inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 17 Machi 2016

BIASHARA: BADO UNASITASITA KUMILIKI KAMPUNI BINAFSI KISHERIA? FANYA YAFUATAYO…

 

Katika kipindi hiki cha utandawazi na uwepo wa soko huria nchini Tanzania  kumeibuka wimbi kubwa la watu kupenda kuanzisha na kumiliki biashara binafsi au katika vikundi ili kupambana na tatizo la ajira nchini.
Kwa bahati mbaya, wafanyabishara walio wengi wamekuwa wakiangukia katika biashara ndogo ndogo na zisizo katika mfumo rasmi, pia hazitambuliki kisheria kwa hofu ya kuhitaki mitaji mikubwa ndipo wasajiliwe; hivyo, kukosa wigo mpana wa kukuza biashara zao na kukosa fursa kem kem za kupata zabuni za Serikalini au kushirikiana na wafanyabiashara wakubwa walio katika mfumo rasmi unaotambulika kisheria.Pia kushindwa kupata urafiki wa karibu na Sekta zinazohusika na kusaidia wajasiriamali wadogo kupata fedha kukuza biashara zao.Hizo ni baadhi ya hasara za kushindwa kusajili Kampuni au Jina la Biashara yako na kutambulika kisheria.
Baada ya kuiona changamoto iliyopo kwa wafanyabishara/ wajasiriamali wadogo wenye nia ya kukuza wigo wa biashara hata Kimataifa, Kampuni ya Jielimishe Kwanza imefanya utafiti wa kina, pia kupitia Mamlaka inayohusika nchini Tanzania na kukuainishia njia rahisi za kufuata ili utoke hapo ulipo na kuifanya kampuni yako itambulike kisheria na kukua, pia kuongeza wigo wa biashara yako.Tambua kuwa kampuni zisizo na malengo ya kukua kwa kuongeza ubunifu zipo kwenye hatari kubwa ya kupotea katika ramani ya biashara ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa biashara.
Je, bado unasitasita kuwa na kampuni binafsi kisheria? Hujachelewa, haijalishi una mtaji mdogo, ikiwa inaitwa biashara yenye kuleta kipato halali ni vizuri kuisajili kisheria. Hivi sasa mfumo wa usajili umerahisishwa sana; sasa unaweza kusajili jina la Biashara na Kampuni yako kwa njia ya mtandao wa Internet (Business Name Online Registration), weka mpango mkakati kuanza kujisajili na kufuata yafuatayo;
  1. Utalazimika kuingia kwenye internet katika mtandao wa http://www.brela.go.tz/
  2. Jisajili* (SIGN UP) katika mfumo huo wa mtandao (ikiwa unasajili kwa mara ya kwanza); INDIVIDUAL ikiwa ni akaunti binafsi na CORPORATE kwa kampuni iliyokwisha sajiliwa.* Ili uweze kusajili unapaswa kuwa na vitu vifuatavyo i) Email ii) Nambari ya simu iii) Nambari ya kitambulisho cha Taifa, Leseni ya biashara au hati ya kusafiria.Ukimaliza kuingiza taarifa zako, mfumo wa usajili utatuma Nenosiri (Password) kwenye email yako.Hivyo, utatumia Email yako na Nenosiri kuingia kwenye mfumo rasmi ya usajili.
Hakikisha una majina matatu (3) pendekezwa ya Kampuni yako. Ukiwa umefuata hatua zote; ( hatua ya 1 na 2), bonyeza BUSINESS NAME CLEARENCE (kwa usajili wa jina la Biashara, ambao unaishia online) na COMPANY NAME CLEARENCE (kwa usajili wa jina la Kampuni), kisha APPLY NEW COMPANY NAME ingiza jina la Kampuni unalotaka kusearch kisha SUBMIT, hapo utakuwa umeomba jina baada ya Mamlaka husika kufanya search.Ikiwa jina limekataliwa (REJECTED) utatakiwa kufuata maoni elekezi au kuomba jina lingine kwa kubonyeza APPLY NEW COMPANY NAME, na kama jina likiwa limekubaliwa APPROVED READ TO REGISTER hapo utatakiwa kulipia jina hilo kwa mfumo rasmi ambao mfumo utaelekeza na hivyo kuandaa MEMORANDUM and ARTICLES OF ASSOCIATION na kujaza FORM NO 14A na 14B kisha ziwasilishwe kwenye ofisi ya Mamlaka husika ya usajili kwa kufanyiwa tathmini ili ulipie ada ya usajili kulingana na thamani ya Kampuni yako. Fahamu zaidi kuhusu Ada ya usajili wa Kampuni na usajili wa Jina la Biashara.
Mwisho baada ya kufanikiwa kusajili, utapatiwa cheti cha usajili.Baada ya hapo utahitajika kughulikia kupata namba ya mlipa kodi (TIN) ambayo hutolewa BURE kupitia TRA na leseni ya biashara kutoka Manispaa ambayo biashara yako ipo.
Ikiwa unahitaji usaidizi zaidi au upo nje ya Dar es salaam unaweza kuwasiliana nasi;
Simu: +255 754 572 143 / +255 716 075 826 
E-mail: jielimishekwanza@gmail.com
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni