inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 11 Septemba 2013

MAZINGIRA: JUHUDI NA CHANGAMOTO ZA USIMAMIZI WA SHERIA NDOGO ZA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA…


Katika pita pita za kuchunguza usimamizi wa sheria ndogo za kulinda na kutunza mazingira zinazowekwa na Halmashauri mbali mbali kwa ushirikiano wa wananchi nchini Tanzania, Jielimishe Kwanza! ilifanikiwa kujionea hali isiyo ya kawaida pembezoni mwa bara bara ya Ali Hassani Mwinyi jijini Dar es salaam. 

Pichani ni bango linalojieleza vizuri kabisa…ikiwa ni amri kutoka katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kudhibiti utupaji ovyo taka katika eneo husika.
Kuna maswali ya msingi ya kujiuliza…je, matangazo/vibao vya kutoa onyo vinaendana na utekelezaji? Je, kuna ufuatiliaji/usimamiaji wa sheria  mara tu baada ya kuweka vibao/matangazo ya onyo?Au ni wakati gani sheria hizo ndogo huwa na meno?...usiku au mchana?...wakati wa ugeni mkubwa au la? Hapo unaweza kulinganisha matokeo ya ukiukwaji au utekelezwaji wa sheria hizo ndogo.

Ifahamike kuwa, kama hakuna ufuatiliaji/utekelezaji wa onyo zinazotolewa, hali huwa mbaya zaidi ya mwanzo…mwanadamu akipewa onyo halafu asione utendaji/madhara ya kukiuka  onyo, hupuuzia onyo hilo na kuchukulia hali kimazoea.

Ushauri wetu namba 1, tunashauri...mabango/vibao vya onyo vieleze aina ya adhabu atakayopata mtupaji taka katika eneo husika…Hasa adhabu ya fedha taslimu.Pia ni vyema kutumia ufuatiliaji shirikishi/jamii kwa kutoa motisha ya nusu ya fedha taslimu itolewayo kama adhabu kwa watoa taarifa ya uchafuzi wowote wa mazingira.Hii inaweza kuwa chanzo cha mapato kwa mtoa taarifa na Halmashauri husika kwa ujumla wakati huo huo jiji liking'ara.
 
 Ushauri wetu namba 2, tunashauri kutenga maeneo rasmi kwa ajili ya kutupa taka na kuwe na ufuatiliaji wa mara kwa mara kuhakikisha taka hazirundikani kwa muda mrefu.Kwa kutumia mapato ya ushauri namba 1...yanaweza kuboresha huduma ya ushauri namba 2.
 
 
Soma mfano wa kuigwa wa mbinu za kuhifadhi mazingira kupitia mji wa Moshi uliofanikiwa katika kusimamia sheria ndogo ya uhifadhi wa mazingira http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/08/mazingira-hii-ndiyo-siri-ya-usafi-wa.html
 
 
Jamii kwa ujumla inapaswa kujua uhalifu na uchafuzi wa mazingira wa aina yoyote ile una athari kubwa kwa kila mwanadamu...tushirikiane kwa pamoja kuipendezesha dunia hii inayotutunza.

 
Imetolewa na,
Jielimishe Kwanza!
Kwa kuthamini umuhimu wa mazingira safi kwa afya bora!
 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni