inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 31 Mei 2013

UJASIRIAMALI NA VIJANA: WAZIRI WA UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI DK. MARY NAGU AFUNGA RASMI MAFUNZO YA WAHITIMU (40)WAJASIRIAMALI LEO !

Leo imekuwa ni siku ya kilele cha mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana-wahitimu wa vyuo vikuu mbali mbali nchini.

 

Mafunzo hayo yaliyowashirikisha vijana 40, yameongeza chachu kwa vijana hao hasa katika kuwajengea uwezo wa kuandika mipango ya kibiashara,uwezo wa kujiajiri na kuweza kuajiri wengine.

 

Kwa kushirikiana na chuo kikuu Dar es salaam, kitengo cha ujasiriamali, Baraza la uwezeshaji la Taifa kiuchumi limeweza kufanikisha mafunzo hayo na kuwatunuku wahitimu 40 vyeti katika Hotel ya Blue Pearl Hotel, ukumbi wa Crystal Hall-Ubungo Plaza, jijini Dar es salaam leo.

 

Zoezi hilo liliambatana na utolewaji wa zawadi kwa washiriki watatu(3) waliofanya vizuri katika zoezi la uandikaji miradi ya biashara.

 

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, akiwa mgeni rasmi alipewa nafasi kuwatunuku vyeti wahitimu hao  na zawadi kwa washindi watatu(3) ambao ni Bw. Anthony Seleli Mhanda aliyepata sh.milioni 10, Bw. Ale Alex Kaaya aliyepata sh.milioni 8 na , Bi Selina Julius Otacho aliyepata sh. milioni 6.

 

Mwisho kabisa Dr. Nagu alitoa hotuba fupi kwa wahitimu na umma kwa ujumla wake.Aliwapongeza wahitimu kwa kuthubutu kuchukua uamuzi wa kujiajiri na ofisi yake haitawaacha, itashirikiana nao kuhakikisha mafunzo waliyoyapata yanazaa matunda.

 

Aliainisha kuwa, katika nchi yetu kuna makundi matatu ya mifumo ya kujipatia mkate wa kila siku; kundi la kwanza ni la watanzania wanaobangaiza bangaiza-wanabahatisha maisha, la pili ni lile la waajiriwa na wachacharikaji ingawaje kipato chao ni kidogo na hakikidhi, kundi la tatu ni la wajasiriamali-kundi hili lina watu wachache, ni watu wenye kuona fursa na kuzitumia ikiwa sambamba na kutengezea vyanzo vingine vya ajira.

 

Alishauri kuwa, imefika wakati kwa watanzania kuhamia katika kundi hili la tatu ambalo linakwenda kuongeza idadi ya ajira na kukuza uchumi wa kila mtu na si kutegemea kukua kwa uchumi wa Taifa. Akimaanisha kuwa; uchumi wa mtu mmoja ukikua, wa Taifa utakua.

 

Ilitaadharisha kuwa kukua kwa uchumi wa Taifa si kiashiria kizuri cha kukua kwa uchumi wa mtu mmoja.Hivyo watu wasijidanganye na kutegemea kukua kwa uchumi wa Taifa ila inapaswa wananchi wenyewe, mmoja mmoja achukue jukumu la kukuza uchumi wake ili uchumi wa Taifa ukue.

 

Dr.Nagu alikazia kwa kusema; ukosefu wa ajira kwa vijana nchini unatokana na kutegemea kuajiriwa katika sekta rasmi...

 

PICHA NA MATUKIO:

Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakiwa katika ukumbi wa mkutano

 

Henry Kazula, akitunukiwa cheti cha mafunzo ya ujasiriamali
Waziri, Dk.Mary Nagu akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wa mafunzo ya ujasiriamali


Waziri, Dk.Mary Nagu akijadiliana na wahitimu wa mafunzo ya ujasiriamali







Henry Kazula (wa kwanza kutoka kushoto), akiwa na wahitimu wenzake

Imeandikwa na Henry Kazula,

Mshiriki wa mafunzo ya ujasiriamali,

Mkurugenzi mtendaji;

1.Jielimishe Kwanza!

2."Science and Fine arts Resource Centre (SFRC)"

 

Kampuni inayokwenda kutoa elimu ya masomo ya sayansi(Baolojia,Kemia na Fizikia) na uchoraji kupitia mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) au kwa kiingereza Information Communication Technology (ICT).

 

Ukiwa mdau wa elimu na unayependa utolewaji wa elimu bora  na inayozingatia mabadiliko ya teknolojia kwa vijana unaweza kuwasiliana na Henry Kazula kupitia: 

 

Simu ya mkononi:

+255 754 572 143/ +255 716 o75 826/ +225 785 175 157.

Barua pepe:jielimishekwanza@gmail.com

Imetolewa na

Jielimishe Kwanza!

(2013).


 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni