inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 5 Agosti 2013

MAZINGIRA: HII NDIYO SIRI YA USAFI WA MJI WA MOSHI


-->
Kwa kipindi kirefu mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro umekuwa kinara wa kudumisha usafi wa mji na makazi ikiwa ni sambamba na kujizolea tuzo za kutunza mazingira nchini na Kimataifa.

Kutokana na utafiti uliofanywa na Jielimishe Kwanza! umebaini siri ya mafanikio ya mji huo ili iwe mfano wa kuigwa kwa miji mingine nchini.Hii ndiyo siri;



Usimizi wa Dhati wa Sera na Sheria za mazingira



Kama ilivyoanishwa katika Sera ya Taifa ya mazingira ya 1997 ambayo inasisitiza umuhimu wa kutunga sheria za mazingira na sheria za Sekta hiyo, kitu ambacho ni cha lazima katika kusimamia ipasavyo  usafi mazingira na kustawisha uhai.


Sheria za mazingira zinazofaa na zenye maana ni lazima zieleweke sawa sawa na kuthaminiwa na jumuiya na watu wanaolengwa.

(Ukitaka kujua Sera ya Taifa ya mazingira ya 1997 soma kupitia NEMC.



Ni jambo linaloeleweka na kila mtu mjini Moshi kuwa hutakiwi kutupa taka ovyo, kukojoa ovyo kutema mate,au makohozi hadharani.Kinyume na hapo ni kutozwa faini isiyopungua Shilingi Elfu hamsini (50,000/=) na hili limesimamiwa kikamilifu.



Huu ni uthibitisho wa mahojiano mengine ya tarehe 24 Juni 2013 yaliyofanywa na http://www.ippmedia.com/frontend/?l=56280  pamoja na Afisa wa Afya wa Manispaa ya Moshi, David Kimaro ambaye alisema; 

sheria hiyo inasaidia halmashauri kupata mapato yatokanayo na faini kwa wanaochafua mazingira kupitia kampuni tatu za uwakala ambazo zinakusanya Sh, milioni 14.4 kwa mwaka.

Kampuni hizo kwa kutumia sheria ya usafi wa mazingira kumtoza faini ya Sh. 50,000 mtu yeyote anayekojoa hovyo, kutema mate, kutupa taka kama chupa za maji, magunzi, vichungi, sigara, maganda ya ndizi, vocha za simu ama kutiririsha maji.


Wageni wa mji huo ukijumuisha watalii wanajulishwa mapema kuhusu suala zima la usafi…tembelea vituo mbali mbali vya kusafirisha watalii utaona tangazo linalohusiana na Sheria hii kali kuhusu utunzaji wa mazingira.



Hivyo jihadhali uingiapo mjini Moshi.Pia huu uwe mfano wa kuigwa nchini kote, kama limewezekana Moshi kwanini iwe shida mikoa mingine nchini?

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!