inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 13 Julai 2013

ZOEZI LA KUTUNUKU TUZO KWA VIJANA CHINI YA MIAKA 30 KWA MWAKA 2013 LAZINDULIWA JIJINI DAR ES SAALAM LEO...

Shirika lisilo la kiserikali Youth for Africa (YOA)” kwa kushirikaiana na TCRA,uhuruone,Clouds FM,Bongo 5,Caravan Records,KINU,onspot magazine,Coca Cola Hussein, Africa 2.0 limezindua zoezi la kutunuku tuzo maalum zijulikanazo kwa lugha ya Kiingereza “Under -30 YOUTH AWARDS 2013” ikiwa ni mwanzo tu wa tukio hilo kubwa linayotarajiwa kufanyika tarehe 17/08/2013.
 
Tuzo zimeandaliwa rasmi kwa vijana waliothubutu na kufanya vizuri katika nyanja za ujasiriamali, Uandishi wa habari, mchango kwa jamii, Sanaa na Ubunifu, Mitindo,Muziki na Burudani, Uvumbuzi na Michezo.

Uzinduzi huo ulishirikisha wadau mbali mbali wa masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano uliongozwa na mgeni rasmi Mhe.January Makamba(MB).

Mhe.Makamba alisisitiza kuwa ni vyema YOA na wadhamini wa tuzo hizo kuweka utaratibu wa kuwatambua vijana ambao hawahamiki na wanafanya vizuri katika nyanja mbali mbali za ubunifu na ujasiriamali na kuwafikia mahali popote nchini Tanzania.

Mhe.January Makamba(MB) akizindua rasmi zoezi la utoaji tuzo kwa vijana wenye umri chini yamiaka 30.

Zoezi zima liliambatana na kutunuku vyeti kwa washiriki wa waliofanikiwa katika hatua ya awali kushiriki kinyang’anyilo hicho.Kama ilivyo ada Mhe. January Makamba (MB) aliwatunuku vyeti washiriki.

Shughuli nzima ya kuwapata washindi wa tuzo itahusisha wanajamii wote kwa kupiga  kura kwa mshiriki husika kupitia ujumbe mfupi wa simu ya mkononi kwa kuandika YOA kwenda namba 15584...ujumbe huo mfupi utatozwa Tsh. 200.

PICHA: UTOLEWAJI WA VYETI KWA WASHINDANI WA TUZO








PICHA ZA PAMOJA

Wakiwa katika nyuso za furaha ni washindani wa tuzo wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe.January Makamba (MB).

Wadhamini wa tuzo "Under 30 Youth Awards 2013" wakiwa na Mhe.January Makamba

Jopo zima la YOA wakiwa na Mhe.January Makamba(MB)




Tushirikiane kwa pamoja kufanikisha zoezi hili ili iwe chachu ya mabadiliko ya kiuchumi  yaliyo na  tija kwa vijana na Taifa kwa ujumla.

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni