inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 4 Mei 2014

MTAZAMO: USITOE MAAMUZI HASI BILA KUFANYA UTAFITI WA KUTOSHA…

-->
 
Napenda kuanza kwa kuwapongeza wafanyakazi wote hasa kwa kuzingatia Mei mosi ilikuwa ni siku ya kilele cha sherehe ya Wafanyakazi.

Photo:http://www.mentoringminds.com/socratic
Nianze kwa kuuliza maswali; ni mara ngapi tumekuwa tukiwafikiria na kuwatendea wengine visivyo(hasi) na baadaye tunagundua kuwa haikuwa kama tulivyokuwa tunafikiria? Je,unajisikiaje katika hali hii ya kuujua ukweli? Bila shaka, hakuna anayeweza kupinga ukweli huu kuwa binadamu tunaamini sana hisia zetu na kujitengenezea majibu mepesi kwa maswali magumu kuliko kuamini akili zetu.
Sina maana kuwa hatutumii akili zetu,ila mara nyingine tunakuwa wavivu kidogo katika kutoa maamuzi sahihi, na hii ni kwa sababu hisia zetu huchukua nafasi kubwa katika mazingira fulani…majibu yatokanayo na hisia hayaumizi kichwa wala kuuchosha ubongo na ni ya haraka.
Mungu katupatia akili ili tufikiri kwa makini, kupambanua na “kujua ukweli wa mambo” kama Mwl.J.K.Nyerere alivyoandika katika kitabu cha TUJISAHIHISHE kuwa Kujielimisha Kwanza ni kujua ukweli wa mambo, huwezi kujua ukweli wa mambo kwa kuendeshwa na hisia.
Nikuhakikishie ndugu msomaji kuwa, hakuna kitu kibaya kama ukamfikiria ndugu au rafiki yako kimtazamo hasi na akatambua jinsi unavyomchukulia tofauti na alivyo kiasili.Itakupa shida sana hapo baadaye ukibaini ukweli wa mambo.Ikiwa unataka kujua ukweli wa mambo unapaswa pia kufanya utafiti wa kutosha kabla ya kutoa maamuzi hasi. Soma
Hatupaswi kukurupuka na kujiwekea majibu ya kihisia…mfano: eti naona ndugu yangu hanichangamkii tena, nafikiri ameona sina kipato. Pia kutoa suluhisho la kupotelewa  pesa kisha kumshuku mtu fulani kaiba na unaanza kumvamia kwa maneno hata ngumi, baadaye kidogo unakumbuka kuwa kuna kitu ulinunua na mahesabu yako sawa…utajisikiaje katika hali hii?
Kuna madhara makubwa ya kutoa maamuzi hasi bila kuwa na utafiti wa kutosha.Nimejaribu kugusia kidogo baadhi ya madhara hayo hasa kuvunjika kwa uhusiano kwa kirafiki, hii inamwonyesha mwingine hali ya kutokuaminiana katika urafiki.
Ikiwa utahitaji kujua madhara mengine ya Kisaikolojia ya kutoa maamuzi hasi bila ya kufanya utafiti, tuwasiliane +255 754 572 143.
Imetayarishwa na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Maoni 1 :

  1. ni kweli kabisa...hii imenitokea! Nashukuru sana Jielimishe Kwanza kwa elimu hii

    JibuFuta