inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 28 Mei 2013

ELIMU NA UTENDAJI: KUFAHAMU BILA YA KUTENDA NI SAWA NA KUTOFAHAMU KABISA! KUJIFUNZA BILA YA KUTENDA NI SAWA NA KUTOJIFUNZA KABISA!

Nimeamua kutumia maneno haya makali kutoka kwa mwandishi Stephen R.Covey katika kitabu chake “The 8th Habits of highly effective people” ili kukumbushana kuhusu masuala muhimu katika elimu na utendaji.
Picha kutoka:www.vpi-inc.com

Nikizingatia mfumo mzima wa elimu, ambao umetuandaa kuwa waajiriwa na si kutumia ufahamu na ujuzi tuliosomea kujiajiri na ikiwezekana kuajiri wengine ni muhimu sana kutafakari na kuwa na mtazamo mwingine.
Utakubaliana na mimi kuwa wafanyakazi wengi nchini Tanzania wanafanya kazi nje ya taaluma zao.Lengo kubwa hapa ni kuangalia maslahi, wakati huo huo wakiweka pembeni ubora na tija katika utendaji. Hapa tunapata tatizo la kushuka kwa ubora wa huduma mbali mbali, hivyo kushusha pato la Taifa.
Imezoeleka kuwa, ili mtumishi apande cheo au kupanda ngazi ya mshahara, ni lazima aende kusoma zaidi.Swali la kujiuliza, je wanachoenda kukisomea wanakitumia kuboresha utendaji?...jibu unalo msomaji. Hapa nitarejea maneno yale yale…kujifunza bila kutenda ni sawa na kutojifunza kabisa!
Kuna ugonjwa mkubwa sana katika Taifa hili, hasa kwa wafanyakazi au waajiriwa kupenda kufanya kazi kwa mazoea na si kutumia taaluma.Wengine wamebaki kunung'unika bila ya kuchukua hatua kwa kufuata utaratibu unaostahili.
Kuna tatizo jingine, hasa kwa wahitimu kutoka vyuoni, utamwona “graduate” anajitamba na vyeti vyake kuwa anafahamu mambo mengi kuhusiana na taaluma yake.Lakini tukimwambia onyesha uwezo wako katika utendaji…mh! Ni shida kubwa.
Ningependa kuwafumbua macho vijana wengi waliomaliza vyuo.Katika kipindi hiki cha mabadiliko makubwa ya uchumi yanayochochewa na Sayansi na Teknolojia ni muhimu kuwa mtendaji na si mtu wa kufahamu peke yake.
Kama malengo yako ni kuajiriwa basi tambua kuwa unatakiwa kuwa mchangiaji wa ubora katika kampuni au sekta fulani. Ukikosa kuwa na mchango wa ubora katika kampuni au sekta hiyo basi ujue utakosa kazi au kupewa ujira usiolingana na ndoto zako.
Mwandishi na msemaji maarufu wa hadhira-Jim Rohn aliwahi kusema “people get paid by bringing value to the market place” akimaanisha, “watu hulipwa ujira kulingana na ubora wa kazi waletao kwenye soko, tunapozungumzia soko inamaanisha uhitaji katika jamii.

Naomba nikuache na usemi kutoka kwa Raisi wa 26 wa Marekani Theodore Roosevelt alisema:
 "Great thoughts speak only to the thoughtful mind, but great actions speak to all mankind."-Mawazo makuu au fikra kubwa hueleweka kwa walio na upeo wa kufikiri, bali matendo makuu hueleweka kwa kila binadamu"

Imeandaliwa na Henry Kazula,
Jielimishe Kwanza!