inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 25 Mei 2013

MAZINGIRA: ONGEZEKO KUBWA LA HEWA UKAA DUNIANI!!!

Utafiti uliofanywa na wanasayansi katika maabara ya serikali nchini Marekani huko Hawaii zimethibitisha kuwepo kwa ongezeko kubwa zaidi la hewa ukaa duniani kufikia mia nne kwa milioni moja ya sehemu za dunia. Ongezeko hili ni la kwanza kihistoria.

Wakiripoti kupitia BBC Swahili, walieleza kuwa ongezeko hilo liliwahi kutokea miaka milioni tatu hadi milioni tano iliyopita ambapo ilikuwa chini ya mia nne kwa sehemu milioni moja za dunia(400ppm).

Wanasayansi hao wamebaini kuwa kuna sababu mbali mbali zinazochangia ongezeko la hewa ukaa duniani, hasa ni hewa ukaa itokanayo na gesi inayotengenezwa na binadamu.

Hii ikimaanisha kuwa ongezeko kubwa la idadi ya watu limepelekea ongezeko kubwa la hewa ukaa.

Vile vile, walibaini kuwa ongezeko kubwa la hewa ukaa limepelekea kuongezeka kwa joto duniani mara dufu.

__________________

Gesi kutoka viwandani katika kuchangia ongezeko la hewa ukaa.                                     www.rose-kajivo.blogspot.com

Nikiungana na sababu moja ya kuwa binadamu ndiye chanzo cha ongezeko la hewa ukaa duniani na nyingine ambazo hazikuanishwa, naweza kusema kubwa ni shughuli za binadamu hasa ongezeko la viwanda duniani vinavyotoa hewa ukaa kwa wingi, utumiaji wa magari na motokaa hasa yale mabovu.

Sababu nyingine ni uharibifu mkubwa wa misitu ambayo kisayansi ina mchango mkubwa sana katika kupunguza hewa ukaa kupitia mfumo wa utengenezaji wa chakula.

Uharibifu wa mazingira unachangiwa sana na umasikini uliokithiri hasa katika nchi za Afrika.Pia kubadilisha maeneo la misitu kuwa makazi ya kudumu.

Kukata miti kama kuni kwa matumizi ya nishati www.lukwangule.blogspot.com




 

Juhudi za makusudi zinapaswa kuchukuliwa na hasa zinaanza na usimamiwaji mzuri wa sera na sheria na kanuni za kila nchi kuhusu utunzaji wa mazingira.

Ukiangalia kwa kina kuhusu chanzo cha tatizo, kinahusu nchi zilizoendelea(kupitia viwanda vikubwa na utumiaji wa magari na motokaa) na nchi zinazoendelea (ukataji wa miti kwa matumizi ya nyumbani kama nishati ya kupikia, magari mabovu na yenye kiwango cha chini).

Tunaweza pia, kuanzia hapo, hasa kwa kubadilisha gesi za viwandani kwa matumizi mengine na si kutupiwa angani.Kupunguza matumizi ya motokaa na magari binafsi hasa yale mabovu na yaliyo chini ya kiwango.

Tunaweza kupunguza matumizi ya magari

                              www.do4five.co

Tuhamasishe upandwaji wa miti kila mahali panapostahili na kuzuia ukatwaji wa miti usikuwa na tija.Ni vyema kuyaboresha maeneo kama mashimo yaliachwa kwa shughuli mbali mbali kuwa misitu.

Tukumbuke kuwa, mabadiliko ya kuifanya dunia yetu kuwa sehemu nzuri ya kuishi yanaanza na mtu mmoja.

 

 

Na Henry Kazula.

Jielimishe Kwanza! Chukua hatua...

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni