inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 6 Agosti 2013

MTAZAMO:UNAWEZAJE KUACHANA NA MAZOEA MABAYA?


Kila mtu ana mazoea ya jambo fulani, hasa baya kwa kufahamu au kutokufahamu.Kuna aina tofauti tofauti za mazoea mabaya. Leo napenda nikujuze aina zifuatazo za mazoea mabaya na mbinu za kuondokana tatizo hilo;

Watu wengi wamejikuta tu wameingia kwenye mkumbo wa kutumia vitu mbali mbali kama ulevi, uvutaji sigara na pia madawa ya kulevya kutokana na ushawishi wa marafiki na watu wa karibu.Bila shaka kila mtu anajua ni jinsi gani alivyoshawishika kuingia katika mkumbo huo na mwisho wa siku kujikuta ni mzoefu aliyebobea katika utumiaji wa vitu hivyo vibaya.
Kama msemo maarufu wa Kiswahili usemao “mazoea hujenga tabia” hivyo basi mazoea mabaya hujenga tabia mbaya.

Tunaondoka vipi hapo tulipo?


Picha na editionstv.com
Jielimishe Kwanza! imewahi kufanya mahojiano mbali mbali na watumiaji wa muda mrefu wa sigara,pombe na wengine wenye tabia zinazofanana na hizo kuhusu  utaratibu wa kuacha, wengi wao walisema wanataka kuacha ila hawawezi.

Leo naomba nikujuze mbinu mbadala za kuondokana na mazoea mabaya:


1.  Anza leo/sasa kujizuia kutumia vitu vibaya...ukihisi hamu ya kutumia vitu hivyo vibaya, tumia chakula,matunda au kinywaji kisichokuletea tatizo kama la awali (Taadhari! Anza kuacha kwa kupunguza idadi ya matumizi)

2.     Jenga uhusiano mwema na Mungu wako kwa kufuata amri zake

3.     Epuka makundi au marafiki wabaya

4.     Jaribu kushirikiana na watu waliofanikiwa kuacha matumizi ya vitu vibaya

5.     Tumia watu wenye tabia njema kukumbusha pale unapotaka kurudia mazoea mabaya

Tuungane kipindi kingine tujuzane kuhusu mbinu za kupambana na zoea jingine la 
"ULAJI MBAYA" ambalo kwa sasa limekuwa ni tishio kwa afya za watu wengi duniani.
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!