inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 5 Aprili 2015

MTAZAMO: IMARISHA MTAZAMO WAKO KWA MAFANIKIO MAISHANI…


Katika kitabu chetu kinachofanya vizuri sokoni cha-Mtazamo Wako Ni Upi? Mtazamo Wako, Maisha Yako Na Mwandishi makini Henry Kazula ananukuliwa akisema; “Mtazamo ulio nao kukuhusu ukilinganisha na ule wa wengine unakuwa uhalisia wako kama utaamini” una mantiki kubwa hasa katika kuamini kuwa mtazamo tulionao unakuwa halisi katika maisha yetu kama tutajilinganisha na wengine. Mfano: ikiwa kimtazamo tutaamini kuwa wote waliofanikiwa wamepitia “njia za panya”; ndivyo itakavyokuwa! Hivyo utajijengea mtazamo hasi kuwa watu wote waliofanikiwa wana mafanikio yasiyo halali, ilhali kuna njia kem kem za halali kufikia mafanikio maishani.Mtazamo huo hutufanya watumwa wa mtazamo wa wengine bila kujijua, yaani kupitia mtazamo huo unaamua hatma ya mtazamo wetu tusipochukua hatua za makusudi kujifunza kwa makini kupitia hao waliotuzidi.
Hatupaswi kuwa watumwa wa mtazamo kupitia mtazamo wa wengine tunaowaona wametuzidi kimaisha. Zaidi ya yote, hatupaswi kuruhusu mtazamo wa wengine uamue hatma ya mtazamo wa maisha yetu.
Tunapaswa kujijengea mtazamo wetu ulio thabiti kupitia kujifunza kutoka mtazamo wa wengine kutuhusu kwa kuzingatia kuundwa kwa falsafa binafsi ya maisha yetu. Hii inamaanisha kuwa; mtazamo wetu ulio “jicho la rohoni” kama ilivyo kwa dhamiri –“sauti ya ndani” huunda falsafa binafsi ya maisha yetu.
Jim Rohn-mmoja wa waandishi na msemaji mashuhuri wa hadhara duniani anaainisha ukweli na umuhimu wa kuwa na falsafa binafsi ya maisha kwa kusema; Jijengee falsafa ya maisha yako-“philosopy of lifeikiwa ni dira inayosimamia, kutawala na kuongoza maisha yako.Pia hutuepusha  na hatari mbali mbali ikiwa sambamba na kuingia kwenye mkenge wa kutawaliwa na wengine kifikra na kimtazamo.
Swali la msingi kujiuliza ndugu msomaji; je, tunaimarishaje mtazamo wetu ili kujijengea falsafa binafsi yenye mafanikio maishani? Ikiwa unahitaji kutoka hatua moja hadi nyingine ya kimtazamo kuwa chanya kwa kuzingatia uundwaji wa falsafa binafsi hauna budi kuzingatia  yafuatayo;
 1.KUSOMA VITABU
Ni ukweli usiopingika kuwa kusoma vitabu mbali mbali ili kujitambua kunachangia kujenga mtazamo thabiti unaopelekea kujijengea falsafa binafsi ya maisha.Hii ni njia nzuri kuweza kujua mtazamo wa wengine kukuhusu wewe na kujitathimini kujenga na kuimarisha mtazamo wako.Soma hii kufahamu SIRI iliyopo ndani ya vitabu.
2.NI VYEMA KUHOJI KWANINI
Soma hii kujifunza kuhoji kwanini….
3.JIFUNZE KWA UZOEFU BINAFSI
Jifunze kupitia makosa.Soma hii
4.JIFUNZE KWA KUTAZAMA WENGINE
Njia mojawapo ya kujifunza ni kuwa mtazamaji mzuri wa yale yanayotokea kwa wengine.Utagundua makosa yao na mbinu walizotumia kuondoa makosa.Kupitia njia hii utajifunza mbinu mbali mbali kutoka kwa watu tofauti kuimarisha mtazamo wako. 
5.CHUKUA HATUA YA UJASIRI KUTUMIA MBINU ULIZOJIFUNZA KWA VITENDO
Kujifunza bila vitendo ni sawa na kutojifunza kabisa.Soma hii kujua zaidi.
____________________________________________________
Wakati mwingine nitajikita kwa undani kuelezea kuhusu “Kujijengea Mtazamo na falsafa binafsi ya maisha yako-“philosopy of life”.
Imetayarishwa na,
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni