inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 19 Desemba 2013

MTAZAMO: TASWIRA UNAYOWAJENGEA WATU WENGINE INAKUWA UHALISIA WAKO…


“The image you create about others and think it is real, becomes your reality”-Henry Kazula.

M
ara nyingi tumekuwa tukiwafikiria na kuwasema wengine kinyume na uhalisia wao.Kuna watu huwafikiria wengine mabaya tu, pia kujiaminisha kuwa mafanikio ya wengine si ya halali au maisha wanayoishi wengine si halisi.
Yaani, tunawafikiria wenzetu mabaya! mabaya! tu.Huu ni mtazamo hasi uliojijenga ndani ya nafsi za watu.
Kwa kipindi kirefu Jielimishe Kwanza! imefuatilia suala la mtazamo wa watu kuhusu maisha na watu kwa ujumla.Imebainika kuwa ukiwasikiliza watu 5 kuhusu ufikiri/mtazamo wao kwa watu fulani waliofanikiwa na hata wale wasiofanikiwa utagundua kuwa ni mmoja tu atakayetoa maelezo yenye mtazamo chanya.Kama huamini, fanya jaribio hili la kupima mtazamo wa watu.
Ikiwa taswira unazojingea kuhusu wengine ni hasi, huu utakuwa ni uhalisia wako! na utajiaminisha, utakuwa ni mtu wa manung’uniko, masengenyo, kukata tamaa ya maisha kwa kujiaminisha kuwa huwezi kufanikiwa kwa njia ya halali inayohusisha juhudi zako binafsi.Madhala yake kwa Taifa ni makubwa, hususan kuongezeka kwa wimbi la umasikini na utegemezi ndani ya jamii.
Pia utajikuta umeanza kujijengea mbinu zisizo sahihi kupambana na uhalisia unaofikiria kuhusu hali na tabia ya maisha ya wengine.
Nikirudi kwenye mahusiano kwa wanandoa, kuna hatari kubwa endapo mmoja wa wanandoa atakuwa na taswira hasi kuhusu mwenziwe.Mfano, mmoja akimfikiria na kujenga taswira kuwa mwenziwe anatoka nje ya ndoa, itamjenga na itakuwa ni uhalisia wake bila ya kuwa na utafiti wa kina.Hili hupelekea kuvunjika kwa ndoa nyingi kwa sababu ya kukosa kuaminiana.
Nakuhamasisha ndugu msomaji, kubadili mtazamo kwa kujifunza jinsi ya kuishi na watu na kufahamu njia halali za mafanikio yao…fuatilia historia zao ili uwe na uthibitisho wa unachokiamini, kufikiria kabla ya kutoa ushuhuda mbele ya wengine.
Tukumbuke kuwa, Maaandiko Matakatifu yanatuasa kuwa si vizuri kufikiria na kuwasemea wengine mabaya.
Imetayarishwa na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni