inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 21 Juni 2013

MTAZAMO: EPUKA KUWA NA MTAZAMO HASI…


Picha na hot100tips.com
Mara kwa mara watu wamekuwa na manung’uniko yaliyo sanjali na hali ngumu ya maisha.Hii imewafanya wengi kukosa muelekeo na mwishowe kukata tamaa, hasa waonapo wengine wakitesa na maisha.
Watu wamesongwa na kulaumu huku wakitumia muda mwingi kusononeka bila kuchukua hatua ya kufikiri tofauti.Ijulikane kuwa jinsi utumiavyo muda mrefu kusononeka na kunung’unika ndivyo unavyojiweka kwenye nafasi kubwa ya kupoteza fursa nyeti za kukutoa kimaisha.
Yafuatayo ni baadhi tu ya madhara ya kuwa na mtazamo hasi wa maisha;
  •       Utajiona huwezi kila kitu
  •      Utakuwa msindikizaji wa maamuzi ya watu, hutaamini maamuzi yako
  •     Utatofautiana na watu wenye mafanikio kifedha mfano; utachulia watu wote wenye fedha ni wezi ,mafisadi, na washirikina.  
Mwandishi maarufu, mfanyabiashara mkubwa nchini Marekani – Robert Kiyosaki
aliwahi kusema;  
“what you think it’s real, becomes your reality”  kwa lugha ya Kiswahili-  “unachofikiri ni halisi kinakuwa uhalisia wako”akitoa mfano kuwa mtu akisema siwezi kuwa tajiri, mtazamo huu huwa halisi kwake kwa sababu hatakuwa na juhudi zozote za kumpeleka hatua ya kuwa tajiri.
  •        Utapoteza fursa nyingi za kukutoa kimaisha
  •      Kukosa ujasiri na uthubutu wenye tija mfano mtu anaweza kusema “nikijaribu kufanya biashara hii nitapata hasara…anaweka uhakika wa kupata hasara kabla ya kuanza biashara yenyewe, hivyo kutothubutu.
Wakati mwingine nitajitahidi kukuletea mbinu za kuwa na matazamo chanya. “JIFUNZE KUWA NA MTAZAMO CHANYA.” Ukitumia mbinu hizo zitakubadilisha sana, hutakuwa kama ulivyokuwa.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni