inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 21 Septemba 2013

MALEZI NA FAMILIA:NDOA KATIKA UMRI MDOGO...


-->
M
Picha na plancanada.ca
ara nyingi wasichana wenye umri mdogo wamekuwa wakiozeshwa kwa kushurutishwa na wazazi, pia ndugu wa karibu kama njia mojawapo ya kujiingizia kipato na mali.Huu umekuwa ni utaratibu uliozoeleka sana, na wengine kuchukulia kama sehemu ya utamaduni.







                                                                                                                                                        
Hali  hii isiyo ya kawaida inajitokeza sana katika nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara. Tabia hii mbaya isiyojali haki ya mtoto wa kike imesababishia wasichana wengi kukosa fursa za kuendelea kukua kifikra,pia kushindwa kuendelea na masomo.
Msichana asipopata mahitaji yote hayo muhimu itamfanya awe tegemezi katika maisha yake yote.Hivyo iwapo mtoto wa kike ataozwa katika umri mdogo kuna uewezekano mkubwa wa kutojua kusoma na kuandika au atakuwa amepata elimu ya kiwango cha chini, hali hiyo itamfanya awe mtu masikini na hataweza kujitetea katika maswala ya ngono na nyumbani ukizingatia kwamba mara yingi msichana anaozwa kwa mtu mwenye umri mkubwa mara mbili yake,  ambaye tayari amekuwa ni mzoefu.
Katika hali hii mtoto huyu wa kike anakuwa na uhusiano tegemezi,uhusiano ambao mara nyingi huwa ni uonevu hasa ukizingatia ukweli wa hali ya kiuchumi. Kwa ufupi matarajio juu ya mtoto wa kike yamedumaa na ndiyo maana watoto wa kike wanapata athari kubwa zaidi ukichulia  kuwa msichana huyu mdogo  anatakiwa atoke kutafuta,lakini pia aangalie familia na kumuhudumia mume, wakati mwingine kukosa haki ya kula matunda ya jasho lake kwa sababu ya ukatili wa mwanaume.
Binti ambaye ndiye mke, asiye na elimu ya uzazi anapata shida ya kutambua haki ya kumuwezesha yeye kupumzika baada ya kujifungua.Hili hupelekea kuwa na watoto wengi ambao ni vigumu
kuwahudumia, matokeo yake ni kuongezeka kwa watoto wa mitaani. Jamii inapaswa kutambua na kubadilika,kujua kuwa jinsia zote zina haki sawa,mtoto wa kike na wanawake kwa ujumla wanapaswa kuheshimiwa na kupewa haki zao kama ilivyo kwa watoto wa kiume na wanaume.
Wasichana wadogo wanapaswa kulindwa na tatizo la ndoa za utotoni  pia kupewa fursa ya elimu.
Picha na plancanada.ca
Ndoa za umri mdogo siyo nzuri na hazitakiwi,madhara yake ni makubwa kuanzia kwenye familia na Taifa kwa ujumla.
Jielimishe Kwanza! Badilika!
Na Linda Kagemulo, 0654289805,
lindakagemulo@gmail.com
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni