inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 21 Septemba 2013

MTAZAMO: SOMO KUPITIA MIMEA…TAFUTA FURSA UONEKANE!

-->

N
 apenda kushirikiana nawe msomaji wangu kuhusu uumbaji wa Mungu ukihusisha na maisha yetu ya kila siku. Aliumba viumbe hai na visivyo hai, pia alimweka mwanadamu kuwa mtawala wa hivyo vyote.

Kupitia utashi aliopewa mwanadamu, aliweza kubuni mbinu mbali za kuwatunza viumbe wengine…natumaini tunatimiza lengo la kuwatunza viumbe hao wengine wasio na utashi.Kama tumesahau basi tukumbuke kazi tuliyotumwa!

Tukirudi katika maisha ya kawaida tunayoishi, mwanadamu amekuwa akigundua vitu vingi ili kutatua changamoto zinazomzunguka.

Kama upo makini na mdadisi utagundua kuwa vitu vingi afanyavyo mwanadamu kwa ubunifu ni kama amedurufu kazi ya uumbaji wa Mungu.

Kuna mifano mingi ya kuangalia; chukulia muonekano wa umbo la chombo cha usafiri wa anga (ndege) kushabihiana na umbo la ndege arukaye, matoleo mengi ya magari yanayopagawisha watu na vyombo vingine vya usafiri hushabihiana sana na viumbe hai alivyoviweka Mungu.
Picha na www.hdwallpaperstop.com


Hapa naomba niseme kuwa hati miliki ya ubunifu wa mwanadamu anamiliki Mungu na si kama wengine wanavyojisifu na kutamba.

Leo naomba tujifunze kupitia mimea hasa kutafuta na kuziona fursa mbali mbali katika maisha.



Kisayansi, mimea hutegemea sana mwanga wa jua kujitengenezea chakula na kumea mwisho kufikia hatua ya kutunza viumbe hai wengine kama binadamu na wanyama.

Fuatilia kwa makini hatua ya awali ya kuanza kuchipua kwa mmea: mmea ulio katika mazingira mazuri ya kupata mwanga wa jua humea vizuri na kuzaa matunda.

Pia mimea iliyo katika mazingira magumu hujitengenezea mazingira kwa hali yeyote ile ili kuliona jua (FURSA). Mimea mingine hujitahidi kupanda juu ya mimea mingine ili kuliona jua (FURSA). Je, mimea ina akili sana kushinda sisi? La hasha!

Mimea iliyo songwasongwa na magugu na kushindwa kujinasua kupata mwanga wa  jua (FURSA) hudumaa na mwisho kufa.

Je, mimea ina akili sana kushinda sisi? La hasha!

Tuhangaikie suala zima la kuziona fursa kwa hali yeyote ile ili tusife kifikra na kiiuchumi kwa kujifunza kupitia mimea.

Imetolewa na

Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni