inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 9 Aprili 2015

AJIRA: USITISHWAJI WA AJIRA KWA SABABU YA UTOVU WA NIDHAMU MAHALA PA KAZI

-->
Picha na dailyjobads.com
Usitishaji wa ajira ni kukoma  kwa ajira (mkataba wa ajira) kunakosababishwa na mambo mbalimbali kama; mfanyakazi kujiuzulu (kuacha kazi kwa hiari), muajiri kusababisha mazingira magumu kwa muajiriwa kuendelea na kazi, muajiri kushindwa kumruhusu muajiriwa kurudi kazini baada ya likizo (ya uzazi au ya mwaka) na mfanyakazi kuachishwa kazi kwa utovu wa nidhamu.
Utovu wa nidhamu ni sababu kubwa inayoweza kupelekea kusitisha ajira. Hata hivyo muajiri hapaswi kuchukua hatua zozote za kinidhamu dhidi ya muajiriwa mpaka pale atakapokutana naye kwanza na kujadili suala hilo. Pia katika Kanuni za Utendaji Bora Mahala pa Kazi za mwaka 2007 imeelezwa wazi kuwa muajiri anapaswa kuweka kanuni za kusimamia nidhamu zinazoeleza namna mfanyakazi anavyopaswa kuzingatia nidhamu mahali pa kazi. Muajiri anapaswa kuwafahamisha wafanyakazi kanuni hizo wakati wa kuajiri.
Kama hiyo haitoshi, Kanuni hizo pia zimetoa muongozo/utaratibu wa kusitisha ajira kwa sababu ya utovu wa nidhamu. Kabla ya kumuachisha kazi mfanyakazi, muajiri anatakiwa kufikiria kwa umakini na kuzingatia mambo yafuatayo:-
    i.         Je, mfanyakazi amekiuka kanuni za nidhamu za kampuni/ taasisi?
  ii.         Je, kanuni iliyokiukwa ni ya msingi na haki?
iii.      Je, kanuni iliyokiukwa inaeleweka kwa mfanyakazi na haina utata? Na
iv.         Je, kanuni iliyokiukwa imekuwa ikitumika na muajiri kwa usawa?
Katika Kanuni za Utendaji Bora Mahala pa Kazi za mwaka 2007, Kanuni ya 12 (2) imeelezwa kuwa kosa la kwanza la mfanyakazi halihalalishi adhabu ya kuachisha kazi isipokuwa pale itakapothibitika kuwa kosa ni kubwa kiasi cha kuharibu uhusiano wa kiajira kiasi cha kutovumilika. Pia katika Kanuni ya 12 (3) yametajwa makosa makubwa yanayoweza kuhalalisha mfanyakazi kuachishwa kazi kwa kosa la kwanza. Makosa hayo yametajwa kuwa ni pamoja na:-
a)   Kukosa uaminifu kulikokithiri
b)  Kuharibu mali kwa makusudi
c)   Uzembe uliokithiri
d)  Kuhatarisha usalama wa watu wengine kwa kukusudia
e)   Kushambulia wafanyakazi wengine, wateja au mtu mwingine yeyote mwenye kuhusiana na muajiri
f)    Ukaidi uliokithiri.
Pamoja na muajiri kuweza kumuachisha kazi mfanyakazi mara moja kutokana na makosa yaliyoainishwa hapo juu, Kanuni zimeweka utaratibu wa haki ambao muajiri anapaswa kuufuata kabla ya kuchukua hatua za kinidhamu juu ya mfanyakazi anayetuhumiwa kwa  kosa la kinidhamu.
Kabla ya kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya mfanyakazi mtuhumiwa, muajiri anatakiwa kufanya uchunguzi ili kubaini iwapo kuna haja ya kuitisha kikao cha nidhamu. Muajiri atakapobaini kuwa ipo haja ya kuitisha kikao cha nidhamu atapaswa kufanya mambo yafuatayo:-
    i.         Kutoa kwa mfanyakazi taarifa ya tuhuma kwa namna ambayo mfanyakazi ataelewa tuhuma hizo.
  ii.         Kumpa mfanyakazi muda usiopungua saa 48 ili aweze kuandaa utetezi wake.
iii.         Kumueleza mfanyakazi haki yake ya kuwasilishwa na mfanyakazi mwenzake au kiongozi wa chama katika kikao cha nidhamu.
iv.         Kuteua mwenyekiti wa kikao hicho ambaye hajahusika na tatizo lililopelekea kuitishwa kwa kikao cha nidhamu.
   v.         Kumpa mfanyakazi nafasi ya kuwahoji mashahidi wa muajiri na ikibidi kuleta mashahidi wake.
vi.         Kikao kitakapothibitisha tuhuma dhidi ya mfanyakazi mtuhumiwa, muajiri atoe nafasi kwa mfanyakazi kueleza hoja ya kupunguziwa adhabu.
vii.         Kutoa nafasi kwa mtendaji wa chama kuwakilisha katika kikao hicho endapo mfanyakazi mtuhumiwa ni kiongozi au muwakilishi wa chama mahali pa kazi.
viii.         Endapo adhabu inayokusudiwa ni kuachisha kazi, muajiri ni lazima aeleze sababu na pia aeleze haki ya mfanyakazi kukata rufaa.
ix.         Kumpa mfanyakazi nakala ya fomu ya kusikilizia shauri la kinidhamu baada ya kikao.
Pamoja na uwepo wa taratibu hizi, mara kwa mara waajiri wamejikuta wakiingia kwenye migogoro ya kiajira dhidi ya wafanyakazi kwa kuzikiuka.
Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini na. 6 ya mwaka 2004 na Kanuni zake za mwaka 2007 imeweka utaratibu huu ili kupunguza au kumaliza kabisa tatizo la waajiri kusitisha ajira au kuachisha kazi wafanyakazi kwa makosa ya kubambikiwa, lakini pia kumfanya mfanyakazi azingatie suala la nidhamu mahali pa kazi.
Imeandaliwa na Emmanuel C. Zongwe kwa msaada wa vitabu vya sheria na machapisho mbalimbali.
Emmanuel C. Zongwe ni msomi na mtaalamu wa masuala ya Ajira na Mahusiano Mahali pa Kazi. Pia ni Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Mashambani na Kilimo (TPAWU), Wilaya ya Mufindi, Iringa.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.

Maoni 1 :