inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 16 Julai 2013

ELIMU NA MTAZAMO: MBINU 10 ZA KUANZA KUSOMA KITABU CHENYE TIJA YA MAENDELEO


Nikizingatia makala iliyoandikwa kuhusu kuijua siri iliyopo ndani ya vitabu http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/ifahamu-siri-iliyopo-ndani-ya-vitabu.html unaweza kujua umuhimu au faida mbali mbali unazoweza kupata.
Imekuwa ni utamaduni wa Watanzania wengi na Waafrika wengi kupuuzia suala la usomaji vitabu hasa vyenye kujenga,kuongeza uwezo wa utendaji,kuamsha hisia za utendaji, na vingine vyenye maudhui chanya.
Kupitia makala tajwa nilieleza faida mbali mbali tunazoweza kuzipata moja kwa moja kwa kusoma vitabu.Tuondoe visingizio mbali mbali kuhusu suala zima la usomaji wa vitabu mfano suala la uvivu.
Picha na www.praesa.org.za
Napenda nikupe mbinu na hatua za kufuata ukitaka kusoma kitabu ukipendacho kuhusu maendeleo, ni vyema ukaanza kuzifanyia kazi hatua kwa hatua kama mtoto mdogo anavyojifunza (kama ilijulikanavyo na wasomi wengi kuwa ukitaka kujifunza vizuri ni vyema kujiweka kwenye nafasi ya mtoto):
1.Anza kusoma kitabu chenye kurasa chache
2.Chagua kitabu kinachoeleza wazo moja kwa kurasa moja au mbili
3.Una uhuru kuanza kusoma wazo lolote unalolipenda…si lazima uanze mwanzo wa kitabu
4.Jiwekee malengo ya kusoma kurasa moja au mbili kwa siku…unaweza kuongeza kutegemeana na uhitaji na shauku ya kusoma zaidi
5.Tumia kalamu ya kuweka kivuli kwa sehemu muhimu sana-zitakusaidia baadaye kuweka utekelezaji
6.Mara zote usiache kutembea na kitabu ukipendacho…unaweza kusoma muda wowote ukihitaji kusoma
7.Ukifanikiwa kutimiza mbinu 1,2,3,4,5,na kumaliza kusoma kitabu ulichokichagua, vuka hatua nyingine kubwa kuanza kusoma kitabu kingine ukiongeza idadi ya kurasa-hasa kile kinachotoa maelezo marefu kuhusu wazo moja kwa kurasa zaidi ya kumi.
8.Jichunguze uwezo na mapungufu yako kulingana na ujuzi uliopata kupitia kitabu ulichosoma.Chunguza fursa zilizopo katika nchi yako ukilinganisha na ujuzi ulioupata kwa kusoma kitabu.
9.Jipongeze unapomaliza kusoma kitabu kimoja na kujifunza mbinu mpya ya kuboresha maisha yako na ya wengine.
10.Chagua wazo moja au ujuzi uliopata kwa majaribio katika maisha halisi(weka katika utendaji).
Pia unaweza kutumia ipad yako kusoma kitabu ukitakacho.

Picha na app-of-ipad.blogspot.com
Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi  zifanyie kazi hizo mbinu 10,  pia tuungane wakati mwingine na makala “Mjengee mtoto wako tabia ya kusoma vitabu”.Makala  ijayo itakuwa ya msaada mkubwa endapo utakuwa kioo kwa mtoto kwa kutimiza hizo mbinu 10 kwa ukamilifu.
Usiposoma kitabu chochote, utapitwa na maarifa, utakosa fursa mbali mbali pia utaamini sana ufahamu wako(si kweli kuwa unafahamu vitu vyote zaidi ya wengine)...

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni