inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 13 Juni 2013

VIJANA NA MAISHA: JIFUNZE KUTAMBUA, KUCHAGUA NA KUISHI KWA UTHUBUTU WENYE TIJA...




Picha imetolewa www.alidavies.com
Kwa kipindi kirefu vijana tumekuwa tukilaumiwa kuwa ni waoga kuchukua hatua ya uthubutu kwa masuala mbali mbali ya kujiongezea kipato hasa kuwa wajasiriamali.

Wataalamu wa masuala ya uchumi na biashara wamemtambua mtu aitwaye mjasiriamali kuwa ni mtu anayechukua hatua ya uthubutu wenye tija, ulio na uwezekano wa hatari bila hofu ya kupoteza.

Pia yupo tayari kwa lolote litalotokea ilihali ana nia ya kutumia fursa iliyopo kujiongezea kipato chake na ikiwezekana kutengeneza milango ya fursa ya kipato kwa wengine.

Kuna sababu mbali mbali zinazowafanya vijana kuchukua muda mrefu, hasa katika suala zima la uthubutu; hofu ya kupoteza kile kidogo walicho nacho,hofu ya kukataliwa na kutengwa na marafiki au ndugu, kutegemea faida ya papo kwa hapo(wengi si wavumilivu wa mafanikio…kila mmoja anataka mafanikio ya haraka).

Swali, tunatokaje hapo tulipo kuelekea kwenye hatua a uthubutu wenye tija unaoendana na ujasiriamali?

Kabla ya kutoa mbinu za kutumia ili kufanikiwa kwenye uthubutu wenye tija ni muhimu kufahamu kuwa suala la uthubutu linaambatana na kukutana na uwezekano wa hatari, kwa lugha ya Kiingereza hujulikana kama “risk”. 

Hivyo,ni muhimu kujifunza jinsi ya kupunguza uwezekano wa hatari hizo.

Daktari maarufu wa masuala ya ubongo na neva za fahamu, nchini Marekani-Dk.Ben Carson, katika kitabu chake cha 
“Take The Risk” ameainisha njia ya kufuata kuelekea kuchukua hatua ya uthubutu wenye uwezekano wa hatari. 

Awali ya yote, amesema “katika maisha kila kitu kina uwezekano wa hatari ndani yake”…mfano mdogo tu, unapotembea kuna uwezekano wa hatari kutokea, unaweza kugongwa na gari, baiskeli,guta,pikipiki au ukiwa unaendesha gari kuna uwezekano wa kupata ajali.Uwezekano wote huu wa kupata hatari hauwafanyi watu kuacha kutembea kwa mguu au kuendesha au kuendeshwa kwenye magari.

Dk. Carson ameainisha njia mbili lakini ni nne ndani yake zilizo sanjali na kujiuliza maswali;

·      Ni kitu gani kizuri kitatokea kama nikifanya?
·      Ni kitu gani kizuri kitatokea kama nisipofanya?

·      Ni kitu gani kibaya kitatokea kama nikifanya?
·      Ni kitu gani kibaya kitatokea kama nisipofanya?

Kwa uzoefu na umahiri wake katika upasuaji wa ubongo na neva za fahamu Dk.Carson amekuwa akitumia njia hii ya kujiuliza maswali hayo manne.Pia, unaweza kuyatumia maswali haya katika mazingira mbali mbali yanayohusu kutoa maamuzi magumu.

Hivyo basi msomaji ni vizuri kujiuliza na kupata majibu ya maswali yote manne kabla ya kutoa maamuzi yaliyo katika njia panda.

Jielimishe Kwanza!
Tenda! Ishi Ndoto!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni