inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 18 Juni 2013

UONGOZI BORA: HII NI SIRI KUBWA YA VIONGOZI WALIOFANIKIWA…

Raisi,(1994-1999), Mwanamapinduzi,Mpigania haki kuhusu ubaguzi wa rangi wa Afrika Kusini-Nelson Mandela.         (Picha na www.newstimeafrica.com). Picha hii imewekwa kwa kuthamini mchango wake, ni mfano wa kiongozi bora wa kuigwa, pia kumtakia heri.

Wataalam wa masuala ya uongozi wamekuwa wakijiuliza swali lifuatalo mara nyingi; viongozi huzaliwa au hutengenezwa? Ikimaanisha-ni mtu tu anajikuta kazaliwa ana uwezo wa kuongoza au anafundishwa kuwa kiongozi?

Mtazamo wa wengi ni kuwa viongozi wanazaliwa…ni kipaji tu cha mtu cha kuzaliwa nacho.Yaani, wakichukulia kuwa tangu kipindi cha utoto utaiona tabia ya mtoto akiwaongoza wenzake katika michezo ya kitoto.

Pia, kiasilia kunapokuwa na watu zaidi ya wawili na wanahitaji kutoa maamuzi ya pamoja utaona kuwa mmoja hujiweka kipaumbele katika kutoa maamuzi na anakubalika.

Mwandishi maarufu, Stephen R.Covey katika kitabu chake cha “The 8th Habit- From Effectiveness to Greatness” anapingana na mawazo ya wengi kwa kuweka msimamo hasi…akimaanisha kuwa viongozi hawazaliwi wala hawatengenezwi ila mazingira huwafundisha na kuwalea.

Akiunganisha na wazo la uwezo wa asili wa mwanadamu…Stephen anasema; "kikawaida mwanadamu ana nguvu ya asili ya kufanya chaguo."

Hivyo basi, akasiliba kwa kusema "viongozi hujitengeneza kwa kuchagua wenyewe", na endapo watafuata kanuni na kujiongezea nidhamu dhabiti, uhuru wao wa kuchagua huongezeka.
Akithibitisha ukweli wa wazo lake Stephen kwa kulinganisha na wazo la Dk.Noel Tichy ambaye alisema;viongozi hawazaliwi ila hufundishwa…Stephen anaunganisha mawazo kwa kusema; watu hutumia nguvu yao ya kuchagua kujifunza na kufuata mafunzo.

Tukifuatilia kwa makini orodha ya viongozi wenye mafanikio duniani ni kubwa.Nikisema nianze kumjadili mmoja hadi mwingine itachukua muda mrefu sana bila ya kumaliza.Ila viongozi wote hawa walikuwa na tabia/wana tabia za kipekee na zinazofanana ambazo ni;
1.   Kuwa na maono”vision” ya mbali yenye tija na kuyafanyia utekelezaji, ambayo wengine (wafuasi) hawayaoni. Mtaalamu wa masuala ya uongozi na mwandishi aliyebobea nchini Marekani Warren Bennin alisema, “uongozi ni kubadilisha maono kuwa uhalisia”

2.     Hutenda kwa kufuata dhamiri “conscience”…hutenda kwa kufuata sauti ya moyo ya ndani inayomfanya mtu kutofautisha jema na baya. Kama Stephen Covey anavyosema; “Sauti hii ya ndani ni tulivu na ya amani. Pia inahusisha kujitoa mzima mzima kwa jambo jema tarajiwa…Ni hii dhamiri inayotafsiri maono kuwa huruma kwa wengine.”

3.     Huwa na shauku”passion” kubwa ya kutenda.Hii hutoka moyoni. Nikimnukuu mjasiriamali mwenye mafanikio na mwandishi wa vitabu Anthony Robbins anasema; "There is no greatness without a passion to be great, whether it's the aspiration of an athlete or an artist, a scientist, a parent, or a businessperson." Akimaanisha kuwa hakuna ukuu au umaarufu unaokuja bila ya shauku ya kuwa mkuu au maarufu, si ndoto ya kuwa mwanariadha au msanii, mwanasayansi, mzazi au mfanyabiashara.Haya yote yanaanza na kuwa na shauku.

4.     Nidhamu”discipline” kwao ni silaha.Kama alivyosema raisi wa  26 wa Taifa la Marekani  Theodore Roosevelt alisema; “kila kitu kinawezekana kwa kuwa na nidhamu binafsi”

5.  Ukifuatilia mafundisho au hotuba zao, huongea na hisia za watu kwa kugusa mioyo. Hupangilia maneno yao si kwa kujifurahisha wenyewe, bali kugusa hitaji la ndani la mioyo ya wengine. Kwa mantiki hiyo, wafuasi hupenda kuwasikiliza na kutendea kazi mawazo na mafundisho yao.

Bila shaka umepata kujua kuwa kila mtu anaweza kuwa kiongozi.Pia ni suala la kuchagua kujifunza na kufuata kanuni za uongozi bora na si bora kiongozi.

Jielimishe Kwanza!
Tutumie maoni yako
Barua pepe:jielimishekwanza@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni