inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 10 Julai 2013

UCHUMI: IKIWA UNAPATA PESA NYINGI HALALI LAKINI HUELEWI ZINAKOKWENDA FANYA YAFUATAYO:


Kumekuwa na msemo uliozoeleka na kuaminika na watu kuwa "raha ya pesa ni matumizi" au "tumia pesa ikuzoee" ... ni kweli kabisa pesa inaendana na matumizi lakini ni vyema kuweka angalizo: zingatia aina ya matumizi unayofanya.

Jiulize "Je, matumizi ninayofanya yanakwenda kubadilisha maisha yangu na kunifanya niwe na fedha zaidi au yananipelekea kwenye umasikini wa kutupa?

Watu wengi wanajishangaa...wanapata fedha nyingi lakini hawaelewi zinakokwenda huku wakati huo huo ndoto zao hazitimii na hali zao za maisha zikizidi kuwa duni bila mabadiliko kila mwaka.
 ________________________________________ 


Kama huelewi fedha zako zinakokwenda fanya yafuatayo:

1.EPUKA MADENI
Jaribu kufuatilia kwa karibu ni kiasi gani cha pesa kinaenda kwenye madeni utapata jibu kuwa ukiyaepuka madeni utaiona pesa yako.Hii ni njia ya haraka ya kuhifadhi pesa yako

2.JIWEKEE MPANGO WA KUTUNZA PESA
Ni rahisi sana kufanya mpango huu kwa malengo ya muda mfupi.Mfano unataka kununua samani za ndani, fuatilia na ujue itakugharimu kiasi gani cha fedha.

Pia kama unataka kununua au kujenga nyumba fanya utafiti na ujue itakugharimu kiasi gani cha fedha kwa nyumba unayoitaka...ni muhimu uwe na ramani ya nyumba yako mapema itakusaidia kukokotoa gharama ya nyumba, hivyo kuanza mpango wa kutunza fedha, mwishowe kuanza kwa hatua moja hadi nyingine.

Kwa malengo ya muda mrefu hasa kustaafu, inabidi ujue na ufanye mpango yakinifu kujua ni kiasi gani cha fedha utahitaji kukufanya uishi bila kutegemea watoto kwa kipindi cha miaka 20-30 baada ya kustaafu au kuacha kufanya kazi, pia unatakiwa kujua aina ya uwekezaji utakaotimiza malengo yako.

3.WEKA KIKOMO CHA MUDA KUTIMIZA UHITAJI WAKO
Mfano: Unaweza kusema kwa dhati kuwa “Nataka kununua gari ndani ya miaka miwili kuanzia sasa”.

Weka kimaandishi siku maalumu kwa tarehe kutimiza malengo ya muda mfupi na uhakikishe malengo yako yanafikiwa ndani ya muda husika.

Ujue fika kuwa usipoweka lengo linaweza kufikiwa utakata tamaa hivyo kutumia pesa ovyo kwa kitu ukipendacho kwa wakati husika bila ya kupanga.

4.JICHUNGUZE NI KIASI GANI CHA FEDHA UNATAKIWA KUTUNZA KWA WIKI,MWEZI AU KWA KILA MSHAHARA KUTIMIZA MALENGO YAKO
Ainisha vitu unavyovitaka na gharama yake, hivyo amua ni kiasi gani cha fedha unatakiwa kutunza kuanzia sasa.

Kwa mafanikio mazuri ni vizuri kutunza kiwango kile kile cha pesa kwa muda uliojipangia. Mfano: Unataka kulipia kodi ya nyumba Shilingi 1,800,000 kwa mwaka, utahitaji kujiwekea akiba ya Shilingi 150,000 kwa kila mwezi.

Kuanzia hapo linganisha na kipato chako kwa mwezi, kama nacho ni Shilingi 150,000 kwa mwezi itakuwa vigumu sana kutimiza mahitaji mengine ya msingi.

5.WEKA KUMBUKUMBU YA MATUMIZI YAKO
Jichunguze umetumia kiasi gani cha fedha na umeingiza kiasi gani fedha kwa siku au mwezi kwa maandishi.Jitahidi kuwa makini uwezavyo kujichunguza matumizi yako na usipuuze wala kuacha kuandika matumizi madogo.Ukiweza kusimamia matumizi yako, utakuwa makini sana na pesa yako.

Tenga kwa makundi kama Kodi ya pango,Bima ya gari, nauli,gharama za simu,gesi,chakula,burudani, gharama za ving’amuzi na mengineyo.
·      Jiwekee utaratibu wa kutembea na kidaftari kidogo kwa ajili ya kumbukumbu zako za matumizi.
·      Mwisho wa wiki kaa,tulia,tafakari na uchukue risiti za manunuzi na hamisha kumbu kumbu za matumizi yako kwenye daftari kubwa  la matumizi
·      Pia unaweza kutumia simu yako kutunza kumbukumbu za matumizi yako

6.EPUKA MATUMIZI YASIYO YA LAZIMA
Ukichunguza vizuri matumizi yako kwa wiki au mwezi utashangaa mwenyewe kuona kuwa kuna wakati umefanya matumizi yasiyo ya lazima…ambayo hayakuwepo kabisa kwenye mpango wako.

Ukilinganisha na kiasi cha fedha unachohitaji kwa malengo uliyojiwekea unaweza kufanya maamuzi magumu ya kujibana kimatumizi.Fikiria sana vipaumbele vya malengo yako.

7.CHUNGUZA LENGO LAKO LA KUJIWEKEA AKIBA
Unaweza kufanya hesabu rahisi kwa kutoa gharama za matumizi kutoka kwenye kipato chako halisi(baada ya makato mbali mbali …kama ni mwajiriwa).Vipi tofauti yake? Je inashabihiana na lengo la kujiwekea akiba?

8.ANDIKA BAJETI YAKO
Ukifanikiwa kusawazisha kipato chako na malengo yako ya kujiwekea akiba na matumizi andika bajeti itakayokuwezesha kujua kila mwezi ni kiasi gani cha fedha utatumia.

9.USILIPE KWA MKOPO, WALA KWA KUTUMIA “CHECKS”-LIPA FEDHA TASLIMU!
Ni rahisi sana kuongeza matumizi zaidi ya malengo yako kwa mtindo wa mkopo.
Ukilipa pesa taslimu utaona jinsi mfuko wako unavyopungua hivyo ni rahisi kujidhibiti na matumizi yako.

10.FUNGUA AKAUNTI YA AKIBA YENYE ZAO LA FAIDA
Ni vyema kuwa na akiba inayotengeneza faida kwa kipindi fulani cha muda.

11.KUWA WAKWANZA KUJILIPA
Katika kipato chako usisahau kujipa mwenyewe hasa kwa jitihada zako, muda uliotumia kuzalisha.Hii ni njia nzuri kwa wafanyabiashara, mara nyingi hujisahau kabisa kuwa jitihada zao na muda waliotumia ni wa thamani sana hivyo wanapaswa kujilipa kwanza.

12.USIFANYE “WINDOW-SHOPPING” UKIWA NA PESA MFUKONI
Utajikuta umetamani kitu fulani na kushawishika kununua bila ya kuwa na malengo ya awali.

13. USIKATE TAMAA, ANZA SASA!
Jiamini kuwa unaweza kufikia malengo yako na kuwa mtu mwenye fedha nyingi kwa kujikita kikamilifu katika suala zima la kujiwekea akiba.

Kama Waswahili wasemavyo; mambo mazuri hayataki haraka-wakimaanisha huchukua muda hivyo basi jinsi unavyojiwekea akiba ndivyo faida inavyokuwa kubwa na utajiri kukunyemelea.

Makala inayohusiana:
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!