inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 23 Septemba 2013

MALEZI NA FAMILIA: MWELEZE YAFUATAYO MTOTO WAKO KUHUSU SHULE…

Wazazi wengi wamekuwa wakipata wakati mgumu sana kuwaeleza watoto wao kuhusu shule na faida zake sanjari na mustakabali wa maisha ya watoto wao.
Picha na
changeyourfate.org 


Wazazi wengine wamefikia hatua ya kuwadanganya watoto wao kuwa “…mimi nilikuwa nashika nafasi ya kwanza darasani hadi namaliza shule…” hii haijalishi kwao kuwa wameenda shule au la! Kila mzazi anasema alikuwa anashika nafasi ya kwanza darasani…mh! Sijui nani alikuwa wa mwisho darasani? Naomba tusifikie hapo, kuna njia nyingine ya kuwaeleza watoto wetu kuhusu shule.
Picha na www.alltreatment.com


...Inafahamika fika kuwa wazazi wengi huitaji mabadiko au maboresho katika mfumo wa elimu, lakini hivyo hivyo wanaona umuhimu wa watoto wao kwenda shule...

Leo naomba uchukue hatua muhimu na rahisi kumueleza mtoto wako kuhusu shule kama ifuatavyo;
1.ELIMU NI HATUA ENDELEVU MAISHANI
Kwenda shule ni hatua mojawapo-lakini ni hatua ndogo sana.Ukiwa shule utajifunza mbinu mbali mbali…hii isikufanye ukaacha kujifunza masuala mengine uyapendayo.Ichukulie elimu kama chaguo la kuboresha kipaji chako(Tukiamini, pia ni uhalisia kuwa kila binadamu ana kipaji chake).

2.SHULE NI HATUA YA AWALI YA KUAJIRIWA.
Shule inakuandaa kujipatia kipato cha halali, lakini si lazima kukupatia mali.

3.TAMBUA KUWA SHULE NI SEHEMU YA KUFAULU NA KUFELI
Soma kwa bidii.Pata ujasiri wa kusonga mbele pale unapofaulu pia pata ujasiri wa kuinuka tena pale unapoanguka(Kufeli).

4.UKIANZA SHULE, JITOLEE KUMALIZA
Jifunze kupambana na changamoto mbali mbali bila ya kukata tamaa.Tambua kuwa shule ni sehemu ya changamoto.

5.SHULE NI SEHEMU MUHIMU YA KUPATA HABARI
Tambua kuwa walimu wako ni watafiti, tumia taarifa zao, uliza maswali…fanya majaribio ya mara kwa mara ukitumia taarifa hizo kulingana na kile unachokipenda.Fuatilia kwa kina taarifa hizo kuliko kutegemea kupata majibu sahihi wakati wote ili ufaulu mtihani.

6. NI VYEMA UKAONEKANA MJINGA KULIKO KUWA MJINGA
Kama huelewi jambo Fulani, ni vyema kuuliza ili kupata ufafanuzi.Mwalimu akihitaji mtu kujitolea, jitolee.Watu hujifunza zaidi kwa kushirikishwa kuliko kukaa kimya ili kuonekana mtulivu.Uwe tayari kufanya makosa-hii ni hatua ya awali ya kujifunza.Fanya makosa sana.Kuwa na heshima lakini mchangamfu!

7.CHUKULIA FAIDA YA KUWA MDOGO
Hatua ya utoto ina faida zake, muda wa kutosha hasa baada ya masomo.Tumia muda huo kudadisi masuala mbali mbali.

8.TAFUTA KUPATA MAJIBU SAHII…LAKINI USIISHIE HAPO!
Tafuta jibu analohitaji mwalimu, lakini hakikisha una majibu si chini ya mawili.Kuwa na uwezo wa kutafuta majibu zaidi kwa maswali na matatizo mbali mbali ni njia mojawapo ya kuwa na wigo mpana wa kutatua matatizo.Maisha bila machaguo ni rahisi sana kuwa taabu.

9.JIAMINI…
Kila mtu ana uwezo wa kuelewa na kupambanua.Alama zako darasani hazibashiri kile utakachoweza kufanya baada ya shule.Fuata ndoto yako haijalishi watu wanasema nini…

10.UPENDO WANGU KWAKO NI WA MILELE
Waambie watoto wako, haijalishi alama gani wanapata shuleni, wao ni wa muhimu kwako.Kumbuka kuwa shule ni kama mchezo wa kupata na kupoteza, lakini utawapenda milele.

Makala hii imeandaliwa na Jielimishe Kwanza! kwa kushirikiana na Kitabu kiitwacho “Be Rich and Happy” kilichoandikwa na Robert Kiyosaki- Sura ya 25, Ukurasa wa  259-261.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni