na majarida utajifunza mambo mengi kuhusu kujiimarisha katika mtazamo wa kufikiri hasa ukilinganisha na wako.Ukitendea kazi mbinu mbali mbali zilizotolewa zitakuongezea uwezo wa kuwa na mtazamo chanya siku hadi siku.


11.SIKILIZA HOTUBA NA MAFUNDISHO YENYE KUIMARISHA

Kusikiza hotuba na mafundisho yenye kuimarisha ukiwa kwenye gari au nyumbani ni njia nzuri kujiongezea uwezo wa kuwa na mtazamo chanya.Kupitia hao utajifunza mbinu walizopitia kufikia malengo yao.
Tuma maoni kupitia:jielimishekwanza@gmail.com
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni