inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 29 Mei 2013

MALEZI NA FAMILIA:HIZI NI TABIA ZA AWALI KABISA KWA MTOTO/KIJANA ANAYEANZA KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA!

Jumanne, 14 Mei 2013 niliandika makala kuhusu utumiaji wa madawa ya kulevya kwa vijana. 

http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/05/vijana-matumizi-ya-madawa-ya-kulevya.html


Picha kutoka:blog.stopyouraddiction.com


Sambamba na makala hiyo, napenda kutoa angalizo kwa wazazi na walezi kuhusu tabia na mwenendo wa watoto na vijana wao.

Wataalamu wa masuala ya afya wanasema "kinga ni bora kuliko tiba."Hivyo ni vyema kufahamu mabadiliko ya tabia kwa watoto/vijana na kufanyia kazi mapema.

Tafiti mbali mbali zimeainisha kuwa vijana na watoto hubadilika ghafla kitabia pale tu waanzapo kutumia madawa ya kulevya.

Zifuatazo ni tabia na ishara za awali na za wazi kwa mtoto/kijana anayeanza kutumia madawa ya kulevya;

1. KUJITENGA NA WANAFAMILIA

Mtoto/kijana hupenda kujitenga na wanafamilia kwa kujifungia chumbani, pia hujitenga katika suala la mlo wa pamoja; kwa kifupi hupenda kula peke yake.Pia hukwepa kujihusisha na masuala mengine ya kifamilia;
Ni vizuri kulitazama badiliko hili la tabia na kulifanyia kazi bila kuchelewa. 

2.KUJIHUSISHA NA MAKUNDI MAOVU

Picha kutoka:http://alcoholism.net/alcohol-abuse/alcohol-abuse
Utashangazwa kumuona mtoto wako akiwa na marafiki waovu na wasio na mwelekeo wa maisha, hapa kuwa makini, chukua hatua.

 Badiliko hili la kitabia huambatana na kuongezeka kwa tabia ya ugomvi inayoendana na kulipa visasi.

3.KUJIAMINI KUPITA KIASI

Mtoto/kijana hubadilika kitabia, kwa kujiona na pia kuona kuwa hakuna kitu kinachomshinda kwenye dunia hii, na hugeuka kabisa kutokubali kushauriwa na mtu yoyote   kuhusu maisha yake.

4 .KUJIBIZANA NA WAZAZI/WALEZI BILA HOFU

Kutokana na sababu ya (3), utashangazwa sana kumuona mtoto/kijana wako akikujibu majibu ya hovyo pale unapomweleza mambo ya maana kuhusu maisha yake.Katika hatua hii kuwa makini sana, unaweza kujikuta unapata "stroke" kwa kuona mtoto/kijana wa kumzaa anakudharau kupita kiasi!

5.KUOMBA PESA MARA KWA MARA

Kutokana na kuongezeka kwa matumizi na uhitaji wa madawa ya kulevya katika mfumo wa fahamu, mtoto/kijana wako atakuwa mhitaji mkubwa wa madawa hayo ambayo yanauzwa.Ukijaribu kumuuliza atakwambia kuna vitu anataka kununua.

6.KUIBA VITU VYA NYUMBANI NA KUUZA

 Endapo mtoto/kijana atashindwa kupata pesa ya kununulia madawa ya kulevya, usishangae kuona vitu vinapungua nyumbani na kuelekea kusikojulikana.Hapa fanya uchunguzi na uchukue hatua.

Kipindi kingine nitaeleza jinsi ya kumsaidia mtoto/kijana aliyapatwa na janga hili!

Lakini tusisubiri tiba ilihali dalili tunaziona, mzazi/mlezi usichukulie mabadiliko hayo kama kitu cha kawaida... 

Jielimishe Kwanza!

Masomo zaidi:




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni