inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 19 Juni 2013

ELIMU: MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO (TEHAMA) KUJIFUNZIA NI SULUHISHO LA ELIMU BORA TANZANIA…




Kufuatia mapinduzi makubwa ya Sayansi na Teknolojia nchini na duniani kwa ujumla mambo mengi yamerahisishwa sana.


Wakati huo huo, uzuri wa Teknolojia unaweza kuleta hasara endapo hakutakuwa na uelewa sahihi wa matumizi.Mfano halisi ni matumizi ya Intaneti kupitia simu za viganjani.Nilitegemea, hii ingekuwa ni fursa kwetu watanzania kuwasaidia watoto wetu kujifunza kwa kupata maarifa kupitia njia hiyo…kinyume chake wanajamii wanatumia intaneti “kuchat” na masuala yanayowahusu, pia kupitia mitandao ya kijamii kwa mambo yasiyojenga. 


Wakati huo huo wanasema walimu hawatoshi na hawafundishi…je umewahi kuchukua jitihada kutafuta njia mbadala? au tunasubiri majibu ya mwisho ya mtihani yatolewe ndiyo tushike vichwa na kutoa lawama kwa Serikali na walimu wake?


Hapa inatakiwa ieleweke kuwa mafanikio ya watoto wetu yanaanzia na sisi wazazi/walezi ikiwa sambamba na watoto wenyewe kujitambua na kutii.


Naomba niwathibitishie kuwa kwa hatua tuliyofikia kimawasiliano na teknolojia ya intaneti kupitia simu zetu, hakuna kitu kisichokosekana mtandaoni kuhusiana na masomo ya watoto wetu. Kuna mwalimu anaitwa Google, You tube…tuanze kuwatumia.


Cha msingi ni kumnunulia mwanafunzi muongozo wa kila somo”syllabus” na kusimamia kujifunza.Shule inakuwa ni sehemu ya kwenda kuuliza maeneo asiyoelewa na kufanya mazoezi kujifua na kile alichojifunza.


Inafika hatua nashangaa sana kuona teknolojia inabadilika kwa kasi na watu wanaipokea kwa kasi kinyume na matumizi hasa kwenye nyanja hii nyeti ya kujielimisha.


Si kitu cha ajabu kumuona kijana/mwanafunzi anatumia tabiti “tablet” kusikilizia muziki, kuchati na marafiki na kutazama sinema…ukimuuliza maswali kuhusu masomo ya shuleni anakujibu mwalimu hajafundisha bado.Hivi, tutamtegea mwalimu kwa asilimia 100% hadi lini? 

Hili linachangia  kwa asilimia nyingi idadi kubwa ya wanafunzi wa sekondari kufeli na wale walio vyuo vikuu kukosa mbinu za utendaji katika soko la ajira. Bila shaka unauona mwelekeo wa jahazi la elimu ya Tanzania…huna haja ya kuwa na Shahada ya uzamili(Masters) au ile ya uzamivu(PhD) ili kujua hatima yake.


Nikiendelea sana, watu watasema nawapangia matumizi ya simu na tabiti au komputa zao.Lakini uhalisia ndiyo huo.Tunatakiwa kubadilika ili kulikomboa jahazi la elimu ya Tanzania.


Ukiwa ni mzazi/mlezi mwenye mapenzi mema na unataka kumuandaa mwanao kusoma kuendana na teknolojia ya habari na mawasialino, pia usiyetaka mizigo isiyo ya lazima hapo baadaye, chukua hatua sasa kumsaidia mwanao kielimu na kujitambua kabla maji hayajamwagika!

Unaweza kuwasiliana  Jielimishe Kwanza! kwa ushauri zaidi.


Simu ya kiganjani: +255 754 572 143

Barua pepe: jielimishekwanza@gmail.com

Imetolewa na Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni