inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 10 Septemba 2013

MTAZAMO: HIVI NDIVYO TUNAVYOWEZA KUONDOKANA NA UTUMWA WA KIFIKRA UNAOPELEKEA UMASIKINI…

-->
Nikianza kwa kumnukuu mwanamuziki maarufu wa "Reggae" dunia-Hayati Nesta Robert Marley almaarufu “Bob Marley” aliwahi kusema katika sehemu ya wimbo wa “Redemption Song” kuwa “Emancipate yourselves from mental slavery; None but ourselves can free our mind.” Akiweka msisitizo huo kuwa hakuna mtu mwingine anayeweza kutukomboa/kukukomboa kifikra isipokuwa sisi wenyewe…au wewe mwenyewe. ANGALIA VIDEO NA MASHAIRI YA WIMBO HUO KUPITIA
Kama utatafakari kwa kina utagundua kuwa walio juu kimaendeleo na wenye upeo wa kupambanua mambo hupenda kuwakandamiza walio chini hasa wazubavu na hata kudiriki kupita juu ya vichwa vyao.
Hata siku moja hawawapi nafasi walio chini kuchomoza kimaisha, hasa kwa kuwapa msaada ili waweze kufikiri vizuri na kutenda sawia na wenyewe wanavyotenda.
Hali hii hupelekea kuongezeka kwa wimbi kubwa la wasio nacho na kuimarika kwa kundi la walionacho. Sina hakika kama lengo la Mungu kumuumba mwanadamu ni kuwa masikini…la hasha! Nini husababisha haya yote?
Wabudha wana msemo wao maarufu sana ulio na uhalisia kuwa “What we think, we become.” Wakimaanisha-kwa tafsiri isiyo rasmi kuwa, tunanyoonekana na jinsi tulivyo kimaisha ni kutokana na mawazo yetu.Mfano, tukiendelea kunung'unika sana kuwa nchi hii ni masikini sana na hali kuna rasilimali nyingi hadi wengine wanakuja kugombania…ndivyo ilivyo na itakavyokuwa!
Kiujasiri kabisa, ndugu msomaji, nikutie moyo kuwa tukibadili mtazamo wetu wa kufikiri na kuepukana na utegemezi wa kufikiri tutaondoka hapo tulipo…hivyo kuacha kuimba wimbo huu wa “Nchi yetu ni masikini sana” ambao walio nacho wanaupenda sana kuuimba na kuucheza wakati huo huo wengine-wasio nacho kusikia kelele ndani ya masikio yao na kusononeka mioyo yao.
Tunatakiwa kuamini, kufikiri tofauti na kuangalia tulicho nacho kwanza-mfano kipaji au uwezo wa asili tuliopewa na Mungu kuwa kianzio cha mtaji wetu sambamba na kulinganisha na rasilimali tulizo nazo kusonga mbele.Kuna uthibitisho kutoka kwa wengine walioiona siri hii ya kutumia kile walicho nacho kwanza. Jielimishe Kwanza! Jitambue! Fuatilia! Simamia kwa kutenda!
Tusipende kuwa bendera fuata upepo na kutumika na hao wanaotukandamiza…hata siku moja hawawezi kutukomboa kifikra.
Huu ni mtazamo wa Jielimsihe Kwanza! Tunakutakia kila la heri katika kubadili mtazamo kuwa chanya!
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni