inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 20 Mei 2013

MALEZI: Zijue mbinu (12) za kumsaidia mtoto wako kuepukana na matumizi mabaya ya Televisheni na intaneti:

www.syracuse.com
Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wazazi na walezi wengi kuwa watoto wao hawabanduki kwenye televisheni na wengine kupenda kushinda kwenye intaneti wakiangalia picha chafu zinazowafanya wakue haraka kabla ya umri wao wa mabadiliko ya kibaiolojia.

Watoto wengi wanaamini na kuheshimu maagizo yatolewayo kutoka katika vipindi mbali mbali, hivyo kupingana vikali na maagizo/matakwa ya wazazi/walezi. 

Hapa utagundua kuwa muongozo wa tabia za watoto wetu unategemea na kuathiriwa sana na kupishana kwa itikadi mbili tofauti; yaani zile za kwenye vipindi visivyo na tija kwenye televisheni na zile za wazazi/walezi.

Tatizo hili limewapelekea watoto wengi kukosa maadili na kushuka kwa taaluma zao na kushindwa kuwa na muda wa kujipangia malengo yao ya baadaye, hivyo kutengeneza kizazi kisichojitambua, kisichokuwa na malengo wala muelekeo.Yaani ni kizazi cha bendera fuata upepo. 
www.mirror.co.uk
Pia kuna matatizo mbali mbali ya kiafya kwa mtoto yatokanayo na kukaa muda mrefu kwenye televisheni au intaneti, nayo ni;

  • Kuongezeka uzito isivyo kawaida
  • Maumivu ya macho kutokana na mionzi
  • Kuumwa kichwa
  • Ubongo kushindwa kuimarika hasa kwa watoto walio chini ya miaka 2
  • Kuwa kwenye hatari ya kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulevya...
Kutokana na utafiti nilioufanya kwa kushirikiana na tafiti nyingine, nimegundua mbinu zifuatazo ambazo wewe kama mzazi/mlezi ukizisimamia kikamilifu zitamsaidia mtoto wako, nawe kuishi maisha ya furaha pamoja na familia yako:

1.Mfanye mtoto wako kuwa msomaji wa vitabu, wewe ukiwa mfano

Mzazi/mlezi unatakiwa kusoma vitabu mbali mbali na pia kumsomea mtoto kitabu na kutoa simulizi mbalimbali kutoka kwenye vitabu.Mpatie majukumu ya kufanya kutoka katika vitabu alivyosoma; hasa kuandika taarifa fupi ihusuyo kitabu husika.

2.Mfanye mtoto aweze kuchagua vipindi vya kuangalia,wewe ukiwa mfano 

Inatakiwa ieleweke kuwa, si kila kinachoonekana kwenye Televisheni kinafaa kuangaliwa na kila mtu.Makampuni mengi huandaa vipindi kwa lengo la kufanya biashara na kwa kiasi kidogo kuelimisha umma.Mzazi/Mlezi unatakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika suala hili na si kuwa mtu wa kuruhusu uozo wa aina yoyote ile.Anza kumkuza mtoto kwa maadili mema na atakulia katika njia hiyo.

3.Panga utaratibu unaoeleweka kwa kila mwanafamilia

Kuishi maisha yasiyo na mpangilio ni hatari kubwa. Ni vizuri kuwa na utaratibu mzuri wa kula, kusoma, na kulala.Ni dhahiri kuwa wazazi/walezi mna majukumu mengi, lakini yasiwafanye kuepuka na kuwa kisingizio cha kutotimiza wajibu wenu.

4.Toa zawadi kwa mtoto akipunguza muda wa kuangalia televisheni

Inaweza kuwa ni zawadi inayohusisha matembezi ya kawaida au kutembelea matamasha, pia unaweza kumpatia mtoto zawadi ya nguo, vitabu au CDs zenye mafunzo. Hii itamfanya mtoto kupata msukumo zaidi wa kupunguza muda wa kukaa kwenye televisheni.

5.Fanya utaratibu wa matembezi kwenye vivutio mbalimbali

6.Usiweke televisheni kwenye chumba cha watoto

7. Mjengee mtoto kuwa kujifunza kunawezekana kwa kuona hali halisi na si lazima televisheni 

Mzazi/Mlezi unaweza kutumia vitu asilia katika mazingira yanayotuzunguka kumssaidia mtoto kujifunza na si kutegemea afundishwe na Televisheni na intaneti.

8.Mweleze mtoto hasara za kutumia muda mwingi kwenye televisheni na intaneti

9.Mhusishe mtoto kwenye klabu za michezo na vikundi vya sanaa ili kukuza kipaji chake

10.Weka namba ya siri kwenye televisheni na kuiwasha pale inapohitajika

11.Hakikisha unakuwa na muda wa kujumuika na familia yako

12. Mpe mtoto majukumu ambayo atatakiwa kuwasilisha kwa wakati

Imeandaliwa na: Henry Kazula

Jielimishe Kwanza! 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni