inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 10 Juni 2013

ELIMU: IFAHAMU SIRI YA MAFANIKIO YA SHULE HIZI BORA NCHINI TANZANIA -2012!




Picha imetolewa:http://www.urusecondary.sc.tz/school.htm
Picha imetolewa:http://www.marianschool.site40.net/


Picha imetolewa:www.sajasemoshi.catholicweb.com/
Tunapozungumzia shule za sekondari bora nchini Tanzania, tunaangalia kigezo kikubwa cha kufaulisha wanafunzi katika mitihani ya kitaifa (NECTA). Mambo mengine ni mbwembwe tu na kupuliza upepo.

Tovuti http://serveafrica.info/tanzania/top-10-secondary-schools imeziainisha shule kumi (10) bora nchini Tanzania katika matokeo ya kitaifa 2012 ya kidato cha (IV) kama yalivyotolewa na baraza la mitihani la Taifa (NECTA).

Shule hizo ni;
1.     URU SEMINARY    http://www.urusecondary.sc.tz/school.htm
2.     MARIAN GIRLS SECONDARY SCHOOL http://www.marianschool.site40.net/
3.     ST. JAMES SEMINARY http://www.sajasemoshi.catholicweb.com/
4.      FEZA BOYS’ SECONDARY SCHOOL http://www.fezaschool.org/
5.     TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
6.    MZUMBE SECONDARY SCHOOL
7.     MAFINGA SEMINARY http://mafingaseminary.com/
8.     DUNGUNYI SEMINARY
9.     PARANE SECONDARY SCHOOL
10. ARUSHA SECONDARY SCHOOL

Kuna suala la muhimu la kuangalia zaidi ya ufaulu wa mitihani.Je, elimu wanayopata wanafunzi wetu ina tija ya kuwawezesha kutumia kile walichokisomea na kujiajiri mara tu wamalizapo mfumo wa kusomea kazi-elimu ya vyuo vikuu? AU ni ule umaridadi wa vyeti lakini hakuna uwezo wa kutumia wanachokifahamu?

Nayasema haya kwa sababu ya ushahidi wa kutosha uliopo katika ngazi wanazoendelea wanafunzi hao kuwa kuna jambo la kushangaza kumuona mwanafunzi aliyepata daraja la I au la II akishindwa kuendelea na hatua ya chuo kikuu.Hapa swali linakuja, mwanafunzi huyu aliwezaje kupata daraja la I akiwa kidato cha IV?

Naomba nisieleweke vibaya, kuwa napinga matokeo mazuri ya kitaaluma, ila naweka angalizo tu kwa shule zilizofanya vizuri na zile zenye ndoto ya kufanya vizuri kwenye matokeo ya mitihani kitaifa.

Tuwajenge wanafunzi wetu kuendana na changamoto za ajira na mabadiliko ya  Sayansi na Teknolojia. Tuwajengee wanafunzi uwezo wa kuwa watendaji na si wajuaji, kwa sababu watu wengi wanajua ili watendaji  wazuri ni wachache.

Tukiachana na hilo, naomba niwajulishe siri ya mafanikio ya shule hizi bora nchini Tanzania kwa mwaka 2012;
·      Uongozi thabiti wa shule hizo
·      Usimamizi mzuri wa maadili ya wanafunzi na walimu
·      Ushirikiano wa karibu wa walimu,wanafunzi na wazazi
·   Wanafunzi wanaochukuliwa kwenye shule hizo ni wenye alama nzuri kutoka shule ya msingi
·      Mazingira mazuri ya kujifunzia…tembelea shule hizo utajionea mwenyewe
·      Ubora wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia
· Naomba ufuatilie motisha wanazopewa walimu wa shule hizo…utagundua kuwa zinawahamasisha kufanya kazi kwa bidii.

Naomba iwe funzo na changamoto kwa shule zinazochechemea ili kuyafikia malengo ya elimu bora nchini Tanzania. Kuna njia kama mbili za kujifunza kutoka katika shule hizo bora; moja tazama mwenendo wa shule hizo, pili nenda uwaulize-kuhusu mbinu wanazotumia kutoa elimu bora.
Jielimishe Kwanza! , zitumie mbinu hizo kwa vitendo, utaona mabadiliko.

Jielimishe Kwanza!
Inaalika maombi kwa shule mbali mbali nchini kwa ajili ya kuwajengea wanafunzi uwezo wa kupambana na changamoto za ajira, kujitambua,kuweka malengo,kuishi kwa kutimiza ndoto, kuboresha vipaji vya wanafunzi na elimu ya jinsia.
Tuwasiliane kwa kutuandikia:
Au
+255 754 572 143
TUTEMBELEE OFISINI:
-->
Sinza “B” Kitalu na 187, Shekilango road
Dar es salaam,
Tanzania.

Maoni 1 :