inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 23 Juni 2013

FAMILIA: UGOMVI WA WAZAZI… WATOTO KUKOSA MUELEKEO!


Malezi bora ya watoto huchangiwa na ushirikiano wa pamoja wa baba na mama.Kisaikolojia, mtoto hujengeka na kuwa na furaha kutokana na kuwepo kwa furaha na upendo wa wazazi.


Ifahamike kuwa muunganiko wa wazazi kwa ndoa au la unaimarika zaidi kwa kuwepo na mtoto/watoto. Licha ya kuwepo na tofauti za hapa na pale ndani ya wapendanao lakini haitakiwi watoto wajue tofauti zilizopo.


Picha imetolewa:www.ehow.com
Ugomvi wa aina yoyote ile unatakiwa kupata usuluhishi wa watu wawili(baba na mama) kama walivyoanza wakiwa chumbani…watoto/mtoto hawapaswi kujua kinachoendelea isipokuwa wawaone wazazi wakipendana na kuona furaha ikitawala ndani ya familia.


Hali ikizidi kuwa mbaya, basi usuluhisi unaweza kufikishwa katika ngazi nyingine za usuluhishi kama viongozi wa dini,wazee wa familia na ngazi nyingine zinazofaa.


Katika jamii zetu tunazoishi, hasa kwa kipindi hiki kumekuwa na tabia iliyozoeleka kwa wazazi kugombana mara kwa mara na kufikia hatua ya kutengana kwa sababu wanazojijua bila ya kujali kuwa wamezaa watoto.


Madhara ayapatayo mtoto kwa wazazi kugombana na kutengana

Hapa nitatoa baadhi ya madhara yanayoonekana kirahisi ayapatayo mtoto/watoto kwa wazazi kugombana na kutengana kwa talaka au njia nyingine;

  •  Mtoto anaweza kujengeka na tabia ya ugomvi-hii ni elimu ya awali kabisa kutoka kwa wazazi wake
  • Suala la wazazi kutengana linaweza kuwafanya watoto kuwa njia panda-waende kwa mama au baba kwa sababu hawana chuki na wazazi wao(wanawapenda wote).Endapo wataenda na kukubaliana na mawazo ya mzazi mmoja, mwingine anakasirika na kusema watoto wa siku hizi wanadharau wazazi wao.

  • Mtoto anaweza kuondoka nyumbani  na kuamua kuishi maisha yake kwa sababu upendo umetoweka nyumbani.Hili humuweka mtoto kuwa huru kufanya lolote kwa sababu ushirikiano wa kumlea umevunjika.Pia ni kichocheo kikubwa cha ongezeko la watoto wa mitaani/watoto waishio kwenye mazingira magumu

  • Mtoto anaweza kupoteza muelekeo kimasomo, hii ni sambamba na kushuka kwa taaluma yake au kuacha shule kabisa

  • Mtoto anaweza kupatwa na msongo wa mawazo ulio juu ya uwezo wake, hivyo kupoteza furaha na kuwa mnyonge


Tukilitazama jambo hili kwa upande wa pili; kuna wakati kutengana kwa wazazi kunaweza kuwa na faida kwa pande zote (mzazi mmoja na watoto).


Kama alivyoainisha mtaalamu wa masuala ya talaka, divorce Judith Wallerstein  kuwa ni jambo la busara kutengana kwa talaka endapo watoto watapata mateso ya kihisia,kupigwa au kunyanyaswa kijinsia na mzazi mmoja, au mzazi mmoja anapokuwa mlevi kupindukia na kusahau majukumu ya familia.


Jamii na wanandoa kwa ujumla tujitaidi kudumisha mahusiano ili tuwalee watoto kwa pamoja hivyo kuepusha ongezeko la watoto wasiokuwa na muelekeo, pia watoto wa mitaani.

Imetolewa na

Jielimishe Kwanza!




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni