inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 15 Julai 2013

KAZI NA UTENDAJI: TAALUMA YAKO ISIWE KIZUIZI CHA KUTIMIZA NDOTO YAKO…UNAWEZA KUTIMIZA NDOTO YAKO NJE YA TAALUMA YAKO!


Picha na www.techtricksworld.com
Nikirejea makala iliyopita kuhusu elimu na utendaji: http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/05/elimu-na-utendaji.html niligusia suala la kufanya kazi nje ya taaluma mtu aliyosomea kutokana na uhaba wa ajira, hivyo mtu kujikuta anafanya kazi yoyote bora mradi kujipatia mkate wa kila siku.

Picha na www.secrets-2-success.com
Kiuhalisia watu wanafanya kazi nje ya kile walichokisomea na nje ya dhamiri (passion) zao, hivyo hufanya kazi bora mradi tu wapate kipato.
Ndani ya mioyo yao wana ndoto kubwa zinazowajia kila siku, zilizo sanjari na vipaji vyao, pia wakiwa na shauku kubwa ya kuzitimiza ndoto hizo lakini majukumu ya kazi yanawabana kiasi kwamba wanashindwa kutimiza ndoto zao.

Je, wewe pia upo katika kundi la watu wanaotaka kuwafurahisha mabosi wao kwa kufanya kazi kwa bidii bora mradi wapate mkate wao wa kila siku? Au upo kwenye kundi la wale wanaosema;
·      “yaani hii kazi…mh! Nafanyia shida tu!”
·      “nafanya kazi bora mradi mkono uende kinywani”
·      nafanya kazi hii kwa sababu mzazi wangu amesema niifanye…lakini siipendi”
·      nafanya kazi hii kwa sababu ajira ni ngumu sana…ila nasogeza siku tu!
Huna sababu ya kunung’unika…fuata dhamiri yako na kile moyo unapenda kwa sababu utakifanya kwa ufanisi, ukiwa huru, pia kutimiza malengo yako na ya wengine.Kama Steve Jobs- mjasiriamali, mwanzilishi na mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya "Apple Computers na Pixar Animation" alivyosema; Have the courage to follow your heart and intuition.They somehow already know what you truly want to become.Everything else is secondary”.

Kama wewe ni miongoni mwa watu (wafanyakazi) wanaofanya kazi kwa manung’uniko tajwa na una lengo la kufanya kile ukipendacho na kutimiza ndoto na dhamiri yako fanya yafuatayo:

1. Andika ndoto yako kwa maandishi mfano unaweza kuiweka katika mpango wa biashara
2. Jichunguze mbinu ulizonazo kufikia ndoto yako…unaweza kuongeza ujuzi kwa kusoma vitabu  husika, pia kupitia mtandao wa internet (muulize mwalimu Google) atakuelekeza au fanya utafiti wa biashara yako
3. Tenga muda japo masaa mawili ya kufanyia kazi ndoto yako
4. Jibidishe mwenyewe zaidi kuliko unavyojibidisha kwa bosi wako-Jim Rohn.Jiwekee utaratibu wa kujifunza kwa hali na mali.
5. Tumia sehemu ya kipato unachopata kuweka msingi wa biashara yako

“Mfumo usikuzuie kutimiza ndoto yako, unaweza timiza ndoto yako nje ya mfumo”
Kwa ushauri zaidi, tuwasiliane.
Huduma ya ushauri ni bure!
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni