inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 28 Juni 2013

JAMII NA MAWASILIANO: HIVI NDIVYO SIMU ZA MIKONONI ZINAVYOTUTENGA…


Mfumuko wa Teknolojia ya mawasiliano na upatikanaji wa simu za viganjani kirahisi hasa zenye intaneti zimetufikisha hapa tulipo. Si kwa lengo baya bali jema kabisa endapo tutakuwa na mipaka ya matumizi na kuchagua vitu muhimu vya kuangalia tukizingatia kutunza wakati.
Tukiendekeza sana urafiki na simu ya mkononi kwa kuchati…tutajikuta tupo mbali na eneo halisi tulipo.Hii ni hatari, kwa sababu itamfanya mtu asijue kitu kinachoendelea jirani yake na wakati huo huo akiwa makini na mambo ya mbali.
Mfano: mtu anakata mazungumzo na mtu aliye naye jirani na kujikita na mawasiliano ya anga hivyo kushindwa kutimiza lengo la kuwa jirani.
Hivi sasa, ndani ya familia kumekuwa na migogoro mingi inayosababishwa na kuendekeza matumizi ya simu kupita kiasi.Wazazi hawaongei na watoto kuhusu malezi na kumwachia mwalimu aitwae “Teknolojia ya Habari na Mawasiliano-TEHAMA” afanye kazi yake.
Nikirejea makala yangu kuhusu umuhimu wa TEHAMA kwa wanafunzi kujifunza ya Jumatano,19 Juni 2013-http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/06/elimu_19.html.Ni vizuri kumtumia mwalimu huyu, lakini tujue fika kuwa anafundisha kila kitu; mema na mabaya kama hakuna uangalizi wa kutosha na uelimishaji sahihi wa matumizi ya teknolojia hii.

Kuthibitisha ukweli wa jambo hili, tazama video ifuatayo;
Hili ni angalizo tu, naomba nisieleweke vibaya…hii ndiyo hali halisi inayoendelea siku hadi siku.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni